Wanasiasa wetu pamoja na viongozi wa serikali waandamizi wanachekesha kama siyo kushangaza.
Wabunge wanalalamika kila siku TAKUKURU haina meno na cha kushangaza hata Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Utawala Bora, George Mkuchika na yeye anadai TAKUKURU haina meno!.
Haya makelele niya kujiosha na kujitakasa kisiasa huku wakikimbia majukumu yao kwa njia hii kwa vile karibia wote siyo wasafi ikichukuliwa kuwa siyo serikali pekee inayopaswa kupeleka hoja au mswaada bungeni wa marekebisho ya sheria peke yake.
Kwao wanaona bora waendelee kuwa na ofisi ya DPP kama ndiye ultimate dicider of corruption cases kwa vile wanaweza kumshake kwa njia yoyote wanayopenda na inakuwa rahisi kwake kuimaliza case iliyofika mahakamani na ambayo haijafika mahakamani bila kuulizwa kwa nini kwa vile tu ana nguvu kisheria za karibia na nguvu za 'Mungu'
Hakuna mwanasiasa au mfanyakazi wa serikali mwandamizi mwenye ubavu wa kujitia kitanzi cha kisiasa au kimaslahi mwenyewe.