NgomaNzito
JF-Expert Member
- Jan 10, 2008
- 559
- 28
Maisha lazima yaendelee na mabadiliko mengine yapo tu. Siku zote changamoto za mabadiliko huleta maendeleo kwa wenye mikakati mizuri ya kutumia mabadiliko hayoMwananchi iliripoti Jumamosi iliyopita kuwa wazee wa Chadema walikuwa wamepanga kukutana na Zitto ili wamuombe aondoe jina lake kwenye nafasi ya uenyekiti na kwamba, angepewa cheo cha katibu mkuu wa chama baada ya anayeshikilia nafasi hiyo, Dk Willibrod Slaa kuripotiwa kuwa anataka kujiweka pembeni na majukumu ya chama, ili awatumikie kwa karibu wananchi wa jimbo lake la Karatu.
Source: Mwananchi
Naona wanabodi wamekoomaa na issue ya Zitto lakini kuna pigo jingine Chadema kuachia ngazi kwa Dr Slaa la uendeshaji na utendaji wa Chama litakuwa na msukosuko mkubwa zaid kwa chama. Dr ni mtu anayeaminika sana kwa matamko yake kuhusu Chama sasa akiondoka naona itakuwa vigumu kuziba pengo hilo.
Nafasi hii akipewa Zitto anaweza kuvaa viatu hivyo??
Sioni tatizo kwa sababu anayosema Dr. siku zote ni maamuzi na msimamo wa chama sasa hata kama aking'atuka bado chadema itaendelea kusimamia mambo yake kama kawaida kwa kupitia katibu mwingine.Mwananchi iliripoti Jumamosi iliyopita kuwa wazee wa Chadema walikuwa wamepanga kukutana na Zitto ili wamuombe aondoe jina lake kwenye nafasi ya uenyekiti na kwamba, angepewa cheo cha katibu mkuu wa chama baada ya anayeshikilia nafasi hiyo, Dk Willibrod Slaa kuripotiwa kuwa anataka kujiweka pembeni na majukumu ya chama, ili awatumikie kwa karibu wananchi wa jimbo lake la Karatu.
Source: Mwananchi
Naona wanabodi wamekoomaa na issue ya Zitto lakini kuna pigo jingine Chadema kuachia ngazi kwa Dr Slaa la uendeshaji na utendaji wa Chama litakuwa na msukosuko mkubwa zaid kwa chama. Dr ni mtu anayeaminika sana kwa matamko yake kuhusu Chama sasa akiondoka naona itakuwa vigumu kuziba pengo hilo.
Nafasi hii akipewa Zitto anaweza kuvaa viatu hivyo??
Kimkakati kama Chadema watakuwa wamepanga Dr Slaa aache uenyekiti ili aende kugombea Urais na kama ikiwa kuna mkakati wa vyama vya upinzani kama ilivyowahi kuwa reported kwamba mgombea Mwenza atatoka CUF Zanzibar na walimtaja Hamad Rashid Mohamed, ambaye ni kiongozi wa upinzani Bungeni nadhani kutakuwa na changamoto kubwa kwa CCM na hiyo itawavuta CUF ambao walianza kupoteza nguvu bara kwa kuonekana kama wanagombana na Chadema.
Haya ni mawazo yangu na pia ni mawazo ya Watanzania wengi kuona CUF na Chadema, pamoja na tofauti zao wanakaa pamoja na kuchukua nchi. Kina Kibaki, Raila, Saitoti, Ruto na wengine, hawakuwa wakielewana na hawaelewani hadi sasa, lakini walifanya uamuzi kwa kufuata matakwa ya wananchi wao na wakaunda NARC ambayo ilichukua nchi. Ni Raila Odinga aliyetaja jina la Kibaki pale Uhuru Park (nilikuwapo) na alisema, "Kibaki atosha?" akaitikiwa "atoshaaaaa!!!" na yeye akasema, "basi tuacheni tukajadili na kuwatangazia" na baadaye wakajadili na kutangaza.
