Dr. Kigwangala Huru!, Sasa Yuko Live On Clouds Radio!

Dr. Kigwangala Huru!, Sasa Yuko Live On Clouds Radio!

Pascal Mayalla

Platinum Member
Joined
Sep 22, 2008
Posts
57,212
Reaction score
128,964
Wanabody,

Mbunge wa Nzega, Dr. Hamisi Andrea Kigwangala, ambaye jana alitiwa nguvuni na polisi wa Nzega, kwa kuendesha maandamano bila kibali, aliachiwa jana usiku wa manane, na saa hizi, ametinga bungeni Dodoma na yuko live on Clouds Radio,

Amesema hakukuwa na maandamano yoyote, wala hapakuwa na fujo yoyote, bali baada ya kufanya mkutano wa hadhara kuwasikiliza wananchi wake wakilalamikia kutimuliwa eneo la wachimbaji wadogo wadogo, walishtukia polisi wakija na kuanza kuwavurumishia mabomu ya machozi.

Amesema hilo eneo ni la wananchi kihalali, mgodi ni wageni tuu waliokaribishwa na hawana uwezo wa kuichimba dhahabu yote wao wenyewe, hivyo anasimama na wananchi wa Geita katika kudai haki yao ya kuvuna rasilimali yao kihalali!.
Amesema anashangazwa na polisi kuwanyanya wananchi wenye mali for the expense ya wageni, wanaovuna dhahabu yao na kuwapatia malipo kiduchu!.

Listen Live!.

Paskali
 
Wanabody,

Mbunge wa Nzega, Dr. Hamisi Andrea Kigwangala, ambaye jana alitiwa nguvuni na polisi wa Nzega, kwa kuendesha maandamano bila kibali, aliachiwa jana usiku wa manane, na saa hizi, ametinga bungeni Dodoma na yuko live on Clouds Radio,

Listen Live!.

Pasco

Siku hizi umeamua kuwa msemaji wake sio
 
Huyu Kigwangala kuanzia jana nimemtoa maanani kabisa, Nilidhani ana akili kwa ajili ameenda shule, Kumbe naye anaiga ule ujinga wa LEMA wa kuvunja amani ya nchi.
 
Ngoja naye tumsikilize unaweza kuta policccm wamemwonea maana nao hawaamini hata kidogo
 
Mhe. Kingwangala Pole!
Lakini nyie wabunge wa ccm si tuliwaambie acheni kuendekeza polisi mkawa mnachekelea wanavyoua na kutesa wapinzani sasa umeona joto ya jiwe? Na pia Mhe. Masele aiipata hivi karibuni huko jimboni kwake shinyanga. Hata hivyo naona kama kamchezo ka kuigiza ili polisi wapate nafuu ya kuwashughulikia wapinzani vile, kwa maana ndoa ya ccm na polisi ni ya muda mrefu sana.
 
nimekuwa nikisema amepanga tukio zima mweh.u huyu,hakuna gamba linaloweza kusimamia maslahi ya taifa,toeni maigizo hapa...hutokaa usikie polisi wakimfungulia kesi....
 
Binafsi wanaccm wote nawaona kama wasanii fulani hivi nikianza na Kikwete mwenyewe.!
 
Mhe. Kingwangala Pole!
Lakini nyie wabunge wa ccm si tuliwaambie acheni kuendekeza polisi mkawa mnachekelea wanavyoua na kutesa wapinzani sasa umeona joto ya jiwe? Na pia Mhe. Masele aiipata hivi karibuni huko jimboni kwake shinyanga. Hata hivyo naona kama kamchezo ka kuigiza ili polisi wapate nafuu ya kuwashughulikia wapinzani vile, kwa maana ndoa ya ccm na polisi ni ya muda mrefu sana.
mkuu usiibiwe kirahisi na haya maigizo,wanatafuta justification ya kuendelea kuwakamata wapinzani...polisi na ccm lao moja.
 
Amesema hilo eneo ni la wananchi kihalali, mgodi ni wageni tuu waliokaribishwa na hawana uwezo wa kuichimba dhahabu yote wao wenyewe, hivyo anasimama na wananchi wa Geita katika kudai haki yao ya kuvuna rasilimali yao kihalali!.

Amesema anashangazwa na polisi kuwanyanya wananchi wenye mali for the expense ya wageni, wanaovuna dhahabu yao na kuwapatia malipo kiduchu!.

Ameishamaliza kuhojiwa!.
Pasco.
 
Huyu Kigwangala kuanzia jana nimemtoa maanani kabisa, Nilidhani ana akili kwa ajili ameenda shule, Kumbe naye anaiga ule ujinga wa LEMA wa kuvunja amani ya nchi.

Watu wenye njaa wana Amani? ama umejitoa ufahamu.!!!! mimi sikuzote napuuza comment zako maana sio analytical, you can come here and post just a single sentense stinking
 
Inaelekea hawa polisi hawakujua kuwa Dr.Kings ni mbunge wa CCM? au waliamua kufanya mazoezi ya wazi.
 

Attachments

  • attachment-17.jpeg
    attachment-17.jpeg
    8.9 KB · Views: 1,562
image.jpg Huyu kijana ambaye amelala kwenye tuta ndio Kafa na Kigwangala unalizungumziaje hilo? Pili , huyo polisi mwenye t.shirt Nyekundu anamwelekezea huyo kijana mwenye orange SMG kiunoni nini kilienda lea hapo baadae ?
 
Back
Top Bottom