Dr. Shein, kosa letu ni kumkatalia Bakar Asseid kugawa eneo letu nusu kwa nusu

figganigga

JF-Expert Member
Oct 17, 2010
25,492
54,890
Na O.Juma,

DK. SHEIN, KOSA LETU NI KUMKATALIA BAKARI ASSEID NA WAPAMBE WAKE WA WIZARA YA KILIMO PEMBA KUGAWANA ENEO LETU NUSU KWA NUSU KAMA KIKOMBOLEO CHA KUPATA HAKI YETU.

Mnamo tarehe 9/6/2017 nilibahatika kusoma makala katika Mzalendo .net yenye kichwa cha habari isemayo:-
“SULUHISHO LA MGOGORO WA MSITU WA NGEZI NA MASHAMBA YA WANANCHI”

Baada ya kuipitia mara kadhaa makala hii, nilivutiwa na jinsi ilivyo wasilishwa nikahisi uko umuhimu wa kufatilia jambo hili kwa kina nikiwa kama mwanaharakati niliye jikita zaidi katika kufatilia migogoro ya ardhi hapa nchini kwetu.

Hatua hii ilikuja kunipa hamasa zaidi baada ya kuangalia Baraza la wawakilishi na kuona baadhi ya wajumbe wakiligusia suala hili wakiwemo mwakilishi wa jimbo la Welezo Mhe. Hassan Hamis na mwakilishi wa jimbo la Tunguu Mhe Simai Mohammed Said, Ambapo walidai kuna eneo la msitu wa hifadhi wa Ngezi umepimwa viwanja, na Mhe. Hamad Rashid waziri wa kilimo alizing’oa Beacon zilizo wekwa na watendaji wa wizara ya ardhi bila ya kushauriana na waziri mwenzake, Jambo ambalo ni ukosefu wa maadili ya uongozi na angepaswa kumuomba radhi aliye mteua pia kumuomba radhi waziri mwenzake, zaidi ya yote alipaswa kujiuzulu nafasi yake, kwani kitendo alicho kifanya ni cha kumdhalilisha waziri mwenzake tena hadharani, hivyo basi kimempelekea kukosa sifa za kuwa kiongozi katika jamii iliyo staarabika kama Zanzibar.

Baada ya kufatilia kwa kina nilikutana na wananchi ambao ni wahusika na wao hawakusita walitaka niwafikishie ujumbe wao panapo husika.
Ukweli ni kwamba wananchi hao walinionyesha document mbalimbali zinazo thibitisha kuwa eneo hilo ni mali yao zikiwemo barua za Serikali zinazo elezea kupimiwa na kupewa haki yao, Tatizo walinitajia mtu anae itwa Bakari Asseid.

Wanasema mtu huyu alishawaambia kwamba wakubali eneo hilo ligaiwe nusu kwa nusu yaani nusu liende kwa wananchi na nusu liende mikononi mwake na wapambe wake ikiwa wanataka haki yao, Vyenginevyo yeye hawezi kulizuwia eneo mda wote alio lizuwia halafu asipate faida yoyote.

Ikiwa wananchi hao watakataa atatumia ushawishi alionao Serikalini kuwaaminisha viongozi wakuu wa serikali kuwa eneo hilo ni msitu japo liko nje ya msitu, kigezo kikubwa atakacho kitumia ni kuwemo kwa miti mingi kwa vile eneo hilo wamelizuwia lisitumike kwa shughuli yoyote tena kwa muda mrefu. Aliendelea kwa kusema kigezo hicho tu, kitatosha kuliita eneo hilo kuwa ni msitu hivyo wananchi hao wachaguwe mawili. Aidha wakubali kutoa nusu eneo au wakatae eneo hilo ligeuzwe kuwa msitu wa Vumawimbi, ajabu sio msitu wa Ngezi kwa maana msitu wa Ngezi unajulikana ulipo pita ni takriban kilomita moja na yalipo mashamba hayo na umepimwa umepewa kiwanja namba 14 Makangale, Ramani yake halisi ipo na Beacon zake zipo. Huo ni msitu wa “Vumawimbi” wawakilishi wajuwe hilo, likini ikiwa wananchi wangekubali wagawane eneo hilo nusu kwa nusu na bwana huyo basi msitu huo wa Vumawimbi usinge kuwepo.

