Mjumbe wa Kamati Kuu CHADEMA na msomi aliyebobea Dr Kitila Mkumbo amesema CCM sasa imezidi kufubaa na kupauka.
Dr Kitila amesema kwa mwaka huu tu CCM imepoteza kata 7 walizokuwa wanashikilia kwa Chadema.
Dr Kitila amesema lililo wazi ni kwamba chaguzi ndogo sasa hivi ndani ya CCM zinasimamiwa na kijana mdogo aliyejaa dharau,kiburi na ulevi wa madaraka anayeitwa Mwigulu Nchemba.
Dr Kitila ameendelea kusema kijana huyu kutokana na dharau zake wananchi sasa wamekuwa wakichukua taswira yake kama ndiyo taswira ya CCM.
Amesema lililo wazi katika kata zote zilizofanya uchaguzi awamu hii ambapo kijana huyu aliweka kambi CCM ilianguka vibaya.
Kata ambazo Mwigulu aliweka kambi ni Kata za Iseke Singida,Iyela Mbeya,Dongobesh Mbulu na Arusha mjini ambapo kote CCM iliangukia pua isipokuwa Arusha ambapo uchaguzi wake utakuwa tarehe 30 June.
Dr Kitila amehitimisha kwa kusema anakumbuka enzi za John Malecela maarufu kama Tingatinga alipokuwa anasimamia chaguzi za chama hicho kwa weledi mkubwa ambapo ilikuwa ni ndoto kwa kata iliyokuwa inashikiliwa na CCM kunyakuliwa na upinzani.
Source:Raia Mwema.
Dr Kitila amesema kwa mwaka huu tu CCM imepoteza kata 7 walizokuwa wanashikilia kwa Chadema.
Dr Kitila amesema lililo wazi ni kwamba chaguzi ndogo sasa hivi ndani ya CCM zinasimamiwa na kijana mdogo aliyejaa dharau,kiburi na ulevi wa madaraka anayeitwa Mwigulu Nchemba.
Dr Kitila ameendelea kusema kijana huyu kutokana na dharau zake wananchi sasa wamekuwa wakichukua taswira yake kama ndiyo taswira ya CCM.
Amesema lililo wazi katika kata zote zilizofanya uchaguzi awamu hii ambapo kijana huyu aliweka kambi CCM ilianguka vibaya.
Kata ambazo Mwigulu aliweka kambi ni Kata za Iseke Singida,Iyela Mbeya,Dongobesh Mbulu na Arusha mjini ambapo kote CCM iliangukia pua isipokuwa Arusha ambapo uchaguzi wake utakuwa tarehe 30 June.
Dr Kitila amehitimisha kwa kusema anakumbuka enzi za John Malecela maarufu kama Tingatinga alipokuwa anasimamia chaguzi za chama hicho kwa weledi mkubwa ambapo ilikuwa ni ndoto kwa kata iliyokuwa inashikiliwa na CCM kunyakuliwa na upinzani.
Source:Raia Mwema.