Kama kina Kibaki na Raila wangefanya tofauti, na kama Moi na wenzake wangezuia mkutano wa Uhuru, basi Kenya leo hii ingekuwa kama Rwanda na matukio ya uchaguzi yangekuwa mabaya zaidi ya yaliyotokea katika uchaguzi uliopita. Haya ni mawazo yangu na ninasema kwamba viongozi wa upinzani wasome alama za nyakati na wasome matakwa ya Watanzania wengi bila kujali vyama vyao. Wajue Watanzania wa sasa wa kizazi cha dot com wana uelewa mkubwa sana na wengi ni wapiga kura wapya kabisa.
Tanzania hatuna Raila Odinga. Ule uamuzi wa raila kusema anatosha huyu mzee ulikuwa wa kishujaa mno. Madaraka ni kitu kibaya mno ndio maana kuyaacha inakuwa kazi kweli kweli.
Ni nani katika viongozi wa vyama Afrika wangeweza kusema vile? labda Nyerere kama angekuwa kwenye hali kama hiyo.
Mwaka 1995 nilikuwa naombea tu Mrema awavute akina Mtei na hata JK na kisha kumwachia mmoja wao kugombea urais ili yeye aje awe PM. Lakini wapi hakuwa na busara hizo na akaona ataweza kuwa rais bila hata kushirikiana na vyama vingine. Matokeo yake wote tumeyaona.
Kwa Tanzania hii ambayo hata kugombea tu mwenyekiti aliyepo inakuwa shida; tusitegemee kumwona Raila Odinga wa Tanzania siku za karibuni.
Halisi,
Mkuu shukran na pongezi kwani mawazo yako ndio yale yanayojenga.. CUF na Chadema wanatakiwa kusoma alama za wakati..
Dr.Slaa - For President, Mwenza akiwa Hamd Rashid, hivyo Dr. hana sababu ya kugombea tena uongozi wa chama.
Zitto kusema kweli mtu kaa mimi nimeisha msoma na naelewa nini dhamira yake kwani nakumbuka vizuri habari ya Harper!.. Zitto hana znia mbaya kwa chama isipokuwa ni mtu ambaye Unachukulia kuwa mwaka huu 2010 - Ushindi kuwa ni lazima.
Binafsi nampongeza sana Zitto kwa azma hiyo kwani ndani ya Chadema inaonyesha wazi kwamba Ushindi kwao sio kitu muhimu sana ila kuwaelimisha wananchi na kupigana na mafisadi. Vita ya Chadema imegeuka kuwa sio ya Kiitikadi ila ni vita against vichwa vya watu (Mafisadi) ndani ya chama CCM as if Chadema ni part au kitengo cha CCM.
Chadema wanatakiwa kufikiria Ushindi mwaka 2010 ni kumwondoa CCM ktk utawala na sio kuendeleza kampeni za kuondoka kwa baadhi ya vichwa vibaya (mafisadi) ktk Uongozi na uwakilishi wa CCM kuwa ndio ushindi unaotegemewa..
Wajipanga kwa urais
Mwandishi WetuMei 21, 2008 Masha, Membe watajwa CCM
Slaa, Hamad kusimama upinzani
MIAKA miwili tu kabla ya Rais Jakaya Kikwete kumaliza kipindi chake cha kwanza mwaka 2010 na huku serikali yake ikiandamwa na kashfa za ufisadi, wanasiasa ndani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) na wale wa upinzani wanajipanga kwa nia ya kujiandaa kushika nafasi hiyo, Raia Mwema imefahamishwa.
Habari zinaeleza kwamba kwa sasa baadhi ya wana CCM wanajenga msingi wa kuwawezesha kumrithi Rais Kikwete katika uchaguzi mkuu ujao lakini wakishindwa, angalau basi kwa uchaguzi mwingine wa 2015; huku wapinzani wao wakipania kuchukua madaraka mwaka 2010, wakitumia kuyumba kwa nchi katika sehemu kubwa ya awamu ya kwanza ya uongozi wa Serikali ya Awamu ya Nne.
