Dr. Slaa amfunika Lowassa kwenye media

Dr. Slaa amfunika Lowassa kwenye media

Dr Slaa unatakiwa kusoma nyakati. Muvi yako imeshapoteza mvuto. Ni miaka kumi sasa tunakusikia na Richmond tu. Ndio umeikariri hiyo hiyo unasafiria hiyo nyota ya Richmond. Kimsingi hiyo muvi imechuja na watu wamekujua rangi yako sasa na wamekupuuza wanakuona mbabaishaji uliyenunuliwa. Kuashiria kuwa muvi imechuja na watu wanekuchoka Jana umeandaliwa MAHOJIANO MAALUMU KIMKAKATI ili ujisafishe ukatumia energy kubwa kuongea yaleyale ya kila Siku na magazeti ya Leo yooote yamekupuuza hayajaandika hata chembe ya stories zako za mipasho. Umefanya mahojiano saa nne had saa tano ambapo kwa wataalamu wa utayarishaji wa magazeti tunasema kwa muda huu template za magazeti zilikuwa bado hazijaprintiwa na walikiwa na nafasi ya kukupa coverage kwenye magazeti. Amka fedheha inakuja na wanaokutumia wakiona huna impact watakugeuka na kukudump.. Angalia jinsi mbowe na Lowassa anbao ulitegemea watakuja kukujibu ili upate kick na uongee zaidi nao wamekupotezea pia.
 

Attachments

  • 1441429705743.jpg
    1441429705743.jpg
    24.6 KB · Views: 453
Mada yangu haijahusu wagombea Urais. Nimewaima yule aliyetakiww kuwa Mgombea Urais na huyu aliyenunua ugombea Urais

Usijipe moyo, upepo upo kwa Lowasa kuliko huyo Slaa wenu.
Pombe ndo kapotea kama hakuna mgombea wa CCM,.
 
Mkuu, yaani mmechanganyikiwa sana. Huwezi kumpa kazi ya kuleta mabadiliko fisadi. Hapo ndipo mlipojinyea kiganjani
Ufisadi upi? Ina maana mpaka leo somo la Richmond hujalielewa tu. Anyway binadamu hatufanani. Vipi kuhusu nyumba za serikali? Kivuko na mengine ambayo Mh Magufuli, Kikwete na Mkapa wanatuhumiwa nayo. Au ni kufikiri unaweza mpata mtu asiye na tuhuma yoyote. Mh raisi (Lowassa) alishaweka wazi kuhusu hili unataka nn kingine. Nachukia umaskini, vijana kukosa ajira, ebu tuuangalie upande huu nao badala ya kuwa rigid na waoga. Mungu bariki Tanzania.
 
Endelea kujifariji. Utakuwa ni punguani kama utadharau nguvu ya Dr Slaa
Wakati kama huu wa uchaguzi mtu makini hawezi kulinganisha mgombea na asiye mgombea.

You are barking up the wrong tree.
 
Moderator unganisheni na huu UZI au na nyie ni Ccm
Maana wengine tukiweka mawazo mnaunga sasa na huu tunasubiri tuone mtasubiri ufike page ya ngapi.
 
Last edited by a moderator:
Kimsingi jamaa amepoteza mvuto. Magazeti yote Leo yamempotezea na ngonjera zake za mipasho. Soma nyakati Babu
 
nimekujankugundua ww ni mtu muhimu sana kwetu sababu unatushtuaga in advance ww hautak tu kujuonyesha ila lowassa unampenda.Swala la media coverage ss litashugulikiwa tena asante lizaboni.Chadema plz now msimjibu babu muachieni rose ajibishane na mumewe zilipendwa
 
Jiulize wachangiaji wengi kwenye hizo mada mnazoanzisha na kimsingi sio za slaa kwa kuwa maudhui ya hizo mada ni lowasa na ndo maana wachangiaji wengi ni wana mabadiliko
 
Wadau, amani iwe kwenu.

Sasa ni dhahiri kwamba Dr Slaa amemfunika kabisa Lowasa kwenye media. Ukiangalia hata hapa JF utaona kuwa mada nyingi zinazoanzishwa ni zile zinazomhusu Dr Slaa. Pia mada zinazomhusu Slaa zinakuwa na wachangiaji wengi kuliko zile za Lowasa. Hii ni dhahiri kwamba umaarufu wa Dr Slaa ambaye alikuwa mhimili muhimu ndani ya CHADEMA na UKAWA unazidi ule wa Lowasa ambao unazidi kuporomoka kila kukicha.

Watu wa media wamekata tamaa kwa vile fedha walizokuwa wanapewa ili wamwandike vizuri Lowasa zinazidi kupungua kila siku. Vijana wake mitandaoni nao hali ni mbaya sana.

