Katibu Mkuu wa CHADEMA Dr Wilbroad Slaa ameshtushwa na Ikulu ya Tanzania kuwalinda wezi wa kashfa ya Escrow ikiwa ni zaidi ya wiki moja tangu Bunge lipitishe hoja ya kuwafukuza mawaziri wawili na mwanasheria mkuu wa Serikali.
Akihutubia Mkutano wa hadhara katika viwanja vya Manzese Tip Top jijini DSM kiongozi huyo kipenzi cha watanzania amelaani hatua ya kupuuza maamuzi ya bunge hadi sasa.
Kiongozi huyo mwenye msimamo mkali dhidi ya wezi wa mali ya Umma ameshangazwa na jeuri ya mawaziri Sospeter Muhongo na Anna Tibaijuka waliokula kiapo cha kukataa kujiuzulu huku Rais akikaa kimya bila kuwafukuza mara moja.
Dr Slaa anayeombwa na watanzania wengi kugombea Urais mwakani ameonya vikali tabia ya watu kukimbilia Ikulu kwa maslahi yao.
Dr Slaa amemtaka Rais Jakaya Kikwete kutoka hadharani kupinga maneno yake kama kweli Ikulu haiwalindi wezi wa Escrow.
Dr Slaa ambaye amekuwa kinara mkuu wa kupigia kelele wizi wa kashfa ya Escrow nje ya Bunge ameonya watanzania wasiichague CCM kwenye uchaguzi wa Serikali za mitaa bali wachague wagombea wa UKAWA
Akihutubia Mkutano wa hadhara katika viwanja vya Manzese Tip Top jijini DSM kiongozi huyo kipenzi cha watanzania amelaani hatua ya kupuuza maamuzi ya bunge hadi sasa.
Kiongozi huyo mwenye msimamo mkali dhidi ya wezi wa mali ya Umma ameshangazwa na jeuri ya mawaziri Sospeter Muhongo na Anna Tibaijuka waliokula kiapo cha kukataa kujiuzulu huku Rais akikaa kimya bila kuwafukuza mara moja.
Dr Slaa anayeombwa na watanzania wengi kugombea Urais mwakani ameonya vikali tabia ya watu kukimbilia Ikulu kwa maslahi yao.
Dr Slaa amemtaka Rais Jakaya Kikwete kutoka hadharani kupinga maneno yake kama kweli Ikulu haiwalindi wezi wa Escrow.
Dr Slaa ambaye amekuwa kinara mkuu wa kupigia kelele wizi wa kashfa ya Escrow nje ya Bunge ameonya watanzania wasiichague CCM kwenye uchaguzi wa Serikali za mitaa bali wachague wagombea wa UKAWA