Kwa mujibu wa habari hizo, tayari mazungumzo na mikakati imekuwa ikifanyika katika maeneo mbalimbali nchini kwa nia ya kuangalia wanasiasa wanaoweza kushika nafasi ya urais, lakini pia kuwazuia wale ambao wanahofiwa kuweza kuharibu mikakati hiyo.
Wanasiasa kadhaa wakubwa nchini wa sasa, wastaafu na hata wale walioguswa na kashfa, wamekuwa wakitajwa moja kwa moja kujihusisha katika mikakati hiyo ama kwa kupima upepo kama wanaweza kujitokeza wao au kwa kuandaa watu wanaowaunga mkono.
Kwa upande wa upinzani, wanasiasa wapya kabisa wanatajwa kuweza kuibuka na kwa kupishwa na wanasiasa waliogombea katika Uchaguzi Mkuu uliopita, ikiwa ni mkakati unaoelezwa kujaribu kuwavuta wapiga kura wengi.
Imeelezwa kwamba waliogombea katika chaguzi za nyuma ikiwa ni pamoja na ule wa mwaka 2005, kupitia vyama vya upinzani, wanaweza kuwaunga mkono wagombea watakaouzika katika uchaguzi wa mwaka 2010.
Wanaopewa nafasi kubwa zaidi ya kuweza kusimamishwa kwa nafasi ya urais kwa upande wa upinzani ni pamoja na Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Wilbroad Slaa na Kiongozi wa Upinzani ndani ya Bunge, Hamad Rashid Mohamed, ambao wanaelezwa kuweza kukubaliana mmoja akawa Mgombea Mwenza.
Wanasiasa hao wa upinzani wanaelezwa kusukumwa zaidi na wabunge wenzao pamoja na watu wa kawaida wanaofuatilia mwenendo wa kisiasa nchini hasa kutokana na mchango wao ndani ya Bunge ambalo limebadili hali ya kisiasa nchini kwa kurudisha mwamko wa wabunge na wananchi.
Hamad Rashid amelithibitishia Raia Mwema jana kwamba ameshauriwa kujiandaa kuwania urais mwaka 2015 lakini baadhi wametaka aanze mwaka 2010, akiwataja baadhi ya wabunge waliomshauri, wakiwamo hata wa Chama cha Mapinduzi (CCM).
Ni kweli nina nia ya kuwania urais lakini si wa Zanzibar na kwamba nilijiandaa kwa mwaka 2015, lakini wabunge wenzangu baadhi kutoka CCM wamenishauri nianze kujitokeza mwaka 2010, alisema Hamad, ambaye amewahi kuwa ndani ya Serikali ya Muungano katika wizara za Fedha na baadaye Mambo ya Ndani.
Akizungumzia suala hilo, Dk. Slaa alisema sasa ni mapema mno kuzungumzia mambo ya urais kutokana na nchi kuwa katika harakati za kupambana na ufisadi unaoihusisha hata Ikulu yenyewe.
Alisema Dk. Slaa: Bado tuko mbali tukipambana na ufisadi. Nchi haitaki wanaokimbilia Ikulu. Inataka wenye ujasiri wa kusafisha Ikulu. Ukisema nawe unakimbilia Ikulu, unakuwa unataka ukafanye biashara au ukachote Ikulu. Wakati ukifika, hayo tutayajadili.
Kwingineko kumekuwa na minongono kuwa Makamu Mwenyekiti wa Chadema, Chacha Wangwe pia ana nia ya kugombea kwa tiketi ya chama. Nia ya kuwania urais ya viongozi hao wawili huenda ikawagombanisha na mwenyekiti wao, Freeman Mbowe, aliyesimama mwaka 2005 na ambaye inaaminika angependa asimame tena mwaka 2010.
Alipoulizwa kuhusu habari hizo za yeye kutajwa kuwania urais, Chache Wangwe alisema, Ni kweli, ikiwa chama changu kitanipendekeza, nitakua tayari kugombea.
Mkanganyiko mwingine wa Chadema unaweza kutokana na habari kwamba Naibu Katibu Mkuu, Zitto Kabwe, akizungumza na Watanzania walioko Houston, Marekani alikokuwa kwa ziara hivi karibuni, alisema atawaunga mkono Dk. Slaa na Hamad kama mazingira ya kisiasa yatawafikisha watu hao wawili katika kugombea mwaka 2010.
