Dr Kitila Mkumbo amwanika Mwigulu Nchemba

Dr Kitila Mkumbo amwanika Mwigulu Nchemba

Mwigulu hachafuki hata mkijikusanya na kutumia matope ya aina yoyote.

CHADEMA mlikuwa mmezoea vya kunyonga kwa sasa hali ya kisiasa ndani ya CCM imebadilika na kwa sasa tunawaletea vya kuchinja na kama mlivyo weupe kihoja, vimewashinda.

CHADEMA hawana hoja tena mezani kwa sababu ngoma ya hoja ya ufisadi mlio wake wananchi wameuchoka kuusikia ikichukuliwa kuwa ndani ya CHADEMA kuna ufisadi wa kila siku unaoharalishwa kupitia CHADEMA Central Commettee.

Baada ya kuwajibu hoja zao kwa sasa wanakuja na style ya political cherry picking. Huyu Dr. Kitila hata watu wa kijijini kwake hawakumpa kura halafu ndiyo anapata moral authority ya kuisemea Tanzania. He's making hullabaloo for nothing.

Dr. Kitila. Welcomme to ground zero.

22nd March 2013

Posts : 1,005

Tunashinda na tunakesha hapa hapa,tunalipwa buku 7
 
Mwingulu anautisha uzalendo wa watu walio wengi...

Lets stand...everybody at his respective place...then, we gonna take over!
 
Tusimlaumu Mwigullu kwa hali ya kisiasa ilivyo hapa nch, hata ccm wakimsimamisha jk azisimamie hzo chaguz ndogondogo bado haitasaidia na chama cha mabomu {CCM} wataendelea kuangukia pua kutokana na kutokukubalika huku uraian.....! Chezea chakula Cha FIKRA {M4C} wananch wa leo fikra zao zinaafya huwez wadanganya tena....! CHADEMA YATOSHA
 
Mjumbe wa Kamati Kuu CHADEMA na msomi aliyebobea Dr Kitila Mkumbo amesema CCM sasa imezidi kufubaa na kupauka.

Dr Kitila amesema kwa mwaka huu tu CCM imepoteza kata 7 walizokuwa wanashikilia kwa Chadema.

Dr Kitila amesema lililo wazi ni kwamba chaguzi ndogo sasa hivi ndani ya CCM zinasimamiwa na kijana mdogo aliyejaa dharau,kiburi na ulevi wa madaraka anayeitwa Mwigulu Nchemba.

Dr Kitila ameendelea kusema kijana huyu kutokana na dharau zake wananchi sasa wamekuwa wakichukua taswira yake kama ndiyo taswira ya CCM.

Amesema lililo wazi katika kata zote zilizofanya uchaguzi awamu hii ambapo kijana huyu aliweka kambi CCM ilianguka vibaya.

Kata ambazo Mwigulu aliweka kambi ni Kata za Iseke Singida,Iyela Mbeya,Dongobesh Mbulu na Arusha mjini ambapo kote CCM iliangukia pua isipokuwa Arusha ambapo uchaguzi wake utakuwa tarehe 30 June.

Dr Kitila amehitimisha kwa kusema anakumbuka enzi za John Malecela maarufu kama Tingatinga alipokuwa anasimamia chaguzi za chama hicho kwa weledi mkubwa ambapo ilikuwa ni ndoto kwa kata iliyokuwa inashikiliwa na CCM kunyakuliwa na upinzani.

Source:Raia Mwema.

Mh Dr Kitila Mkumbo kwanini unamfumbulia fumbo hili "Mjinga" ungeacha kuwapa taswira ili wakumbuke kukiwa kumekucha. Mwigullu hajafahamu siasa za CCM kama utakumbuka yule aliyekuwa Mkuu wa Propaganda wa CCM aliyekuwa akitukana wapinzani, CCM walipoona wame "bugi" wakamtema hadi leo hata jina binafsi nimemsahau.
 
Na kwa kuonyesha ya kwamba amechokwa bwana Mwigulu Nchemba yaani ni lazima jimbo lake liondoke na kuchukuliwa na msomi maarufu Mh Dr Kitila Mkumbo.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Na kwa kuonyesha ya kwamba amechokwa bwana Mwigulu Nchemba yaani ni lazima jimbo lake liondoke na kuchukuliwa na msomi maarufu Mh Dr Kitila Mkumbo.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums

Hilo liko dhahiri na Chadema itampa kila aina ya Sapoti Dr Kitila kumuondoa huyu kijana aliyejaa dharau na kiburi anayefikia mahali pa kujilinganisha na Mungu.

Atapewa hata helikopta kuzunguka nayo katika kipindi chote cha kampeni kuwafumbua macho wana Iramba.

Chadema uwezo huo tunao.
 
mtu ana doma linamwaga matusi mazito! Kwenye facebook alikuwa anawadhalilisha dada zetu kisa wanaenda mwezi! Ni mwanasiasa mchafu wa maneno.. Hana hekima kwa kweli..
Bila kuweka unazi viongozi wengi wa ccm kwa sasa si viongozi.. Ni watu wa ajabu ajabu.. Sijui wameokotwa wapi..

mirembe,
 
mwigulu mwiba wa CHADEMA

Mimi hoja hii ningeweza kuikubali kama huo ushahidi wake alionao akidai hata mbinguini ataonyesha kama angekuwa na ujasiri wa kupeleka police ili wao wafanye uchunguzi kwa tuhuma zote cdm wanazotuhumiwa;kinyume cha hapo hana ubavu
 
Mimi hoja hii ningeweza kuikubali kama huo ushahidi wake alionao akidai hata mbinguini ataonyesha kama angekuwa na ujasiri wa kupeleka police ili wao wafanye uchunguzi kwa tuhuma zote cdm wanazotuhumiwa;kinyume cha hapo hana ubavu

Umeongea kweli mkuu
 
Mtu anayeiungamkono CCM ama ni fisadi, ama ana ndugu mafisadi huko ama ni mbumbumbu. Mtu mkweli na mwenye kuitakia mema nchi hii hawezi kuishabikia wala kuipenda CCM
 
Tufike mahali sasa tuache kumjadili tunampa publicity ya Bure maana kila ukichungulia JF Mwiguli, mwigulu savimbi!!!! mimi nimeshaboreka kwa kweli!!!
 
Back
Top Bottom