Dr. Francis Michael, Dr. Tulia Ackson: Mmeonesha picha gani? Mmechafuka

Dr. Francis Michael, Dr. Tulia Ackson: Mmeonesha picha gani? Mmechafuka

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,006
Nyinyi wote ni wasomi wa ngazi ya Shahada ya Uzamivu. Nyinyi wote ni Wahadhiri wa UDSM. Nyinyi wote mmeanza kusikika na kuonekana wakati wa Bunge la Katiba. Nyinyi wote mlikuwa Wajumbe wa Bunge hilo. Wote mkawa na nyadhifa kwenye Bunge la Katiba.

Nyinyi wote mliteuliwa na aliyekuwa Waziri wa Uchukuzi,Samwel Sitta kuwa Wajumbe wa Bodi ya Mamlaka ya Bandari Tanzania. Kutokana na imani kubwa kwenu na weledi wa kusaidia taifa katika nyanja zenu,mliteuliwa. Bodi ya Shirika au Kampuni ndiyo serikali ya mahali husika.

Bodi huamua,hung'amua,huchuja,huchunguza,huanzisha na hata kusitisha masuala mbalimbali kuhusu shirika au kampuni husika. Ndiyo watawala wenyewe. Mambo yote ya kimaamuzi,mema au mabaya,hufanywa na bodi. Pale Bandarini,watawala wa juu na pekee ni Bodi ya Mamlaka ya Bandari.

Mlikuwa Wajumbe wa Bodi iliyovunjwa hivi karibuni. Dr.Michael,kama mtaalamu wa biashara,ulikuwa wapi kuepusha makandokando ya kibiashara Bandarini? Dr. Tulia,kama mtaalamu wa sheria,ulikuwa wapi kudhibiti makandokando ya kisheria Bandarini kama Mjumbe wa Bodi?

Nyinyi mmechafuka. Mmetoa taswira mbaya kwa wasomi wanaopaswa kuaminiwa na kutumiwa. Mnapaswa kuwajibishwa katika kulinda chama,wasomi na hata uaminifu kwa watu weledi kama nyinyi. Mmechafuka!

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
 
Ahhahhaa, we mzee wa lumumba, si muanze kumwajibisha huyu naibu spika? ndani ya chama chenu.
 
Ni aibu kwa Taifa na Wasomi waliowaamini.. Dhaifu kuliko wote ni yule aliyewateua
 
Uko sahihi kabisa lakini kwa kuwa hawa ni wasomi wachumia tumbo watajifanya hamnazo!
Hili la dr Tulia ni wake up call kwa Rais achukue tahadhari sana katika teuzi zake mbali mbali! Nji hii imeoza, kwa jinsi alivyofast track uteuzi wa Tulia hadi kufikia unaibu spika inambidi JPM azinduke!
 
wanatakiwa wakaozee segerea ....majambazi hawa....
 
Wamesoma ila hawajaelimika, elimu-mivyeti waliyoipata imeshindwa kuwasaidia. Nawapa pole.
 
dkt tulia amewekwa pale na watu fulani kwa mkakati maalum
 
Mzee Tupatupa umemsahau Prof. Msambichaka aliyekuwa Mwenyekiti wa Bodi. Huyu ni msomi aliyebobea kwenye masual ya uchumi sijui alitumia vipi taaluma yake kuisaidia nchi.
 
Sisi tulijua chama chao sasa mafisi basi kumbe bado!.... Ndo maana ni bora baraza likachelewa kidogo ili kila idara imulikwe na isafishwe- pasiwepo na kasoro kama hizi, Mbobezi ataleta maelezo yake mareeeeeeefu kwa swali dogo-
 
Mzee Tupatupa umemsahau Prof. Msambichaka aliyekuwa Mwenyekiti wa Bodi. Huyu ni msomi aliyebobea kwenye masual ya uchumi sijui alitumia vipi taaluma yake kuisaidia nchi.

Hakika. Lakini,nimelenga hawa 'hazina' za taifa.

Mzee Tupatupa
 
Uko sahihi kabisa lakini kwa kuwa hawa ni wasomi wachumia tumbo watajifanya hamnazo!
Hili la dr Tulia ni wake up call kwa Rais achukue tahadhari sana katika teuzi zake mbali mbali! Nji hii imeoza, kwa jinsi alivyofast track uteuzi wa Tulia hadi kufikia unaibu spika inambidi JPM azinduke!

Tena aliukosa Uspika kamili kidogo sana.
Otherwise ndiyo angekuwa spika leo yule dada.
Nchi hii akiendelea kufukua bila shaka hata yeye mtumbua majipu ataishia kujitumbua, vinginevyo nauona mwisho wa aibu katika hizi sarakasi.
 
Huyo Tulia ajiuzuru nafasi yake ya unaibu spika maana ni aibu
 
Waftiwe uwanachama ili kunusuru chama pendwa Na chama dola.au waondolewe nyazifa zao kupisha uchunguzi kwakuwa hizo ndiyo procedure Za civil servant wa nchi ye2 au Hao wako above ze law procedure Za kupisha uchunguzi haziwahusu?

Mbona Daniel Yona.Basil Mramba.A.Massawe.R.Bade Na wengine wengi wamerespond Na walikuwa Na nyazifa kubwa? Au huyu mwingine anasubiria wabunge wamuwajibishe? Mmmh wahadhiri wa UDSM Kweli ni wabobezi...!
 
Nafikili hzo PhD Holder zinazo zalishwa kwa style hii tuombe sana mwenyezi mungu atunusuru kila mtu mpigaji jaman tutafika wap
 
Back
Top Bottom