Siku za karibuni zimeshuhudia kutoaminiana miongoni mwa viongozi wa Chadema na hata kumhusisha Zitto na madai ya kuwa na urafiki wa karibu na Rais Kikwete, kiasi cha Kikwete kutaka kumteua kuwa waziri katika Serikali kabla ya mabadiliko ya Baraza la Mawaziri ya Februari mwaka huu.
Zitto ameiambia Raia Mwema wiki katika mahojiano kuwa wakati hapingi kuwa ana ukaribu wa kiasi fulani wa siku nyingi na Rais Kikwete, hakuna wakati alipotaka kuingia katika serikali yake.
Sijawahi kuombwa na Rais Kikwete kuingia katika serikali. Msimamo wangu siku zote umekuwa ni kutumikia taifa bila kujali itikadi. Hata Rais anajua hili, kwamba siwezi kuhama chama au kwenda kinyume na maamuzi ya chama changu. Kwamba Rais Kikwete ni rafiki yangu, si kweli. Ninafahamiana naye kitambo. Ninajua ananiheshimu sana. Lakini hakuwa chaguo langu la urais wakati wa mchakato wa chama chao na hata katika uchaguzi mkuu, alisema Zitto.
Lakini wafuatiliaji wa masuala ya kisiasa wanasema Zitto hajawahi kusikika akimshambulia Rais Kikwete katika hotuba zake na mara kadhaa amekuwa akimsifia katika maamuzi yake mbalimbali ambayo yamepingwa na wenzake. Hata kuingizwa kwake katika Kamati ya Madini ya Jaji Mark Bomani kulizua maswali mengi kutoka kwa wanasiasa wa CCM iliyombana alipoibua hoja ya mgodi wa dhahabu wa Buzwagi, na wa Upinzani.
Wengi hawaamini maelezo ya Zitto kwani anaonekana ni mtu mwenye kujiandaa kutokana na kuwa kwake na mahusiano ya karibu sana na wastaafu kama Jaji Joseph Warioba na Dk. Salim Ahmed Salim, watu ambao wana ushawishi mkubwa katika jamii.
Alipoulizwa kuhusu hili Zitto alisema kuwa yeye anawaheshimu sana viongozi wastaafu na hupenda kujifunza kutoka kwao na mahusiano yake nao hayana maana ya kutafuta kuungwa mkono.
Nimekuwa na mahusiano na wazee hawa kama viongozi. Sio hawa tu. Ninazungumza na mzee Kaduma (Ibrahim), mzee Butiku (Joseph), mzee Kimiti (Paul) na mzee Jackson Makweta. Pia ninazungumza sana na Spika Samuel Sitta. Huwezi kusema hawa wote wananiandaa mimi kuwa Rais. Huo ni woga tu wa watu. Ni hulka yangu kuheshimu wakubwa na kujifunza ndiyo maana ukinikuta na Hamad Rashid hutaona mahusiano ya kiubunge. Utaona mahusiano ya mwalimu na mwanafunzi, anasema Zitto ambaye mwaka jana gazeti moja la kila wiki lilimshutumu kwa kujipendekeza kwa viongozi wakubwa.
Kwa upande wa CCM, habari zinaeleza kwamba tayari makundi yameanza kujipanga kwa uchaguzi mkuu wa Rais mwaka 2010 na wa 2015 kama Rais Jakaya Kikwete atafanikiwa kushinda patashika ya mwaka 2010 na kuendelea muhula wa pili ambao ni wa mwisho kwa mujibu wa katiba.
Makundi hayo yanajipanga mapema na kwa kuanzia imeelezwa kwamba wanasiasa na wafanyabiashara wanajiandaa kuweza kupata wajumbe wa kutosha katika Mkutano Mkuu wakati wa uchaguzi, wajumbe ambao ndio watakuwa waamuzi wakubwa wa mgombea kutoka chama hicho.
