Dr. Slaa kesho atasema nini?

Critical thinking is the missing course in our college curriculum that is why most chase a followers. Your leaders might be wrong. Learn to think for yourself.
 
Sisi wote ni wanafunzi na wahanga wa Dr. Slaa kifikra na kisiasa. Dr. Slaa umetufundisha watanzania wote kuwa CCM haifai na ndio chanzo cha ufisadi, ubadhilifu, wizi, matumizi mabaya na sera mbaya zisizotekelezaka na zilizosababisha maisha ya watanzania kuwa mabaya. Ukiwa na wenzako wa chadema kwa kutumia kampeni za sangara, M4C, redio na tv, ulitufundisha kuikataa CCM na tulikuelewa vizuri, tuliamini na tukafanya hivyo kwa moyo, kwa nguvu na kwa akili zetu zote. Wewe ndiye uliyesababisha taifa lote liichukie na kuikataa CCM kwa moyo na nguvu zote, watu wameshalielewa somo lako kuhusu ubaya wa CCM kwetu. Ulitufungua akili tuliokuwa hatujui siasa za chama cha CCM. Tulifanya hivyo kwakuamini kwamba wewe ni msomi mzuri na mtumishi wa Mungu husemi uongo na utakuwa umefanya utafiti mzuri kuhusu uhusiano uliyopo kati ya maisha ya watanzania na sera, utekelezaji wa sera na utawala wa CCM. Uliamsha hamasa na ari ya watanzania katika siasa na kufikiri juu ya maisha yao. Sasa tumeelimika sana kupitia wewe na wenzako wa chadema kuhusu ubaya wa CCM kwetu na kwa taifa, watu hawataki tena kusikia habari za CCM mitaani na maofisini. Ahsante sana baba!

Sasa wafuasi wako tumeanza kushikwa na butwaa kubwa kukuona wewe tena unakipigia debe CCM kiendelee kubakia madarakani!!!!@***&.com???. Hapa kuna mawili, ama wewe unataka kutugeuza sisi kichwa chini miguu juu, au wewe ndo umegeuka mwenyewe kichwa chini miguu juu. Tunajiuliza nini kimetokea kwa mwalimu wetu Dr. Slaa hadi kufanya hivi? Kama shida ni Lowassa kuhamia chadema basi hata wewe hukupaswa kuwa na uhalali wa kukilaumu CCM kwa ufisadi, ubadhilifu na huduma mbovu kwa wananchi, badala yake ulipaswa kuwalaumu viongozi waliotokana na CCM tu peke yake wasiofanya vizuri na sio chama chote cha CCM kuwa hakifai. Vinginevyo wewe ulikuwa katibu mkuu wa chadema hivyo ungeweza kuhakikisha kuwa rais (Lowassa) anayetokana na chama cha chadema angeongoza nchi kwa mujibu wa kanuni, taratibu na maadili ya chadema tu basi. Hivyo ukiwa kama katibu mkuu wa chadema hukuwa na sababu za msingi za kumuogopa Lowassa 'fisadi' kuhamia chadema au kugombea urais kupitia chadema maana chama chini ya katibu mkuu (wewe) kingemnyoosha na kumfanya kuongoza nchi kwa mujibu wa chadema. Kama hili limeshindikana kwako na kwa chadema kwanini ulitaka hili liwezekane kwa CCM? Ulikuwa unatudanganya kuhusu ubaya wa CCM? Ulipaswa kuwalaumu viongozi na watendaji wabaya wa CCM na sio chama cha CCM chote kama chama. Unapaswa kuwaomba samahani CCM hadharani kwa kukisema chama chao vibaya badala ya kumsema mwanachama/kiongozi wa CCM ambaye ni mwizi, mbadhilifu, fisadi, n.k, pili, uwaombe radhi watanzania kwa kuwapotosha kuhusu ubaya wa CCM kama chama.

