Dr. Azaveli Lwaitama: Hakuna Tanganyika!

Dr. Azaveli Lwaitama: Hakuna Tanganyika!

Ni ukweli usiopingika kwamba tunasherehekea uhuru wa Tanganyika ambayo ilipata uhuru 9/12/1961, a.k.a Tanzania Bara baada ya kuungana na Zanzibar 1964. Tanzania haikuwepo miaka 50 iliyopita, iliyokuwepo ni Tanganyika. Kama tungependa kuienzi Tanzania inavyostahiki, basi tungelenga kufanya sherehe kubwa wakati wa miaka 50 ya Muungano.


Kwani marekani insherkea uhuru wake kwakuanzia lini??maana baada ya uhuru wake kuliunganika nchi nyingi tu nazilizokuwa huru na sasa zilifuta uhuru wao nakuunganisha uhuru wanchi waliyo ungana nayo!!sasa iweje tukumbuke Tanganyika wakati tulisha sema basi na sasa tunamzaa mtoto tanzania!
 
Labda KakaKiiza tu ningependa kukufahamisha kwamba mimi nina mawazo huru na ninadadisi, sijamkabidhi Dr Lwetama kufikiri kwa niaba yangu, Kama wewe unadhani au unafikiri kwamba analowaza Dr Lwetama ndio sahihi basi hata chama cha siasa atakachojiunga au kushabikia unapaswa umfuate, maana wewe tayari ni mateka wake.
Nawasiwasi na uhuru wa mawazo yako kwa jinsi unavyo uamini huo uhuru wakati unakupoteza mimi ninakubali kwa Dr Ezavel lwaitama nimetekwa!!ila wewe unahitaji kukombolewa katika lindi la mawazo duni.........nenda pale UDSM Nkhuruma hall kwenye mdahalo au kama ulipata bahati ya kusoma pale basi huwezi kubishia kitu!! au ni ninyi wale mnasema punda ukimpaka rangi anageuka punda milia!!!Fata mawazo ya wana JF wenziyo watakutoa hapo ulipo kwenye ukimbizi wakufiria!
 
:smash::A S 465:Wanaosema hakuna Tanganyika acheni upuuzi katika vitu ambavyo huwezi pigana navyo ni historia Tanganyika ipo kama ilivyo Zanzibar na Tanzania ni muungano wa Tanganyika na Zanzibar hutaki unaacha msitupotezee muda kujadili vitu ambavyo ni ovious!
 
Ni ngumu sana kulazimisha nchi iitwayo Tanganyika. Muda ushatutupa mkono.
 
Kwani marekani insherkea uhuru wake kwakuanzia lini??maana baada ya uhuru wake kuliunganika nchi nyingi tu nazilizokuwa huru na sasa zilifuta uhuru wao nakuunganisha uhuru wanchi waliyo ungana nayo!!sasa iweje tukumbuke Tanganyika wakati tulisha sema basi na sasa tunamzaa mtoto tanzania!

KK, mfano wa Marekani ni tofauti kabisa na muungano huu wetu. Marekani hizo states ziliungana na kuunda nchi moja. States ziliuua 'u-nchi' wake na kuuzamisha kwenye taifa kubwa moja. Ebu waambie wazanzibari kwamba waliuua u-nchi wao uone kama watakukubalia.
Tunapozungumza hivi si lazima iwe kwamba tunataka kuifufua Tanganyika, tunaonyesha utata uliopo kwenye mfumo wetu wa muungano.
 
DR azaveli lwaitama ana falsafa ya kuchukiza umma na mkomunisti wa kukubuhu. Makala zake zote hazijengi umma bali kuchukiza umma . Hivi ndivyo walivyo wakomunisti wa kukubuhu. Tanganyika ilikuwepo na imefutwa kwa ujanja ujanja tuu wakupotosha umma. Uhuru tusherekaao ni wa Tanganyika na sio tanzania, nashangaa azaveli halioni hilo ile yeye ni kutaka kuchukiza umma tuu.

Nyerere aliyeleta muungano wa kimwamba kafariki na sisi ni watu wazima hatuwezi kuishi kwa kero ambazo tunaweza kuziondoa. Wako watu kama akina azaveli, wao ni kulinda fikira sahihi za nyerere tuu na hata kama fikira hizo zina maumivu ya kugongwa na jiwe ugokoni. Jamani tusipobadili katiba na kuunda katiba yetu wenyewe na kutoa kero za muungano basi tutayarishe majeneza 2015 uchaguzi mkuu.

Joseph mihangwa nakushukuru sana kwa makala zako zimenitoa ujinga na kuniweka pazuri. Hongera sana kwa kuelimisha umma kwa mapana ya muungano kama ulivyoandika. Hii itasaidia sana kurudisha jina la tanganyika mitaani.
 
Nawasiwasi na uhuru wa mawazo yako kwa jinsi unavyo uamini huo uhuru wakati unakupoteza mimi ninakubali kwa Dr Ezavel lwaitama nimetekwa!!ila wewe unahitaji kukombolewa katika lindi la mawazo duni.........nenda pale UDSM Nkhuruma hall kwenye mdahalo au kama ulipata bahati ya kusoma pale basi huwezi kubishia kitu!! au ni ninyi wale mnasema punda ukimpaka rangi anageuka punda milia!!!Fata mawazo ya wana JF wenziyo watakutoa hapo ulipo kwenye ukimbizi wakufiria!
Usinilazimishe unaloamini wewe basi na mimi ndio niamini hivyo, nchi yetu sio ya kwanza kuungana, kinacholeta tabu ni style ya muungano wetu wa kuchanganya mchanga kama waganga wa kienyeji badala ya kuunganisha watu, kama hili swala lisingekuwa na walakini ni kwa nini watu wahoji miaka 50 baadaye? open ur eyes & open ur mind, hao unaowaona wewe kwamba ni wasomi si watu wa kuaminika kwa kila jambo.