Hakika CHADEMA wanajuuutaaaaa kuchukua fisadi Lowasa. Dr Slaa hakukosea aliposema kuwa walichofanya CHADEMA ni kama kupakua kinyesi kwenye choo na kuweka chumbani kwako. Sasa CHADEMA hapakaliki. Wamekuwa kama wajenzi wa mnara wa Babeli. Kila mtu anasema lake. Wamefikia hatua ya kumlaghai Rose Kamili ili amseme vibaya mzazi mwenzake lakini haijasaidia kitu zaidi ya yule mama kujidhalilisha tu na kudharauliwa na wanawake wenzake.

Dr Slaa unatisha. Mapambano dhidi ya fisadi Lowasa yanaendelea na sisi humu tunazidi kupigilia misumari ya moto. Mpaka Oktoba 25 watakuwa wamechakazwa vibaya na wamekuwa ndembendembe
Mkuu nilijua umeandika cha maana kumbe umeishia kumsifia Dr Slaa huyu huyu uliyemwita Padree.
 
Dr slaa ni nami katika nchi hii? anazidiwa hadi na Savimbi wa bongo,kama huna upendo kwa wanao utakuwa na upendo kwa watz? tunatatizo la uwezo mdogo wa kuchanganua mambo tuache ushabiki.
 
Maskini CCM...wamechanganyikiwa hawaamini kinachoendelea maana mapenzi ya wananchi kwa Lowassa na UKAWA yameongezeka zaidi ya awali, hiyo inaitwa positive feedback.

Uchicheme mapenji chema mahabat.Leo nipo maeneo ya Nzega,Jana nilikuwa Mwanza watu wanamvua nguo Dr Mihogo sijawahi kutegemea.Kumbe heshima ya mtu na mambo makubwa aliyowahi kumiliki huweza kupotezwa na kinywa chake?Ama hakika mdomo huponza kichwa na kukaa kimya ni HEKIMA KUTOKA KWA MUNGU.Huyu kiumbe anayeitwa Lowassa ukitaka kumdhibiti inabidi unyamaze ili apotee kwenye masikio ya watu kinyume na hapo ni kujidanganya tu.VICE-VERSA IS TRUE kwani kipindi cha nyuma sisiem walibishana na slaa alipokuwa anahamasisha watu kukichukia chama hicho pamoja na washirika wake lakini leo wapo pamoja katika kukipaka mafuta chama hicho.Bila kusahau CDM leo wapo na yule papa wa mafisadi wakimtumia kama jiwe fatuma katika kutimiza azma yao.Naona ni bora kila mtu kati yao akakubali mapungufu yake na kuangalia ya mwenzie ambayo yanawezekana kwenda au kupelekwa mahakamani yakapelekwa ili hizi kelele zisizokuwana tija ziishe.
 
Lizaboni sisi ni wa Lowassa, sisi ni wa mabadiliko. Hizo takataka nyingine hatuna habari nazo. Tubadili kwanza mfumo usiwe wa chama kimoja baada ya miaka 5 ukawa nao tunawacheki. Kwa hii nchi ni Mali ya kundi CCM pekee? Chadema na vyama vingine katiba haivitambui? Kwa kufanya hivyo faida inaturudia cc wananchi wa kawaida na kila chama kitakachokuwa kikipata ridhaa hakitafanya makosa. Fuatilia alichotuahidi mwinyi, aliahidi Mkapa, akaahidi Kikwete na sasa anaahidi Magufuli miaka 54. Hapana walichofanya hakiendani na muda tuliowapa. Ni wakati wa UKAWA kuitawala. Mungu bariki Tanzania.

Lizaboni=ahadi ya u-dc=Lumumba propagandist=ant mabadiliko=mfumo pingwa=chama chawala etc.Kama humjui endelea kujisumbua kumshauri upoteze wino wa smartphone yako bure.
 
Kaka achana na Dr Slaa kwa sasa unapaswa ulinganishe Lowassa na Magufuli. Huyo Slaa wenu tuachieni siye wananchi tunajua nini cha kufanya, ashapuuuziwa kitambo sana ndo maana unaona magazeti yote leo kimyaaa. Hakuna anayejali, mtamtumia kwa muda tuu na mtamtema vilevile.
Lizaboni
 
Last edited by a moderator:
pombe yupo wapi au dr slaa ndio mgombea wa ccm ?

Nyie watu wa Ukawa narudia kusema, hamjielewi, Dr kamaliza saa4 kuhojiwa ni vp magazeti yangeandika na kuhariri habari alafu itoke leo.Zitatoka kesho.
 
Back
Top Bottom