Licha ya kwamba kuna fununu za wagombea wengine kujitokeza kushindana na Rais Kikwete katika kinyanganyiro cha ndani ya CCM mwaka 2010, inaonekana uwezekano wa ushindi ni mdogo kutokana na utamaduni wa CCM kuendeleza muhula wa pili wa Rais aliyeko madarakani utaendelea. Hata hivyo, hali inaweza kubadilika kama Kikwete atakumbwa na dhoruba yoyote kubwa ya kisiasa kabla au kuelekea 2010.
Magazeti kadhaa, hivi karibuni, yalimtaja Profesa Mark Mwandosya kama mgombea anayetajwa kuweza kumkabili Rais Kikwete ikifika mwaka 2010. Mwandosya alikuwamo katika hatua za mwisho za mbio za urais mwaka 2005.
Wengine wanaotajwa kwa sasa kwa upande wa CCM kujiandaa ama kuandaliwa kumrithi Kikwete, iwe 2010 au 2015, ni pamoja na Waziri wa Mambo ya Ndani Lawrance Masha na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe.
Kumekuwapo pia na mijadala ya Watanzania, na hasa walioko nje, inayotaka Dk. Salim agombee ama kupitia CCM au kupitia muungano wa vyama vya upinzani. Yeye na Profesa Mwandosya walishindwa na Kikwete 2005, wote wakiwa wamefikia hatua ya mwisho kabisa.
.Kuna watu wengi hapa forum mnasema tu mko Ulaya na Marekani hata kuja nyumbani hamji mana you cannot leave those countries na baadaye ukapata visa ya kurudia so mnaongea tu kwa kuwa una access ya comp.Hali ya siasa tanzania ni ngumu na watu kama Slaa , Zitto , Mbowe wana sacrifice sana .Ushabiki tuache tuje kwenye ukweli wa siasa .Kitila waambie hawa .
Lazima tusonge mbele sana na hivyo ni lazima kuona kuwa kuna haja ya CHADEMA kujipanga kwa ajili ya mwakani na ni tegemeo kubwa sana kwa Watanzania woteHalisi,
Mkuu shukran na pongezi kwani mawazo yako ndio yale yanayojenga.. CUF na Chadema wanatakiwa kusoma alama za wakati..
Dr.Slaa - For President, Mwenza akiwa Hamd Rashid, hivyo Dr. hana sababu ya kugombea tena uongozi wa chama.
Zitto kusema kweli mtu kaa mimi nimeisha msoma na naelewa nini dhamira yake kwani nakumbuka vizuri habari ya Harper!.. Zitto hana znia mbaya kwa chama isipokuwa ni mtu ambaye Unachukulia kuwa mwaka huu 2010 - Ushindi kuwa ni lazima.
Binafsi nampongeza sana Zitto kwa azma hiyo kwani ndani ya Chadema inaonyesha wazi kwamba Ushindi kwao sio kitu muhimu sana ila kuwaelimisha wananchi na kupigana na mafisadi. Vita ya Chadema imegeuka kuwa sio ya Kiitikadi ila ni vita against vichwa vya watu (Mafisadi) ndani ya chama CCM as if Chadema ni part au kitengo cha CCM.
Chadema wanatakiwa kufikiria Ushindi mwaka 2010 ni kumwondoa CCM ktk utawala na sio kuendeleza kampeni za kuondoka kwa baadhi ya vichwa vibaya (mafisadi) ktk Uongozi na uwakilishi wa CCM kuwa ndio ushindi unaotegemewa..
Halisi,
Mkuu shukran na pongezi kwani mawazo yako ndio yale yanayojenga.. CUF na Chadema wanatakiwa kusoma alama za wakati..
Dr.Slaa - For President, Mwenza akiwa Hamd Rashid, hivyo Dr. hana sababu ya kugombea tena uongozi wa chama.
Zitto kusema kweli mtu kaa mimi nimeisha msoma na naelewa nini dhamira yake kwani nakumbuka vizuri habari ya Harper!.. Zitto hana znia mbaya kwa chama isipokuwa ni mtu ambaye Unachukulia kuwa mwaka huu 2010 - Ushindi kuwa ni lazima.
