Yule ni Taperi tu,, mi wife Kala Sana DAWA zake bila mafanikio,,, ,, ALIENDA KUPONEA KWA KAIRUKI HOSPITAL,,,tena huyo MWAKA DAWA zake ni gharama kubwa mno na hazisaidii
Acha ujinga wewe, umeona cheti chake alichosomea? Wee umeambiwa huyu traditional healer, yeye kajigeuza dokta wa modern medicine bado unabwek bweka hapa kasomea kasomea.
Tatizo letu waafrika ni kuona kila kilichopangwa na mzungu ndio basi hata kama hakionyeshi faida kwetu.
Wagunduzi siku zote ni watu wa kawaida .
Kazi ya wasomi ni kutafiti huo ugunduzi na kujenga hoja za kuboresha au kuja na formula rahisi zaidi.
Eti tatizo ni kujiita dr.
Hata angejiita Mungu sina shida naye kama anayoyafanya yanalingana na anavyojiita.
Tunao madaktari wengi wasio na wito na waendekeza ufisada na kuiba madawa na vifaa vya serikali ili wafungue maduka binafsi ya dawa.
Hawa ndio hatari kuliko Dr. Mwaka.
Nadhani tumpime Dr. Mwaka kwa uelewa wake juu ya tiba anayotoa ya magonjwa ya uzazi.
Je,ni wapi anatoa maelezo yasiyo sahihi?
Je,hasomea kile anachokifanya na kutoa Elimu.
Tatizo watanzania hasa vijana waliozaliwa mjini hawajui kuwa kuna tiba mbadala za uhakika ambazo zimetumika kwa karne nyingi . Kuitwa sijui dokta sjui ushuzi gani hayo ni madaraja tu ya viwango vya elimu vilivyowekwa na wazungu.
Mwaka naye kwa kiwango cha tiba mbadala ni dokta. Watu ndio wanaomwita hivyo na amejubali wito wa wateja wake. Hakuna dhambi hapo.
Watu watampuuza pale tu wale tuliowaweka kwenye majengo ya umma na kuwapa madawa na vifaa kwa pesa za umma watakapoweza kuwapenda na kuwahudumia wagonjwa kwa ukarimu na kujali. Kwa sasa hata Manyaunyau atajiita dokta kutokana na wale tuliowaamini kugeuza hospitali za umma kuwa vijiwe vyao vya wizi na rushwa.
Na ukiona mtu ameenda kule kwa kina Mwaka ujue amesumbuka sana kwa hizo hospitali za wazungu na akakosa tiba.