Dr. Azaveli Lwaitama: Hakuna Tanganyika!

Azaveli Lwaitama ni bora angeamua kukataa kuhojiwa kuliko kutamka vitu ambavyo mdomo wake unalitamka lakini moyo wake hauliamini. Muda si mrefu atapoteza heshima aliyojijengea kwenye jamii ya wasomi.

Rais mwenyewe juzi juzi akizungumza na wazee wa DSM alitamka wazi wazi bila kuuma maneno kwamba tunasherehekea miaka 50 ya Tanganyika.

Halafu BBC siwaelewi. Lwaitama amespecialize kwenye linguistics, wao wanamtumia kama mchambuzi wa mambo ya kisiasa. BBC nao ni wababaishaji ..
 
natumai itarudi tu Tanganyika baada ya muda si mrefu. wazanzibari wanatucheka kweli na kutona mabwege kwa kutokuwa na nchi katika muungano. wao anaweza akachomoza mtu akawa rais Tanzania kutoka kwao, yaani anaitawala mpaka Tanganyika iliyokuwa huru mwaka 1961, yaani tulipata Uhuru halafu 1964 tukauza nchi hadi kina Mwinyi nao wakaja wakatutawala. Yaani sisi bado ni koloni, tena sa ivi ni koloni la wazanzibari, yaani wao hadi mawaziri tunashare wakati kule kwao hamna kitu kama icho. tunaanza kuamka sasa, either serikali tatu ama moja, zanzibari ife kama tanganyika ilivyokufa. watachanganyaje udongo wa nchi mbili, halafu zanzibar iendelee kuwepo?
 
  • Thanks
Reactions: ram
Labda mkuu si unakumbuka kulikuwa na nchi inaitwa Congo? lakini wakaja wahuni kama hawa wa hapa kwetu wakaipachika jina la Zaire! je Zaire bado ipo au wananchi wamerudisha jina lao la Congo?
Tusiwe wavivu wa kukumbuka, maana ukitaka kumtawala mtu milele mnyime Historia yake. its matter of time but Tanganyika will rise again.
Hapo kwenye rangi... umenena vema.. will raise again
 
Tanganyika inapaswa kuwepo, haya mambo yanachanganya sana. Tanganyika ilipata uhuru wake mwaka 1961, so hapa tunasherehekea uhuru wa Tanganyika baada ya uhuru Tanganyika iliishi kwa miaka miwili na miezi kadhaa ikaja ikaungana na Zanzibar, ikazaliwa Tanzania, swali langu Tanganyika ilifia wapi, kwasababu hadi leo Zanzibar ipo tena ikiwa na serikali yake kamili, wimbo wa taifa, bendera, rais n.k vya Tanganyika vyenyewe vilifia wapi?

Tanganyika hakuna, imewekwa kwenye kichupa na kuwa delisted!!!
 
Kama alizaliwa mtoto TANZANIA kwanini Zanzibar ipo hadi leo na wakati waliungana?

Kwani marekani insherkea uhuru wake kwakuanzia lini??maana baada ya uhuru wake kuliunganika nchi nyingi tu nazilizokuwa huru na sasa zilifuta uhuru wao nakuunganisha uhuru wanchi waliyo ungana nayo!!sasa iweje tukumbuke Tanganyika wakati tulisha sema basi na sasa tunamzaa mtoto tanzania!
 
Mwanzo hakukuwa na tanganyika wala tanzania,tanganyika imekuja na wajermani around 1919. Hadi kufikia mwaka 1964 ni miaka 45,tanzania imezaliwa mwaka 1964 na kesho tar 9 dec 2011 itatimiza miaka 47 jeee miaka hamsini 50 tunayoadhimisha ni ya nini
 
huyu mtu huwa namkubali sana. kila mara huwa anakuja na kitu na wazo jipya kabisa, tofauti na 'wasomi' wengine type ya Dr Banna ambao kimsingi huwa wanaongea mambo mepesi sana yanayojulikana karibu na raia yeyote masikini wa nchi hii
 
Sasa hapa nimechanganyikiwa, hivi tunasherehekea nini sasa? Mbona mimi, sijui nilitaka niseme nini, nikumbusheni!
 
Mwanzo hakukuwa na tanganyika wala tanzania,tanganyika imekuja na wajermani around 1919. Hadi kufikia mwaka 1964 ni miaka 45,tanzania imezaliwa mwaka 1964 na kesho tar 9 dec 2011 itatimiza miaka 47 jeee miaka hamsini 50 tunayoadhimisha ni ya nini
Na wewe ni sehemu ya wapotoshaji, mwanzo nchi yetu ilikuwa inaitwa German East Africa, na baada ya Waingereza kuichukuwa na kuwa koloni lao ndio wakabadili jina na kuiita Tanganyika.
 
Wazanzibar huwa wana siku yao yakukumbuka mapinduzi na hiyo huitwa siku ya mapinduzi ya zanzibar na wala sio Tanzania.Sasa ni kwaniniupande wa pili isiwe hivyo hivyo?
 
Back
Top Bottom