Ibrah
JF-Expert Member
- Mar 22, 2007
- 2,729
- 528
Si ajabu kuona Lt Gen Shimbo anajifanya Polisi wa CCM na kuzingizia ati kuna watu wanataka kuleta fujo; Umati huo wa Mbeya ni ujmbe tosha kuwa Shimbo na Jeshi letu la Wananchi (JWTZ) si Jeshi lake Shimbo na CCM na Wananchi wenyewe (sehemu ndogo tu) ni hao kwenye picha za Mbeya.
Hii ni nguvu ya Umma; Kuna mifano mingi ya nguvu ya Umma. Shimbo akumbuke kuwa Milesovic alijaribu kushinda uchaguzi kutumia Jeshi, pamoja na kupanga maelfu ya Wanajeshi kuizingira Ikulu lakini wananchi wa Yugoslavia hawakuogopa waliandamana hadi Ikulu na Wanajeshi waliokuwepo waliwaangalia tu bila kuchukua hatua yoyote na hatimaye Milosevic akaikimbia Ikulu na baadaye kujikuta The Hague ICC.
Shimbo na wenzako, msijaribu kushindana na Wananchi, acheni demokrasia ifuate mkondo wake.
Hii ni nguvu ya Umma; Kuna mifano mingi ya nguvu ya Umma. Shimbo akumbuke kuwa Milesovic alijaribu kushinda uchaguzi kutumia Jeshi, pamoja na kupanga maelfu ya Wanajeshi kuizingira Ikulu lakini wananchi wa Yugoslavia hawakuogopa waliandamana hadi Ikulu na Wanajeshi waliokuwepo waliwaangalia tu bila kuchukua hatua yoyote na hatimaye Milosevic akaikimbia Ikulu na baadaye kujikuta The Hague ICC.
Shimbo na wenzako, msijaribu kushindana na Wananchi, acheni demokrasia ifuate mkondo wake.