Kama wewe ukishindwa kuyafanya haya yote mawili kwapamoja taifa hili litakuwa juu ya kichwa chako kwa kuliyumbisha na kutaka kulipasua vipande. CCM wanafunzi wako tunakuona kama mwalimu usiyekuwa na msimamo, uliyehongwa, mwenye ubinafsi wa kuwa rais kwa gharama yoyote, unayependa porojo, usiyependa maamuzi ya pamoja ndani ya chama, mpotoshaji, muongo, usiyejali wafuasi na familia yako, na usiyefaa kusikilizwa tena na watu wenye shida za maisha kama sisi. Hatujui kesho tena utasema nini, utakuwa wapi na nani. Kwaheri huwaminiki mzee!!!

Hoja zako dhaifu sana. Dr Slaa amekuwa akiishi na ameendelea kuishi kwa kuamini Lowasa ni fisadi na hajawahi kubadili msimamo huo. Na alikubali ujio wa Lowasa kama mwanachama na kuna masharti alitoa kama katibu mkuu likiwemo la yeye mwenyewe kujisafisha hadharani jambo ambalo hata moja halikufanyika! Sasa huu upotoshaji unaouleta humu ni siasa nyepesi zisizo na tija kwa kuukwepa ukweli ulio dhahiri kuwa Lowasa bado ni Fisadi na huo ndio ukweli anaouishi Dr Slaa.
 
Nadhani atawananga hawa wafuatao
1.Mkewe Rose Kamili
2.Wanawe
3.Mbatia
4.Lowassa
5.Viongoz wa dini
6.Watanzania wanaotaka mabadiliko
7.Waandishi wa habari
 
Hiki kizee kinakoelekea kitaokota makopo,yaani kinapayuka tu hovyo hovyo.Kwa taarifa yenu ccm sasa basi,wametudanganya vya kutosha, tucheki na chama kingine.
 
Hoja zako dhaifu sana. Dr Slaa amekuwa akiishi na ameendelea kuishi kwa kuamini Lowasa ni fisadi na hajawahi kubadili msimamo huo. Na alikubali ujio wa Lowasa kama mwanachama na kuna masharti alitoa kama katibu mkuu likiwemo la yeye mwenyewe kujisafisha hadharani jambo ambalo hata moja halikufanyika! Sasa huu upotoshaji unaouleta humu ni siasa nyepesi zisizo na tija kwa kuukwepa ukweli ulio dhahiri kuwa Lowasa bado ni Fisadi na huo ndio ukweli anaouishi Dr Slaa.

Je kuhusu kikwete slaa anamuwazaje?
 
Wewe hujaelewa. Sio Kwamba Dr Slaa anaipenda ccm no Ila yeye tatizo lake ni Lowasa kama ingewezekana mngemtoa Lowasa alafu mngempa Tundu lisu mngeona Dr Slaa akiwaunga mkono. Huwezi kufanya mabadiliko kwa kumtumia fisadi alafu ubaki na amani..... Kumbuka mafisadi wote waliobaki ccm wanasubiri mzee mnvi aapishwe waanze kugawana vya kugawana.

Great Thinkers mpo wachache sana.
Wengine ni washabiki tu wanaoshabikia wasivyovielewa.
 
Hoja zako dhaifu sana. Dr Slaa amekuwa akiishi na ameendelea kuishi kwa kuamini Lowasa ni fisadi na hajawahi kubadili msimamo huo. Na alikubali ujio wa Lowasa kama mwanachama na kuna masharti alitoa kama katibu mkuu likiwemo la yeye mwenyewe kujisafisha hadharani jambo ambalo hata moja halikufanyika! Sasa huu upotoshaji unaouleta humu ni siasa nyepesi zisizo na tija kwa kuukwepa ukweli ulio dhahiri kuwa Lowasa bado ni Fisadi na huo ndio ukweli anaouishi Dr Slaa.

