Elections 2010 Dr. Slaa in Mbeya (picha)

Si ajabu kuona Lt Gen Shimbo anajifanya Polisi wa CCM na kuzingizia ati kuna watu wanataka kuleta fujo; Umati huo wa Mbeya ni ujmbe tosha kuwa Shimbo na Jeshi letu la Wananchi (JWTZ) si Jeshi lake Shimbo na CCM na Wananchi wenyewe (sehemu ndogo tu) ni hao kwenye picha za Mbeya.

Hii ni nguvu ya Umma; Kuna mifano mingi ya nguvu ya Umma. Shimbo akumbuke kuwa Milesovic alijaribu kushinda uchaguzi kutumia Jeshi, pamoja na kupanga maelfu ya Wanajeshi kuizingira Ikulu lakini wananchi wa Yugoslavia hawakuogopa waliandamana hadi Ikulu na Wanajeshi waliokuwepo waliwaangalia tu bila kuchukua hatua yoyote na hatimaye Milosevic akaikimbia Ikulu na baadaye kujikuta The Hague ICC.

Shimbo na wenzako, msijaribu kushindana na Wananchi, acheni demokrasia ifuate mkondo wake.
 
Nyota njema huonekana asubuhi. Nyota ya Slaa ilianza kungara mapema tu wakati wa kuomba wadhamini, sasa imeshamiri na kueneza nuru yake katika kona zote za nchi. JK yeye anategemea ulinzi wa viumbe visivyoonekana vya mnajimu Yahya bali Slaa anategemea ulinzi wa Mungu uonekanao ndani ya watu wake. (people's power)
GO SLAA GOOOOOOO!!!
 
Slaa+Mbalizi.jpg
 
Hali kama hii lazima kuna watu hawapati usingizi na lazima vikao vya usiku kucha vya kupanga mikakati vinafanyika. Mapambazuko yako karibu na hakuna kupunguza mwendo.
 
Amazing, wonderful, ooohh GOD of Ibrahim, Isaka na yakobo, hawa watu WENGIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIII saaaaaaaaaaaaaana wameamua, aiseee, aaaaaaaaaaaaaahhhh, watu wa mbeya au wengine wametoka zambia? ni wengi mnoooooooooo, mabadiliko si mchezo nimeamini, Dr Slaa umeshinda,







 
Mungu wa Israeli awe pamoja nawe utufikishe nchi ya ahadi yenye maziwa na asali! Sasa ninaanza kuona nuru inayoashiria enzi mpya kwa Tanzania! Mungu awabariki WaTZ wajitokeze kwa wingi kumpigia kura Dr. Slaa ili nchi irudi mikononi mwa wenye nchi.

Tumepuuzwa kiasi cha kutosha. Tumeonewa kiasi cha kutosha. Tumenyanyaswa kiasi cha kutosha. Tumenyonywa kiasi cha kutosha. Tumeibiwa kiasi cha kutosha. Tumedhauliwa kiasi cha kutosha. Unyonge wetu ndio uliotufanya tupuuzwe, tuonewe, tunyanyaswe, tunyonywe, tuibiwe, na tudharauliwa. Sasa tunataka mageuzi na kiongozi wetu wa Mmageuzi haya ni Dr. Slaa.
 
Wow wuuuuuuuuuuuuiiiiiiiiiii, i can'n imagine my eyes, heart and soul, such a BIG crowd,
watu kama utitiri, DR. Slaa ur another Obama, picha carries a big message. GOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOO Dr.

Dah! raha sana! nitalia machozi ya furaha yaliyochanganyika na ya huzuni kwa ushindi wa kishindo wa Dr Slaa. Huzuni ni kutokana na miaka 25 tuliyopoteza ya kuwa na mafisadi Ikulu. Tungekuwa na watu makini kama Dr Slaa nchi ingekuwa mbali sana kimaendeleo. Nakutakia kila la heri na baraka na Mungu akulinde dhidi ya wanaotaka kukudhuru kwa namna moja au nyingine.
 
Huu ni mwaka wa Watanzania kuchukua nchi yao toka mikononi mwa mafisadi na wasanii. Na mafisadi wote Dr Slaa na serikali yake watawapandisha kizimbani ili kujibu tuhuma mbali mbali dhidi yao na pia kufilisiwa mali zote zilizopatikana kwa kuwadhulumu Watanzania.
 
Nina uhakika sasa hata JWTZ wataelewa kuwa wakijaribu kufanya maagizo waliyopewa, basi wajue wanaandika Historia nyingine hapa Africa kama ya SOWETO. Najaribu kufikiria umati kama huo, unaambiwa kura zenu zimeibiwa na wanaamua kuingia mtaani, sijui itakuwaje. Narudia tena, Mwamunyange, Othman, Mwema, mmekalia kiti moto, tena ni cha moto kuliko hata cha wagombea uraisi wenyewe. Tafadhari, ni busara ndogo tu, inahitajika hapo. kazi kwenu na familia zenu.
 
Hii inabidi irudiwe aisee..............Dr. Slaa inabidi urudi tena mbeya wakati wa kumalizia malizia kampeni zako.............sasa inabidi tuhamie nyanda za kati na nyanda ya Ziwa..............inbidi kuwa very strategic...........kwa mwendo huu helikopta ni muhimu sana
 
Sorry mods, naona wengi wanaziulizia picha hizi lakini nimeona niwaletee kipekee bila kuingiza kwenye ile ya nyanda za juu kusini, mnaweza kufanya hivyo baadae baada ya wadau kuziona na kutoa maoni yao kwa hali hii ya Mbeya.

Mabango_slaa_mbeya.jpg

Sehemu ya umati wa wakazi wa mji wa Mbalizi mkoani Mbeya, wakiwa na mabango yenye ujumbe mabli mbali, wakati wa mkutano wa mgombea urais wa Tanzania kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa. (Picha na Joseph Senga)

slaa_akihutubia_mbalizi.jpg

Mgombea urais wa Tanzania kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, akiwahutubia maelfu ya wakazi wa mji wa Mbalizi mkoani Mbeya, kwenye Uwanja wa Stendi ya Mabasi. (Picha na Joseph Senga)

sugu_mbeya.jpg

Mgombea ubunge katika jimbo la Mbeya Mjini kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Joseph Mbilinyi "Mr Sugu", akiwatumbuiza wananchi wa mji wa Mbalizi, wakati wa mkutano wa kampeni za mgombea urais kwa tiketi ya chama hicho, Dk. Willbrod Slaa, uliofanyika kwenye Uwanja wa Stendi ya Mabasi. (Picha na Joseph Senga)

Mimi nimependa ujumbe kwenye yale mabango matatu!
 
Mheshimiwa Raisi wa awamu ya nne.

fanyika kazi ufisadi, viwanda vilivyouzwa kinyemela na mahoteli yarudishe serekalini.

kwa kifupi turudishie rungu letu << AZIMIO LA ARUSHA>>>
 
I said it. and am saying once more! Slaa will be our next president! kuna watu hawaamini. but Thats the reality. Shimbo ulijuaje CCM hawatakubali matokeo?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom