Dr. Kitila ampa tabu Thabo Mbeki


Utashabikia swali ambalo hata hulijui?

Kama halikuwa swali bali tusi kwa Mbeki kwa nini ajibu?

Kama ni swali ambalo haliendani na mada husika kwa nini ajibu, hususan kama limeulizwa kifedhuli?

Hapa muite huyo Kitila unaemuaminia sana atueleze swali alilouliza kwanza kabla ya kuanza kumpamba kwa jumla jumla
 
Nadhani swali lilikuwa stahili na kama kweli ni muungwana alitakiwa kutoa majibu, kuwa na kiongozi mkubwa wa aina yake halafu unatoa majibu mepesi kwenye masuala sensitive yahusuyo maisha ya watu ni makosa makubwa. Ufafanuzi wake unahitajika ili kuweka mambo sawa-lakini kwa upande mwingine viongozi hawa wa SA wananishangazi kwe misimamo yao kwenye suala hili la ukimwi; kuna huyu aliyepo sasa yeye alisema baada ya kumbaka yule mtoto wa rafiki yake kavukavu alikimbilia bafuni kuoga ili asipate ukimwi!!! Sisi maamuma tukisikia kauli kama hizi nim rahisi kuziamini na ndio inakuwa kiam chetu
 
Mimi nna shaka kuwa hajauliza hili swali kama lilivyoanishwa hapa
Dk. Kitila Mkumbo tafadhali njoo utupe swali ulilouliza tulijadili.

Ninachokiona hapa wengi wameacha hoja ya msingi
na badala yake wanamuattack Dr. Kitila, nadhani kwa
chuki au vinginevyo. Ingalau wewe umesema jambo la
msingi sana...
 
Dr Kitila,
Nakuona humu. Fafanua. Thabo Mbeki hana mtoto wake wa kuzaa.
 
From the very outset mbeki aliweka wazi that was a very pinchin question as kitila alitaka kupotray mbele ya dunia kwamba msimamo wa mbeki kua ukimwi kuenezwa kwake ni umasikini umesababisha vifo vingi sana as yeye(mbeki akiwa rais) alipuuzia scientific investigation about kuenezwa kwa ukimwi hatimae watu wakaendelea kufa. (Kitila alitaja data,sizikumbuki).

Mbeki kwa hasira(alichange fascial expresion) alimwambia kitila "the information that you have is wrong" from statement itself na takwimu alizotoa. Mbeki alielezea vizuri sana kauli yake ya umasikini na tafiti za kisayansi kuhusu ukimwi...ila hakujibu alichouliza Dr mkumbo kwa sababu it seems hakuona kama kuna swali rather aliliona lipo kisiasa ama pengine kifitna.

My take...Kuuliza sio ujinga, na kukosea sio tusi. Sikufahamu dhamira ya kitila ila iwe ilikua ni nzuri ama mbaya watu wengi pale nkuruma walinyong'onyea..kwa lugha ya magazeti ya tanzania ungedema "kitila achafua hali ya hewa Nkuruma"
 
Aliyeulizwa swali ameshindwa kujibu, haya unayotoa ni mawazo yako binafsi.
Mnataka watu waulizwe maswali rahisi ili kuwafuarisha ama?


Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Mkuu sixgates jee Kitila aliuliza kuhusu mtoto wa Mbeki kufa kwa UKIMWI?

Au muanzisha mada Kiingereza kimempiga chenga hapa anatulisha kasa?
 
Last edited by a moderator:

HUYU KITILA NKUMBO hana akili utaulizaje swali kama hilo ambalo linalenga familia ya unayemuuliza utafikiri ni mwandishi wa magazeti ya udaku aka tabloids. jukwaa lile lilikua la kuelimishana na maswali yangekua direct yanatoa ukweli bila ya kugusa mambo sensitive ya kifamilia.
 
Maswali yaliruhusiwa kwa yeyote aliyekuwa ukumbini, Dr kitila alikua na haki ya kuuliza.

Mbona kama umepata jazba kupita kiasi??


Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 

Kwani uyo Mbeki alivyosema kuhusu ukimwi unasababishwa na umaskini unajua alizigusa familia ngapi ambazo zina wanandugu waliofariki kwa ukimwi au wanaougua gonjwa hili??
Uwanja ulikuwa wazi kwa swali lolote linayoigusa jamii.
Dr. Kitila aliuliza swali zuri sana.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Ninachokiona hapa wengi wameacha hoja ya msingi
na badala yake wanamuattack Dr. Kitila, nadhani kwa
chuki au vinginevyo. Ingalau wewe umesema jambo la
msingi sana...

Nadhani hakuna attack yeyote kwa Dr Kitila, watu wanaitaji tu kufahamu kama yupo humu ni vizuri atuweke sawa kuhusu swali lake.
 

Sijaona umuhimu wa kuingiza neno CHADEMA kwenye mjadala huu na kuita watu vilaza.
Tujadili tu hili swali zuri la Dr. Kitila ambalo Mbeki amekua mzito kulijibu.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 

Ndio, kasa ama turtle kwa Kiingereza.




*Tanabahi
Kwa Kiswahili cha pwani kulishwa kasa maana yake ni kulishwa taarifa zisizokuwa na uhakika wa ukweli wake kama kulishwa kasa ambae kwa mujibu wa sheria za Kiislam uhalali na uharamu wake una utata
 
Ndo maana ya kuwa na Google.

Sio Google tu, hata Mamma na Ameoba bado hazitoi taarifa zozote kuhusiana na mtoto wa Mbeki aliyekufa kwa UKIMWI. Hayupo kwenye kumbukumbu zozote za mtandao wa intaneti.

Kama wewe unamjua jina lake tuwekee utusute
 
Tatizo letu tunafikiri UKIMWI ni ugonjwa wa MASKINI peke yao.Je inamaana hakuna matajiri wanye maabukizi ya Virusi (HIV/AIDS) Je hakuna wabunge na mawaziri walioathirika na ugonjwa huu.Je ni sisi walala hoi tu?Kwa maoni yangu Dr.Kitila aliuliza swali zuri sana ili tunapofanya jambo tuangalie na matokeo yake.
Na pili Thabo Mbeki alipaswa kuomba radhi kwa ile sentensi yake kuwa umaskini wa mtu ndio unaomletea au utakaomletea UKIMWI.Ukiangalia kwa mapana wenye pesa ndiyo waathirika zaidi kuliko hao maskini sababu ya kutumia vibaya hizo pesa zetu tulizonazo.
 

Wewe ni mmoja kati ya watu mnaotaka kumjibia Mbeki swali aliloshindwa kujibu.
Swala la ukimwi linagusa familia ya kila mmoja wetu hapa duniani,
sasa nyie kama mnamuona Mbeki ni mungu na hapiswi kuulizwa maswala ambayo yeye mwenyewe ndo kaanzisha mjadala wake mtakua mnapotoka sana.
Dr. Kitila aliuliza swali zuri sana.
Watanzania acheni uoga, nyie ni mfano wa wananchi wanaoshindwa kuwauliza viongozi wao maswali ya msingi kwa kuogopa kofia za uongozi wao.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…