Ajabu ilioje, Jee! wanaweza kuugawa Msitu wa Jozani nusu kwa nusu endapo wananchi watakubali nusu ya msitu huo uende kwa Bakari Asseid? Jibu ni hapana. Hilo haliwezekani. Kitendo cha Bakari Asseid kuomba apewe nusu ya eneo analodai kuwa ni msitu wa serikani ni kithibitisho tosha kuwa eneo hilo sio mstitu kama anavyo dai ila kinachofanyika ni kiinimacho na hasadi kwa wamiliki wa eneo hilo. Ikumbukwe mwaka 1998 eneo hili lilikuwa miongoni mwa maeneo yaliyotangazwa kuwa ni maeneo ya utalii Zanzibar kupitia gazeti rasmi la serikali la mwaka 1998 Toleo CVII Namba 5785.

Tunamuomba Hamad Rashid amuulize Bakari Asseid anachukuwa mali ya watu na kuiingiza serikalini
Jee! Amewalipa fidia wananchi kama katiba ya Zanzibar ya 1984 toleo la 1995 kifungu 17/C kuhusiana ulipwaji wa fidia unao lingana na mali ya wananchi inayo chukuliwa na serikali? Au anafanya tu kwa matamanio ya nafsi yake?

Hamad Rashid Muogope Mungu mwisho wetu nikutiwa kwenye mwana wa ndani, usimuendekeze dhalim atakupoteza, huko mbele ya Mungu kila anae kushawishi udhulumu atakukimbia mzigo wanao kubebesha ni mzito.

DK. Shein, Bakari Asseid aliwatisha wananchi kwa kuwaambia kuwa yeye ndiye semaji wa mwisho akiamua eneo liitwe msitu basi Rais hawezi kulikataa hilo, Rais hato msikiliza waziri,katibu wa mkurugenzi yoyote baada ya kutoa maamuzi yake, hivyo endapo wananchi hao watakataa atapigana mpaka tone lake la mwisho la damu lakini atahakikisha wananchi hao hawapati haki yao hata wakapewa barua na kiongozi gani yeye atapinga kwa vitendo. Hivyo aliwaonya wasijaribu kutafuta njia yoyote ya kumfikia Raisi kwa suala hili, wakikataa wataishia kukosa haki zao kwa Rais hamsikilizi mtu yeyote zaidi yake. Bila shaka ndio ndio maana akamshawishi Hamad Rashid akang’oa beacon zilizo wekwa kisheria.

Nilicho gundua kilicho kuwepo sio mgogoro wa wananchi na serikali yao kwani kwa barua nilizi ziona za viongozi
wakuu wa serikali ni wazi serikali hana mgogoro na wananchi wake bali mgogoro uliokuwepo ni Bakari Asseid na wapambe wake kwa maslahi yao binafsi dhidi ya maamuzi ya Serikali(barua za viongozi wakuu), Mahakama na wananchi wanao miliki eneo husika.

Mwisho kabisa wananchi hawa wanasema wako tayari kutoa ushahidi wa haya waliyo yaeleza mbele ya Rais na Bakari Asseid akiwepo ili mkweli ajulikane ikiwa watatakiwa kufanya hivyo.

Sisi kama wanaharakati wa kupigania haki za wananchi, Tunakuomba DK. Shein uyachukulie kwa uzito madai haya ikiwezekana uende ziara eneo husika kwa kulitambua eneo la msitu wa Ngezi lililopimwa kisheria mwaka 1998 kwa mujibu wa ramani ili ikithibitika kuwa maeneo wanayodai wananchi hao hayamo katika msitu wa Ngezi uliopimwa kisheria mwaka 1997 basi wananchi hao wapewe haki yao ili mgogoro huu umalizike kwa amani.
Tunategemea ombi letu utalikubali.

