Dr. Nchimbi, the beginning of an end

Dr. Nchimbi, the beginning of an end

Duh kweli CCM wababe sana Dr wetu ndio hivyo tena kwishey.

CCM ni wababe mithili ya Mbowe kumpitisha EL kuwa mgombea pekee wa nafasi ya urais ndani ya UKAWA bila kushindanishwa na mtu yeyote. Afadhali CCM angalau wanatupa viini macho vya watu kushindanishwa kuliko UKAWA wa Mbowe!
 
Nchimbi hakugombea ubunge kule Songea. Alitoka mbio kupinga maamuzi ya kamati kuu ya CCM kumpitisha Lowassa. Hakuhama chama. Akarudi kuiomba kamati kuu impitishe awe mgombea uspika, ikambwaga. Nini hatma yake? Je, ndio amefika ukingoni katika siasa?


Ya Nchimbi; CCM na matumizi mabaya ya Vijana!. ''Ndiyo mzee''
Nchimbi anatakiwa kujifunza jambo namshauri ajiunge na Mhe.Zitto na kabla ya kufanya hivyo amtembelee Malema S.A!

cc Juliana Shonza
 
Last edited by a moderator:
Ya Nchimbi; CCM na matumizi mabaya ya Vijana!. ''Ndiyo mzee''
Nchimbi anatakiwa kujifunza jambo namshauri ajiunge na Mhe.Zitto na kabla ya kufanya hivyo amtembelee Malema S.A!

cc Juliana Shonza
Cha kujiuliza pia, ni sahihi kupinga maamuzi ya taasisi au chama chako hadharani? Anaonewa au ameponzwa na upofu wa kukurupuka?
 
Last edited by a moderator:
Nchimbi hakugombea ubunge kule Songea. Alitoka mbio kupinga maamuzi ya kamati kuu ya CCM kumpitisha Lowassa. Hakuhama chama. Akarudi kuiomba kamati kuu impitishe awe mgombea uspika, ikambwaga. Nini hatma yake? Je, ndio amefika ukingoni katika siasa?
Kama kuna kitu cha kijinga ambacho Nchimbi alifanya ni kupinga maamuzi ya CC hadharani.
Halafu unampinga mwenyekiti wa chama CCM aliyeshika mpini!!!
Kundi hilo hilo kama vile tusi la usoni likaimba mbele ya mwenyekiti wa CCM, "Tuna Imani na Lowassa .....oyaaa....oyaaaa....oyaaaa"

Pili kupinga kule kulikuwa kwa matakwa binafsi yaliyotokana na kuahidiwa kitu na Lowassa.
Damage ile kwa ushawishi wake ilikuwa kubwa mno.

Lowassa huyoo akakihama chama, nuksi nyingine kwa walio msapoti.
yu Nchimbi kwa sasa hawezi kuaminika kwa lolote, alimradi nafsi yake iko kwa Lowassa.
 
Cha kujiuliza pia, ni sahihi kupinga maamuzi ya taasisi au chama chako hadharani? Anaonewa au ameponzwa na upofu wa kukurupuka?

Exactly!na kupinga kutokana na kuwa mtu wako amekatwa....yeye na Sofia Simba hakuna namba wataacha kuisoma
 
Katika watu ambao walibugi ni huyu jamaa alikuwa ana nafasi kubwa sana ya kupitishwa akaacha kugombea
 
Kusema haki haikutumika ndani ya kamati kuu ndicho kinachomla Nchimbi! Visasi vya kijinga tena wakubwa ni vibaya na ni kiburi na machukizo hata kwa mola. na watoto wao watakuja kufanyiwa hivyo hivyo kwani ni laana!
Kimtazamo wa kiimani unaweza kusema hivyo. Kumbuka kwamba usipoweka misingi ya kinidhamu katika Taasisi kila mtu atakurupuka na kuropoka na heshima itapotea. Kila Taasisi ambayo ni imara ina njia na taratibu zake za kutatua matatizo. Ninachoweza kukiona ni kwamba CCM wamekuwa waoga saana wa kufukuza watu uanachama, huyu atawagharimu muda si mrefu. Inatakiwa Taasisi kwanza na si jina mtu. Ningependa nikutolee mfano wa kwenye mpira kama ni mfuatiliaji; Meneja aliyepita wa Manchester United alikuwa na falsafa kwamba hakuna mtu mkubwa kuliko klabu. David Beckham alivyoanza kupaa akamsogezea Madrid, vivyo hivyo kwa Ryan Giggs. Baadae Man Utd waliendelea kupata mafanikio. Isitokee mtu mmoja akawa mkubwa kuliko Taasisi, huo ni udhaifu.
 
Back
Top Bottom