Dr. Slaa: Kikwete Amerahisisha Urais

Dr. Slaa: Kikwete Amerahisisha Urais

Mtoto wa nyoka ni nyoka,
umesahau hata jei kei aliutaka uraisi toka 1995,mzee nyrere akiwa mei mosi mbeya akasema.
'nchi haiwezi kuongozwa na wahuni wanao amka leo na kutamani kuingia ikulu bila kufikiria watawafanyia nini watanzania'
-rejea ombi aliloenda nalo butiama na kikwete akaambiwa aende nairobi akikutana na dk.salim a.salim amwambie kuwa aje agombee uraisi.
Ndipo mzee salim kwakuwa hakuwa na uroho wa madaraka alikataa ili aendelee kuitumikia afrika kwa ujumla.
-hawa akina makamba,kigwangala wametumwa na makundi yao kupima upepo.
 
Mwl Jk Nyerere(RIP) aliwahi kusema, urais ni mzigo haukimbiliwi. Na ukweli hiyo ndio sababu kubwa mwaka 1985 hakuna aliyeelezea nia yake ya kuwa rais. Mwinyi yeye aliirahisisha urais sana na wakajitokeza watu wengi sana kumrithi.

Kuna rafiki yangu nilikuwa nazungumza nae kwa simu ananiambia alikuwa na informal conversation na Dr Slaa jana akawa anamwambia kwa jinsi JK anavyoongoza nchi kishkaji kila mtu anajiona anauweza urais. Anasema usishangae wakajitokeza watu mia mbili come 2015 kuutaka urais maana hata diwani nae atataka awe rais. Alikuwa hamzungumzii Zitto lakini inaonyesha hata Zitto ameona kazi ile ni laini sana hata yeye anaweza!

''Mungu akitaka linakuwa hata kama watu wote hawataki'' - JK AKIMBARIKI JANUARY MAKAMBA
 
SUgu na lema nao wanautaka urais,mzee slaa pumzika sasa hata useme vipi watu hawakuelewi siku hizi
 
Hebu fikiria kuna mkutano wa marais alafu nchi kama Uganda inawakilishwa na Y. Mseveni, Kenyatta anaiwakilisha Kenya, Malawi Prof Mtharika, Rwanda Kagame, Zambia M. Satta alafu eti Tanzania tunawakilishwa na Makamba au Kigwangalla. (Kweli!!) Tunataka rais wa kwenda kutoa shikamoo kwa marais wenzake na kuwabebea mafaili? Hawa vijana wamejipima kidplomasia? au wanajipima kwa rais aliyepo? Kiwete kwa maoni yangu hajawafikia marais wote waliomtangulia nchi hii, lakini ni bora mara mia ukimlinganisha na hawa 'watoto' ambao wanatamani ofisi kuu ya nchi hii.

Hawa hawajamaliza hata kipindi kimoja cha ubunge, hawako hata kwenye 20 bora ya wabunge waliopo sasa hivi. Eti wanauota urais (kweli???) Hivi kama Nyerere ndiye angekuwa anaachia kijiti wangejipanga katika mstari wa kumpokea kweli? Hivi wanajiona wangeweza kuvaa viatu kama vya mzee Mwinyi? Urais nchi hii umeshuka kiasi hiki? Kutoka kupanda tumbaku ukaenda chuo kikuu ukarudi kugombea ubunge umeshafaa kuwa rais? (Kweli???) Au kutoka chuo kikuu ukapata nafasi ya kuandika hotuba za rais, ukagombea ubunge umshajiona unafaa kuwa rais? (Kweli???)

Kampeini yangu kuheshimi Ikulu yetu haitakoma leo, tunahitaji kuheshimu Ikulu yetu na mtu anayekaa pale lazima awe na hadhi ya mtazania namba moja kweli. Nchi isiyoheshimu Ikulu kasri yake sijui ni nchi ya aina gani. Nadhani hatukumuelewa Mwl Nyerere aliposema Ikulu ni mahali 'patakatifu' au hatuelewi maana ya 'utakatifu'. Haiwezekani kila mtu ajione anaweza kuwa rais, kwanza ni kumdharau rais aliyepo na kudharau cheo cha urais ambacho ni alama ya nchi kimataifa.

munataka tuongozwe na watu wanaoamini katika gongo kama slaa ndio watakao upa heshima urais? tuaachie vijana
 
naona slaa anataka aachiwe agombee peke yake.
Lakini katiba si inakubali mtu yeyote kama anakidhi vigezo kikiwemo kile cha miaka 40 na kuendelea?.
Kisa cha kuchagua rais ambae lifespan yake iko ukingoni?
 
kuna KATIBU KATA MMOJA HUKU KWETU , AMEJIAPIZA KWAMBA ATACHUKUA FOMU YA urais CCM 2015 !
 
naona slaa anataka aachiwe agombee peke yake.
Lakini katiba si inakubali mtu yeyote kama anakidhi vigezo kikiwemo kile cha miaka 40 na kuendelea?.
Kisa cha kuchagua rais ambae lifespan yake iko ukingoni?

kwani WEWE UNAJUA UTAKUFA LINI ?
 
Siku hizi usishangae hata makonda akataka kugombea urahisi wa masisiem
 
Mwl Jk Nyerere(RIP) aliwahi kusema, urais ni mzigo haukimbiliwi. Na ukweli hiyo ndio sababu kubwa mwaka 1985 hakuna aliyeelezea nia yake ya kuwa rais. Mwinyi yeye aliirahisisha urais sana na wakajitokeza watu wengi sana kumrithi.

Kuna rafiki yangu nilikuwa nazungumza nae kwa simu ananiambia alikuwa na informal conversation na Dr Slaa jana akawa anamwambia kwa jinsi JK anavyoongoza nchi kishkaji kila mtu anajiona anauweza urais. Anasema usishangae wakajitokeza watu mia mbili come 2015 kuutaka urais maana hata diwani nae atataka awe rais. Alikuwa hamzungumzii Zitto lakini inaonyesha hata Zitto ameona kazi ile ni laini sana hata yeye anaweza!

Ni kweli kabisa mkuu, Kikwete ka-turnish image ya urais hadi hata wauza unga (kama makamba jr) wanatamani kuingia ikulu. UBOYA wa JK ndin uliosababisha haya yote.
 
Ni kweli kabisa mkuu, Kikwete ka-turnish image ya urais hadi hata wauza unga (kama makamba jr) wanatamani kuingia ikulu. UBOYA wa JK ndin uliosababisha haya yote.

Weee ! Unasema kweli ?
 
Back
Top Bottom