Ahsante.
 
mi nimemuelewa sana Dr, Hajasema uchague ccm bali yeye haamini ktk fisadi lowasa.
yeye ndiye aliyetufungua macho juu ya ufisadi na ubaya wa ccm...
kubwa zaid ni list of shame, ufisadi wa lowasa... leo iweje mtu huyo huyo mwenye akili timamu amsafishe mtu huyu/??
ni unafiki ambao mm siukubali... Generally, CHADEMA dissappointed me,siamini ktk lowasa ambao wao walinambia hafai hafai, leo tena anafaa
NEVER
 
Kwa Thread hizi kweli CHADEMA mpo vizuri kwa Propaganda.
Mlimtukana sana Zitto.
Leo mmegeukia kwa Dr. Slaa
Sitawashangaa siku mkijitukana wenyewe.
Niliipenda CHADEMA ila kwa siasa hizi za kuchafuana mmh...
 
ZOEZI LA UUZWAJI WA NYUMBA LILIFANYIKA WAKATI WA UONGOZI WA AWAMU YA TATU.... 1995 - 2005
AZIMIO LILIPITISHWA NA BARAZA LA MAWAZIRI LILIOKUWA LIKIONGOZWA NA MALAMKA YA WAZIRI MKUU Ndugu FREDRICK SUMAYI.... Pamoja na yeye alikuwepo Waziri Mkongwe Lowasa ( alikuwa na uzoefu wa kufanya kazi ndani ya Serikali ya ccm kwa miaka 30) na Waziri asiye na uzoefu wa muda mrefu serikalini Ndugu John Pombe ( alikuwa na uzoefu wa miaka 5)
Natumain nimekusaidia Ndugu!
 
mi nimemuelewa sana Dr, Hajasema uchague ccm bali yeye haamini ktk fisadi lowasa.
yeye ndiye aliyetufungua macho juu ya ufisadi na ubaya wa ccm...
kubwa zaid ni list of shame, ufisadi wa lowasa... leo iweje mtu huyo huyo mwenye akili timamu amsafishe mtu huyu/??
ni unafiki ambao mm siukubali... Generally, CHADEMA dissappointed me,siamini ktk lowasa ambao wao walinambia hafai hafai, leo tena anafaa
NEVER

Jamani ifike mahali tukawa wazi tu kuwa dr slaa anatumiwa na ccm..kakatiwa mkwanja...amenyan'ganywa tonge mdomoni..kimada wake ndo mwenye maamuzi ya mwisho katika familia yao! Anakaa serena hotel a 5 ¤ hotel..analindwa na usalama wataifa24/7..that's incredible! Kama alivyosema naye ni binadamu ana moyo. .kuwa ni kweli kaumia sana kunyan'ganywa kugombea dkk za mwisho....kimada wake is the one who is running the show..alimtupia nguo zake nje na kulala kwenye gari..toka siku ile hakutoka tena!..strange! Ku sum up. .issues ya lowassa fisadi hapa haipo maana huko alipo au washika dau wake wapya ndo wachafu zaidi..hadi akajichanganya na kuifananisha ccm na choo! Ile list of shame ilikuwa na watu 11 katoka moja tu wengine wote wapo huko aliko hivi sasa..tafadhali tusipotoshe wapenda mageuzi kwa interest za pande tunazozishabikia!
 
Yaani kama kuna mtu anayejisahau na Dr.Slaa akiwemo kwamba watanzania hawajui lolote Kuhusu Richmond anajidanganya.Ndugu zangu Watanzania wa leo sio wale uliowaona jana wasiojua lolote ,hawa wa leo ni balaa kabisa wanajua wapi Richmond ilianzia na mpaka sasa mwenye Richmond yake ameshajulikana,Hivyo unayetaka Lowasa ashitakiwe unajifanya kuvaa tintedi eti humjui mwenye Richmond ww endeleza ngonjera zako SISI haturudi nyuma achaneni na hiyo kitu mtaongea sana mwisho mtapasuka midomo SISI haturudi nyuma LOWASA ndio habari ya mjini na inaitwa ALUTA CONTINUE.
 
Dr. Slaa amejimaliza mwenyewe kwa sababu anazo zijua yeye mwenyewe,tumuache apumzike kwa amani. Hana jipya tena ni mtu wa kutumiwa na maboss wake CCM kama doli la mtoto!
 
Back
Top Bottom