Nenda ukajionee mwenyewe, mambo ya mvuto, wacha kuota ndoto mchana.Babu hana mvuto wowote ameshachuja kisiasa bora atafute shughuli nyengine.Dar inawenyewe wakina Lyatonga na Mtikila enzi hizo wlisukumwa mpaka magari yao compare na huyu mzee uone.Hajaweza kushawishi wala kukubalika Dar es salaam mjini.
Suala la itikadi lazima liwepo usitake kuhadaa wananchi wacha Chadema wachache toka nje ya Ukonga waje.Na usisahau kuleta picha kama zile za Iramba.
Tumesha sema huju JF na kwengineko kuwa, CHADEMA Dar hamna lenu.
Ni vyema nguvu kubwa muielekeze vijijini, kwani Dar tayari wameshaikataa CHADEMA siku nyingi ingawa makao makuu ya chama yapo hapa hapa Dar.
Baada ya kuona Dar ngumu kwa Chadema umeamua kusema ukweli wananchi waje bila kujali itikadi zao, teh teh teh,Ahsante sana kamanda Molemo kwa taarifa hii.
Mkutano wa Dkt. Slaa uwanja wa Kampala utaanza saa 10:00 alasiri. Wananchi wote wakazi wa jimbo la Ukonga cila kujali itikadi zao mnakaribishwa kutoa maoni yenu juu ya rasimu ya katiba mpya ya 2013!
Chadema Yatosha!
Mkuu,Suala la itikadi lazima liwepo usitake kuhadaa wananchi wacha Chadema wachache toka nje ya Ukonga waje.Na usisahau kuleta picha kama zile za Iramba.
HAMY-D, Hivi Ubungo siku hizi ipo Singida? maana ina mbunge wa Chadema, na kama Dar wamekataa Chadema tuone leo katika Mkutano CCM, CUF, TLP na vyama vingine waje kushangilia viongozi wa CHADEMA. Mara nyingine tunatoa hoja ambazo zinasababisha tunatiliwa shaka
Katibu mkuu wa Chadema Dr Wilbroad Slaa leo Jumamosi anatarajiwa kuhutubia mkutano mkubwa wa hadhara Dar es Salaam katika uwanja maarufu wa Kampala ulioko Gongolamboto.
Katibu wa Jimbo la Ukonga Juma Mwaipopo akizungumza na vyombo mbalimbali vya habari amesema Dr Slaa ataunguruma katika viwanja hivyo ikiwa ni maalum kwa ajili ya kukusanya maoni ya Katiba mpya.
Dr Slaa anatarajiwa kuambatana na Mjumbe wa Kamati Kuu Mabere Marando,Wabunge John Mnyika na Halima Mdee,Mkurugenzi wa sera na utafiti Mwita Waitara pamoja na viongozi mbalimbali walioko makao makuu.
Kwa siku za karibuni Chadema imekuwa ikipata ufuasi mkubwa jimboni Ukonga na hii ni kutokana na jimbo hilo kuwa kama vile halina mbunge kutokana na matatizo makubwa yaliyopo jimboni humo.
Kumekuwa na ubovu mkubwa wa miundombinu jimboni Ukonga hasa kipindi cha mvua ambapo nauli ya daladala imekuwa ikifika hadi shilingi 1000/-
Tayari kuna shamrashamra nyingi kusubiri ujio huo wa Dr Slaa ambaye ana mvuto wa kipekee nchini.
Ngebe za nini? mechi ya finali ni 2015. Takriban mwaka mmoja na nusu! Nani zaidi Dar----ccm au cdm......kama kutakuwa na fair play na marefa wataamua kwa haki wakitumia sheria zote 17 za mchezo bila shinikizo toka nje ya uwanja au kuruhusu uchakachuaji, ni dakika 90 tu za mchezo, mbabe atajulikana!!! Naona kuna wengine watalia baada ya mechi kwani hawaataamini kuwa hawako mioyoni mwa Watanzania!
Baada ya kuona Dar ngumu kwa Chadema umeamua kusema ukweli wananchi waje bila kujali itikadi zao, teh teh teh,
Mkutano wa Gongolamboto utikise Dar es Salaam? Wewe kweli msukule wa Dr.Slaa.Acha kutumia meya wa Dsm kufikiria we msukule. Wiki mbili tu zilizopita kata ya Ukonga tuliandaa mkutano ukafurika wananchi sasa unategemea akija Dkt. Slaa kiboko ya misukule itakuwaje? Kama ccm mnaweza kufanya hujuma ya mikutano ya Chadema ni kwingine lakini kwa Ukonga hamuwezi, we subiri tu muda si mrefu mtakimbia JF kwa aibu mtakayopata kufuatia wananchi kumwagika kwa wingi uwanjani.
Suala la katiba ni la watanzania wote kwahiyo tunawashirikisha wananchi wote watoe maoni yao. Sisi si sawa na ccm inayowalazimisha wanachama wake watoe maoni waliyokaririshwa ambayo ni msimamo wa chama.
Hivi Kawe kuna cha maana kimefanyika au ubungo? Acheni siasa za maji taka nyie CDM....come sun come rain Dar Ukonga hamuwezi pata kitu. Ni sawa na kusema mnapanga mikakati ya kulitwaa jimbo la Ilala lol hizo zitakuwa ndoto za alinachi.
CDM mnaoteza mda wenu bure Dar