Chanzo: Mzalendo
 
Na O.Juma,

DK. SHEIN, KOSA LETU NI KUMKATALIA BAKARI ASSEID NA WAPAMBE WAKE WA WIZARA YA KILIMO PEMBA KUGAWANA ENEO LETU NUSU KWA NUSU KAMA KIKOMBOLEO CHA KUPATA HAKI YETU.

Mnamo tarehe 9/6/2017 nilibahatika kusoma makala katika Mzalendo .net yenye kichwa cha habari isemayo:-
“SULUHISHO LA MGOGORO WA MSITU WA NGEZI NA MASHAMBA YA WANANCHI”

Baada ya kuipitia mara kadhaa makala hii, nilivutiwa na jinsi ilivyo wasilishwa nikahisi uko umuhimu wa kufatilia jambo hili kwa kina nikiwa kama mwanaharakati niliye jikita zaidi katika kufatilia migogoro ya ardhi hapa nchini kwetu.

Hatua hii ilikuja kunipa hamasa zaidi baada ya kuangalia Baraza la wawakilishi na kuona baadhi ya wajumbe wakiligusia suala hili wakiwemo mwakilishi wa jimbo la Welezo Mhe. Hassan Hamis na mwakilishi wa jimbo la Tunguu Mhe Simai Mohammed Said, Ambapo walidai kuna eneo la msitu wa hifadhi wa Ngezi umepimwa viwanja, na Mhe. Hamad Rashid waziri wa kilimo alizing’oa Beacon zilizo wekwa na watendaji wa wizara ya ardhi bila ya kushauriana na waziri mwenzake, Jambo ambalo ni ukosefu wa maadili ya uongozi na angepaswa kumuomba radhi aliye mteua pia kumuomba radhi waziri mwenzake, zaidi ya yote alipaswa kujiuzulu nafasi yake, kwani kitendo alicho kifanya ni cha kumdhalilisha waziri mwenzake tena hadharani, hivyo basi kimempelekea kukosa sifa za kuwa kiongozi katika jamii iliyo staarabika kama Zanzibar.

Baada ya kufatilia kwa kina nilikutana na wananchi ambao ni wahusika na wao hawakusita walitaka niwafikishie ujumbe wao panapo husika.
Ukweli ni kwamba wananchi hao walinionyesha document mbalimbali zinazo thibitisha kuwa eneo hilo ni mali yao zikiwemo barua za Serikali zinazo elezea kupimiwa na kupewa haki yao, Tatizo walinitajia mtu anae itwa Bakari Asseid.

Wanasema mtu huyu alishawaambia kwamba wakubali eneo hilo ligaiwe nusu kwa nusu yaani nusu liende kwa wananchi na nusu liende mikononi mwake na wapambe wake ikiwa wanataka haki yao, Vyenginevyo yeye hawezi kulizuwia eneo mda wote alio lizuwia halafu asipate faida yoyote.

Ikiwa wananchi hao watakataa atatumia ushawishi alionao Serikalini kuwaaminisha viongozi wakuu wa serikali kuwa eneo hilo ni msitu japo liko nje ya msitu, kigezo kikubwa atakacho kitumia ni kuwemo kwa miti mingi kwa vile eneo hilo wamelizuwia lisitumike kwa shughuli yoyote tena kwa muda mrefu. Aliendelea kwa kusema kigezo hicho tu, kitatosha kuliita eneo hilo kuwa ni msitu hivyo wananchi hao wachaguwe mawili. Aidha wakubali kutoa nusu eneo au wakatae eneo hilo ligeuzwe kuwa msitu wa Vumawimbi, ajabu sio msitu wa Ngezi kwa maana msitu wa Ngezi unajulikana ulipo pita ni takriban kilomita moja na yalipo mashamba hayo na umepimwa umepewa kiwanja namba 14 Makangale, Ramani yake halisi ipo na Beacon zake zipo. Huo ni msitu wa “Vumawimbi” wawakilishi wajuwe hilo, likini ikiwa wananchi wangekubali wagawane eneo hilo nusu kwa nusu na bwana huyo basi msitu huo wa Vumawimbi usinge kuwepo.

