Dr Benson Banna: Mimi ni muumini wa serikali moja

Dr Benson Banna: Mimi ni muumini wa serikali moja

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
52,640
Reaction score
164,788
Dr. Bana yuko live Channel 10 muda huu na katika mazungumzo yake na mtangazaji, anasema yeye ni muumini wa serikali moja na kwamba haamini mfumo uliopo wa serikali mbili utamaliza kero za muungano.

Katika mazungumzo yake anasema,haamini kama Wazanzibari wengi wanaunga mkono serikali tatu na amesisitiza tusubiri kuona kwenye kura za maoni.

Msikilize live sasa hivi kupitia Channel hiyo...

Wana jamvi Dr. Bana kasema ni sahii kufukuzwa Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar. Ameyasema hayo leo katika kipindi cha barugumu channel 10 kua ni sahihi kwa kufukuzwa mwanasheria mkuu wa Zanzibar kwakua ametenda kosa la kiuongozi kwakua yupo chini ya mamlaka ya rais
 
sasa kama ni mumini wa serikali moja kwa nn aseme hii rasimu ya ccm ni bora?
 
Dr.Bana yuko live Channel 10 muda huu na katika mazungumzo yake na mtangazaji, anasema yeye ni muumini wa serikali moja na kwamba haamini mfumo uliopo wa serikali mbili utamaliza kero za muungano.

Msikilize live sasa hivi kupitia Channel hiyo
Huyu bwana BANA sijui katoka wapi hapa TZ anatumia nafasi yake kutuchanganya,majuzi tu amehojiwa akaisifu sana katiba pendekezwa ya ccm......uwa huyu bwana anakwenda na upepo!anatafuta cheo huko ccm.
 
Tuzungumze vitu vinavyoeleweka kwa akili ya kawaida kuwa na SERIKALI MOJA sidhani kama inawezekana. maana ukishakuwa na SERIKALI MOJA hapo umeshaifuta ZANZIBAR na sidhani kama WAZANZIBAR watakubali nchi yao IPOTEE.
TUONGELEE MAMBO YANAYOWEZEKANA.
 
Huyu mzee kila siku yupo kwenye Tv, anafundisha saa ngapi? UDSM ndio chanzo cha umaskini wa hii nchi. Heri Sasa vyuo vimeanza kuwa vingi huenda Tanzania ikaanza kuwa na maendeleo maana hawa wasomi wa UDSM na walimu wao Ni majanga ya kidunia.
 
Na ma CCM wanamtumia sana.Hivi huyu anajua kuliko Jaji Nyalali,Jaji Kiasga,Jaji Warioba,Dk SalimAhmed Salim.Mbona hawampi hata U Nape? Wanamtumia kama kondomu wakimaliza shida zao wanamtupa chooni.Yuko wapi Masumbuko Lamwai,na lile VUVUZELA la TEMEMEKE Richard hata u tendaji wa kata hawana.
 
Haamini katika mazingira yaliopo kungepatikana maridhiano.Anasema maridhiano yangekuwa na serikali mbili na nusu
 
Wana jamvi ameyasema hayo leo katika kipndi cha barugumu chanel kua ni sahihi kwakufukuzwa mwanasheria mkuu wa zanzibar kwakua ametenda kosa la kiuongozi kwakuayupo chini ya mamlaka ya rais
 
Wana jamvi ameyasema hayo leo katika kipndi cha barugumu chanel kua ni sahihi kwakufukuzwa mwanasheria mkuu wa zanzibar kwakua ametenda kosa la kiuongozi kwakuayupo chini ya mamlaka ya rais

Achana na huyo TZ tatizo la kwanza ni hao wanaojiita wasomi HAWAJIAMINI PIA USOMI WAO HAUJAWAWEKA HURU bado ni mateka wa watawala, watanzania wakawaida ndio watakao ikomboa hii nchi awa wengine sijui wasomi ni wachumia tumbo.
 
lazima niwe mkweli. huyu prif. huwa simwelewi kabisa nashindwa kuelewa uprof. wake wote hivi hasomi hata alama za nyakati kuwa watu siku hizi wanaelewa vitu kuliko enzi za mzee wetu.? je ingepigwa kura ya siri wangejuaje kapiga hapana?
 
nashangaa sana wanachuo wa UDzm kuendelea kufundishwa na huyu jamaa coz anaongeaga pumba tu na sio kama msomi ila mtetea kitumbua
 
Huyu Bana bado haoni aibu? Anadhalilisha uprofesa wake kwa kushindwa kuchambua mambo. Serikali ya mapinduzi haikuwa na msimamo wa pamoja kuhusu katiba inayotakiwa ukizingatia serikali ile ni ya umoja wa kitaifa. kila mtu alienda na msimamo wa chama chake. Wajumbe wa CCM Zanzibar, walenda na msimamo wao wa serikali mbili; wajumbe wa CUF walienda na msimamo wao wa serikali tatu. Mwanasheria mkuu siyo mwanachama wa chama chochote cha siasa kwa mujibu wa katiba. Huyu alienda Dodoma na msimamo wake wa kulinda katiba ya Zanzibar. Huyu anayejiita profesa anashindwa kuyajua haya kweli?
 
"Dr" Bana bhanaaaa!!!!! Na kujikomba kote huko, mbona hao jamaa hawakupi ujiko??? Au wanakufundisha ukweli wa ile methali,"Kuchamba kwingi........."??????
 
ufike wakati kuwekwe namna ya kukagua upya u-Dr wa mtu na ikiwezekana anyang'anywe...maana huu ni uzalilishaji kwa taaluma na level yake ya elimu
 
Aiseee. 2015....kweli inakaribiaaa.....mi acha nijifunze siasa jf.....
 
Dr Bana Ni Mmoja Wa Wasomi Ambao Nimewaweka Kwenye IGNORE LIST YANGU YA WASOMI WA TANZANIA.
 
Lazima tuheshimu maoni yake ila atujibu maswali yetu pia iko wapi hadhi ya Zanzibar na kama hadhi ya Zanzibar ipo na ya Tanganyika mabae ni mwenza katika muungano iko wapi hadhi yake maana ya muungano lazima uonekane na uende kwa vigezo na masharti!!!!!!!!
 
Back
Top Bottom