Dr. Slaa Hatatuangusha Watanzania

Dr. Slaa Hatatuangusha Watanzania

Kama kuna mtu anawanyima usingizi CCM ni Dr. Slaa! Wanajua kuwa hatakamatika Uchaguzi mkuu ujao!

Naona utakuwa umechanganya majina.

Anayewanyima usingizi viongozi wa CCM kwneye urais mwaka huu ni mtu mmoja tu, Laigwan Edward Lowassa, basi.

Dr Slaa alivyo sasa hawezi msumbua mgombea yoyote wa CCM.
 
Naona utakuwa umechanganya majina.

Anayewanyima usingizi viongozi wa CCM kwneye urais mwaka huu ni mtu mmoja tu, Laigwan Edward Lowassa, basi.

Dr Slaa alivyo sasa hawezi msumbua mgombea yoyote wa CCM.
Pole sana!!
 
Imenichukua miezi 36, kujifunza ndani ya chama cha demokrasia na maendeleo( chadema), nimejifunza mengi.

Tangu kuondoka kwa ward Kabour aliyekuwa katibu Mkuu kutokea kigoma na nafasi yake kushikwa na mtaalamu wa sheria,na falsafa ya theolojia,Dr wilbroad Slaa,nimeona hakika kiongozi huyu ni wa kutukuka.

Kuonesha kuwa amefanya kazi kubwa pale alipofanya yafuatayo:

KUIMARISHA TAASISI ZA CHAMA

Alianza na kuwajengea uwezo watumishi wa makao makuu katika nyanja ya kitaalamu na kitaaluma,akawapa nafasi kwenda nje kusoma,akaanzisha kurugenzi ya sheria,kurugenzi ya habari,kurugenzi ya ulinzi na usalama,kurugenzi ya fedha,na kurugenzi nyingine nyingi ambazo zimeiweka chadema kuwa taasisi.

Usishangae unapoona timu ya Tundu Lissu,Tumaine Makene, Mohamed Mtoi,Lwakatare,na John Mrema ( kutaja wachache), ccm imepata kazi kweli kiasi cha kuishi wasiyoyatengeneza.kwa mujibu wa katiba ya chama aliitekeleza


KUUNDA TAASISI

Baada ya kazi hiyo,alianza kujenga taasisi za Bawacha,Bavicha,Chaso na Baraza la wazee..

Hii ilikuwa kazi yake aliyopewa na wanachama wa chadema.amefanya kazi kubwa sana.

Bawacha ambaye ilikuwa na wanachama laki tano 2000,imepelekea kuwa na wanachama milioni tatu nchi nzima.2015

Baraza la vijana,Bavicha kutoka wanachama laki mbili,2000, kwa sasa wanachama wamefikia milioni moja. Na si kuongezeka kwa idadi tu,bali pia mabaraza haya yapo ngazi za chini kabisa ya tawi nchi nzima,huwezi kwenda Itungu,Ikungi,mahaha,longido,kyaka,matemanga,nyamagoto, Misenyi,Madabank usikute ofisi za bawacha na bavicha.

Haikutosha akishirikiana na Mh.Mbowe,na timu yake,waliona chama bila wasomi, akaunda chaso ambaye kusema kweli limekuwa zao la vijana wabunge akina Kafulila,Zitto kabwe, Halima Mdee,Mnyika na wengineo wengi wanaotarajiwa kuwatumikia watanzania kupitia Udiwani na Ubunge Mwaka huu 2015.

Baraza la wazee amelifanikisha kuliimarisha likikishauri chama kwa kiasi kikubwa.
Dr.Slaa akiamini nidhamu,uvumilivu,utu,kiasi na umoja ndio njia ya kujenga Taifa lenye Usawa,na uchapakazi alishauri chama kuwa mwaka 2013 kisingefanya uchaguzi bali kiende ngazi ya kata,tawi na kisha msingi.Uchaguzi wa serikali za mitaa umeonesha matunda ya ushauri wake.kwani chadema imeshinda kwa kishindo kuliko wanavyojinasibu ccm kuwa ushindi mdigo,maana yapo maeneo ambapo tangu uhuru 1961 ccm imekuwa ukitawala vijiji,vitongoji na mitaa,lakini safari hii maeneo hayo yameenda na chadema yote.

Watu makini,kwa kazi makini,hakika Dr.Slaa ni mtu makini asiyeyumba kwenye kusimamia kanuni,katiba sheria na taratibu. Kiongozi ambaye ni very strategic katika mipango yake.
Inaonesha,katika mahojiiano binafsi niliyofanya na watumishi wa serikali ya Tanzania,wanamuona kama kiongozi wa kupigiwa mfano ameijenga chadema viliyo kutoka falsafa ya mtu,kwenda falsafa ya kitaasisi.

Si ajabu unapoongea na watu kupitia mitandao ya kijamii nje na ndani ya nchi, kwenye twitter,facebook,jamiiforum na sciber utakuta wanasema" Dr Slaa ni hazina ya watanzania,
Na hata angepewa nchi hatawaangusha watanzania"

Chadema Kwanza

Slaa ni Mheshimiwa rais awamu ya tano
 
Aliwaambia hawa waliopatwa na balaa hili kuwa mfuko wa cement ungekuwa 5,000 wakapuuzia, sasa ona kuta za nyumba zao zinabomoka kama biskuti!

mafuriko_kahama.jpg
 
Uzuri wa Pro-Chadema mwenzao yeyote akija na pumba kama zinawafurahisha uwa hawezi kuhoji zaidi ya kishangilia tu bila kutimia akili zao.

Huyu mleta mada anawadanganya wenzake kuwa Bavicha na Bakwata wana wanachama milioni 4.

Ukiangalia uchaguzi mkuu ulioshapita Dr.Slaa alipata kura milioni 2 tu Tanzania.

jivue ubongo wa fisi usimix na kiroba weka wa binadamu huu ni mwaka gani na uchaguzi ulikua ni mwaka gani?
 
Dr Slaa ni Kiongozi pia ana sifa ya Utendaji.


wenye sifa kama Dr Slaa ni wachache sana hapa tanzania, kidogo Lowassa kiutendaji ila hana sifa ya uongozi ulio tukuka kama Dr Slaa.

Nakumbuka Dr Slaa uchaguzi ulio pita wapinzani wake walikuwa hawana madhaifu yake zaidi ya ishu binafsi kama vile ndoa na kadhalika. lakini maswala ya kiutendaji na kiuongozi hakuwa na udhaifu wowote.

Dr Slaa ni niongozi na ni mtendaji mzuri na Alie tukuka.
 
Hahaha hata jakaya anajua lazma ampe kijiti slaa la sivyo ataenda the hague kama gbagbo
 
Back
Top Bottom