Binafsi nampongeza sana Zitto kwa azma hiyo kwani ndani ya Chadema inaonyesha wazi kwamba Ushindi kwao sio kitu muhimu sana ila kuwaelimisha wananchi na kupigana na mafisadi. Vita ya Chadema imegeuka kuwa sio ya Kiitikadi ila ni vita against vichwa vya watu (Mafisadi) ndani ya chama CCM as if Chadema ni part au kitengo cha CCM.
Chadema wanatakiwa kufikiria Ushindi mwaka 2010 ni kumwondoa CCM ktk utawala na sio kuendeleza kampeni za kuondoka kwa baadhi ya vichwa vibaya (mafisadi) ktk Uongozi na uwakilishi wa CCM kuwa ndio ushindi unaotegemewa..
.Kuna watu wengi hapa forum mnasema tu mko Ulaya na Karekani hata kuja nyumbani hamji mana you cannot leave those countries na baadaye ukapata visa ya kurudia so mnaongea tu kwa kuwa una access ya comp.Hali ya siasa tanzania ni ngumu na watu kama Slaa , Zitto , Mbowe wana sacrifice sana .Ushabiki tuache tuje kwenye ukweli wa siasa .Kitila waambie hawa .
Lunyungu,
Acha hizo kamba zako. Wewe kuwa na visa hapo Holland mara hii unaanza kusagia Watanzania wenzako wanaoishi nchi zingine?
Kama hawana visa inatakiwa uwaombee na wenyewe wafanikiwe na sio kuingiza vijembe.
Umeongea upumbavu hapo juu na imebidi nikuambia ukweli kwamba uko Holland.
Wengine pia tumewahi kuishi bila visa Europe wakati tunatafuta na sasa tumerudi nyumbani lakini hatudharau wenzetu ambao bado wanahangaika.
Kuwa mwungwana brother! Acha vijembe visivyo na maana, au unataka mpaka tutaje na jina lako ndio ujue tunakufahamu vizuri?
Itakuwa ngumu kumpitisha Dr. Slaa 2010.Kimkakati kama Chadema watakuwa wamepanga Dr Slaa aache uenyekiti ili aende kugombea Urais na kama ikiwa kuna mkakati wa vyama vya upinzani kama ilivyowahi kuwa reported kwamba mgombea Mwenza atatoka CUF Zanzibar na walimtaja Hamad Rashid Mohamed, ambaye ni kiongozi wa upinzani Bungeni nadhani kutakuwa na changamoto kubwa kwa CCM na hiyo itawavuta CUF ambao walianza kupoteza nguvu bara kwa kuonekana kama wanagombana na Chadema.
Haya ni mawazo yangu na pia ni mawazo ya Watanzania wengi kuona CUF na Chadema, pamoja na tofauti zao wanakaa pamoja na kuchukua nchi. Kina Kibaki, Raila, Saitoti, Ruto na wengine, hawakuwa wakielewana na hawaelewani hadi sasa, lakini walifanya uamuzi kwa kufuata matakwa ya wananchi wao na wakaunda NARC ambayo ilichukua nchi. Ni Raila Odinga aliyetaja jina la Kibaki pale Uhuru Park (nilikuwapo) na alisema, "Kibaki atosha?" akaitikiwa "atoshaaaaa!!!" na yeye akasema, "basi tuacheni tukajadili na kuwatangazia" na baadaye wakajadili na kutangaza.
Kama kina Kibaki na Raila wangefanya tofauti, na kama Moi na wenzake wangezuia mkutano wa Uhuru, basi Kenya leo hii ingekuwa kama Rwanda na matukio ya uchaguzi yangekuwa mabaya zaidi ya yaliyotokea katika uchaguzi uliopita. Haya ni mawazo yangu na ninasema kwamba viongozi wa upinzani wasome alama za nyakati na wasome matakwa ya Watanzania wengi bila kujali vyama vyao. Wajue Watanzania wa sasa wa kizazi cha dot com wana uelewa mkubwa sana na wengi ni wapiga kura wapya kabisa.