Brooklyn
JF-Expert Member
- Mar 17, 2009
- 1,459
- 284
Jana katika taarifa mbalimbali za habari, Makamu wa Rais Mh. Dr. Shein alisikika akiwahutubia wananchi kwamba serikali inatambua matatizo ya waalimu kama ambavyo yeye na viongozi wenzanke wanavyoyafahamu majina yao, sanjari na hilo, akitembelea kivuko cha Kilombero, alikaririwa akisema serikali inakumbuka ahadi zote ilizotoa mwaka 2005 juu ya kuwapatia wananchi wa Kilombero kivuko kipya, na kwamba wataalamu wako kwenye upembuzi yakinifu ili kuhakikisha suala hilo linapatiwa ufumbuzi wa kudumu.
Binafsi namuheshimu sana kiongozi huyu, ambaye ameonekana ni mtulivu pengine kuliko viongozi wengi katika baraza la mawaziri la awamu ya nne. Lakini kauli zake za hivi karibuni zimeanza kunipa hofu kwamba pengine mheshimiwa ameanza kuingia kwenye kauli za "kisiasa" zaidi ambazo hazilingani na jinsi alivyojipambanua katika jamii.
Watanzania tumechoka na kauli kama hizi, upembuzi gani unaofanyika toka mwaka 2006?? Kama matatizo ya waalimu wanayafahamu vyema, kwa nini wasiyatafutie suluhisho la kudumu???
Binafsi namuheshimu sana kiongozi huyu, ambaye ameonekana ni mtulivu pengine kuliko viongozi wengi katika baraza la mawaziri la awamu ya nne. Lakini kauli zake za hivi karibuni zimeanza kunipa hofu kwamba pengine mheshimiwa ameanza kuingia kwenye kauli za "kisiasa" zaidi ambazo hazilingani na jinsi alivyojipambanua katika jamii.
Watanzania tumechoka na kauli kama hizi, upembuzi gani unaofanyika toka mwaka 2006?? Kama matatizo ya waalimu wanayafahamu vyema, kwa nini wasiyatafutie suluhisho la kudumu???