Ajabu ilioje, Jee! wanaweza kuugawa Msitu wa Jozani nusu kwa nusu endapo wananchi watakubali nusu ya msitu huo uende kwa Bakari Asseid? Jibu ni hapana. Hilo haliwezekani. Kitendo cha Bakari Asseid kuomba apewe nusu ya eneo analodai kuwa ni msitu wa serikani ni kithibitisho tosha kuwa eneo hilo sio mstitu kama anavyo dai ila kinachofanyika ni kiinimacho na hasadi kwa wamiliki wa eneo hilo. Ikumbukwe mwaka 1998 eneo hili lilikuwa miongoni mwa maeneo yaliyotangazwa kuwa ni maeneo ya utalii Zanzibar kupitia gazeti rasmi la serikali la mwaka 1998 Toleo CVII Namba 5785.

Tunamuomba Hamad Rashid amuulize Bakari Asseid anachukuwa mali ya watu na kuiingiza serikalini
Jee! Amewalipa fidia wananchi kama katiba ya Zanzibar ya 1984 toleo la 1995 kifungu 17/C kuhusiana ulipwaji wa fidia unao lingana na mali ya wananchi inayo chukuliwa na serikali? Au anafanya tu kwa matamanio ya nafsi yake?

Hamad Rashid Muogope Mungu mwisho wetu nikutiwa kwenye mwana wa ndani, usimuendekeze dhalim atakupoteza, huko mbele ya Mungu kila anae kushawishi udhulumu atakukimbia mzigo wanao kubebesha ni mzito.

DK. Shein, Bakari Asseid aliwatisha wananchi kwa kuwaambia kuwa yeye ndiye semaji wa mwisho akiamua eneo liitwe msitu basi Rais hawezi kulikataa hilo, Rais hato msikiliza waziri,katibu wa mkurugenzi yoyote baada ya kutoa maamuzi yake, hivyo endapo wananchi hao watakataa atapigana mpaka tone lake la mwisho la damu lakini atahakikisha wananchi hao hawapati haki yao hata wakapewa barua na kiongozi gani yeye atapinga kwa vitendo. Hivyo aliwaonya wasijaribu kutafuta njia yoyote ya kumfikia Raisi kwa suala hili, wakikataa wataishia kukosa haki zao kwa Rais hamsikilizi mtu yeyote zaidi yake. Bila shaka ndio ndio maana akamshawishi Hamad Rashid akang’oa beacon zilizo wekwa kisheria.

Nilicho gundua kilicho kuwepo sio mgogoro wa wananchi na serikali yao kwani kwa barua nilizi ziona za viongozi
wakuu wa serikali ni wazi serikali hana mgogoro na wananchi wake bali mgogoro uliokuwepo ni Bakari Asseid na wapambe wake kwa maslahi yao binafsi dhidi ya maamuzi ya Serikali(barua za viongozi wakuu), Mahakama na wananchi wanao miliki eneo husika.

Mwisho kabisa wananchi hawa wanasema wako tayari kutoa ushahidi wa haya waliyo yaeleza mbele ya Rais na Bakari Asseid akiwepo ili mkweli ajulikane ikiwa watatakiwa kufanya hivyo.

Sisi kama wanaharakati wa kupigania haki za wananchi, Tunakuomba DK. Shein uyachukulie kwa uzito madai haya ikiwezekana uende ziara eneo husika kwa kulitambua eneo la msitu wa Ngezi lililopimwa kisheria mwaka 1998 kwa mujibu wa ramani ili ikithibitika kuwa maeneo wanayodai wananchi hao hayamo katika msitu wa Ngezi uliopimwa kisheria mwaka 1997 basi wananchi hao wapewe haki yao ili mgogoro huu umalizike kwa amani.
Tunategemea ombi letu utalikubali.

Chanzo: Mzalendo
Hii habari ingetolewa kwenye Magazeti makini wananchi wengi wangepata ujumbe, mimi mwenyewe bila JF nisingepata ujumbe huu
 
Back
Top Bottom