Tunaye Dr Bana, tunaye Profesa Mkandara, je wajuwa kazi ya wasomi hawa ni nini? hakuna mtu mwenye akili timamu anaeweza kuwasikiliza watu hawa eti kwa kigenzo cha usomi. hawa Traitors.
 
wewe ndiye utakuwa na mapungufu ya akili kama unadhani kuna Taifa linaloitwa Tanganyika...Hawa magamba wanajustfy means ya kutafuna fedha za wananchi kwani baada ya miaka miwili kama sio mitatu watasherehekea uhuru wa miaka 50 ya Tanzania...wewe na Professor mkandara akili zenu zimefanana
 
Nchi iliyopata uhuru mwaka 1961 ni Tanganyika, mwaka 1964 wakati Tanganyika inaungana na Zanzibar, nchi ya Tanganyika ikabadili jina na kuwa Tanzania Bara(hapa sioni mantiki ya kubadili jina toka Tanganyika kuwa Tanzania Bara baada ya kuungana, jina lingeweza kubaki lilelile Tanganyika), kwa hiyo jina la Tanzania Bara halijafikisha miaka 50 bali ni miaka 47.

Tunaweza kusema Tanganyika haipo kwa maana ya jina lakini kwa maana ya nchi(ardhi) bado ipo na kipande hicho cha ardhi(nchi) ndio kinaitwa Tanzania Bara kwa sasa.

swali la kujiuliza ni je kulikuwa na umuhimu gani wa kubadili jina kutoka Tanganyika na kuwa Tanzania Bara wakati tunaungana na zanzibar ili kupata Tanzania? kwani bila kubadili jina la Tanganyika,je Tanzania ingeshindikana kuwepo? Hapa kuna walakini.

Kwa nini wabadili jina la nchi ambayo ilikuwa inakufa-yaani ilikuwa haiendi kuwa sovereign state tena?

Kama Dr. Lwaitama anasema tunasheherekea uhuru wa Tanzania Bara, je TZ bara ina hadhi ileile ya Tanganyika ya 1961 to 1964 ilipokuwa ni sovereign state? au ni nchi jina isiyokuwa sovereign? duu kichwa kinauma!
 
Wakuu nashindwa kumuelewa huyu Dr Lwetama nae amejiunga na kundi la wapotoshaji kwamba eti tunasherehekea Uhuru wa Tanzania bara na kwamba wanaosisitiza ni Tanganyika wana ajenda za kisiasa, je ni huyu Dr Lwetama ninayemfahamu mimi amekua mpuuzi kwa viwango hivi?

Source: BBC Swahili sasa hivi iko live.

Lwaitama nahisi ni mganda.......Tanganyika ipo na mimi ni Mtanganyika
 
Dr. Lwaitama nami nilimsikia jana akihojiwa na BBC. Hata hivyo, kama msomi naona hakufikiri sana anaposema tunasherehekea uhuru wa Tanzania. Tunaposherehekea uhuru wa Tanzania, je Mkoloni wake ni nani aliyetupa huo uhuru? Kwa mawazo yangu naamini tunasherehekea uhuru wa Tanganyika kwasababu Mwingereza ndiye aliyetoa uhuru kwa Tanganyika!
 
TANGANYIKA (1961)=TANZANIA BARA (1964) ??????:A S embarassed:

TANZANIA BARA+ZANZIBAR=TANZANIA
???????????:A S embarassed:
 
Kwa hilo si jina kama CRDB ya zamani na CRDB yaleo je maana ni ileile??funguka Azavel Lwaitama hawezi kuwa mpuuzi kwawatu wenye uwezo kiakili ni mmoja wapo!!wewe ndo unawezakuwa mpuuzi watu wanaomjua Azavel lwaitama na hii thread yako haiitaji kuwa jiniasi!!!dairekiti wewe ndiye mpuuzi!!!

Wapendwa acha matusi jenga hoja. nyote mnatukana tu hakuna aliyejenga hoja. Ndilo tatizo la watu. Do not present ad hominen arguments!!!
 
Azaveli Lwaitama ni bora angeamua kukataa kuhojiwa kuliko kutamka vitu ambavyo mdomo wake unalitamka lakini moyo wake hauliamini. Muda si mrefu atapoteza heshima aliyojijengea kwenye jamii ya wasomi.
 
Wakuu nashindwa kumuelewa huyu Dr Lwetama nae amejiunga na kundi la wapotoshaji kwamba eti tunasherehekea Uhuru wa Tanzania bara na kwamba wanaosisitiza ni Tanganyika wana ajenda za kisiasa, je ni huyu Dr Lwetama ninayemfahamu mimi amekua mpuuzi kwa viwango hivi?

Source: BBC Swahili sasa hivi iko live.

Wewe unavyodhani na kujua kwani Tanganyika ipo?

 
Ndo maana mimi hata mtanzania aniambie yeye ni DR au Profesa (kasoma vyuo vya Bongo au USSR) mimi huwa sitishiki kabisa. Huwa najua tu kuwa amekaa muda mrefu darasai kukariri basi, lakini upande wa akili na common sense najua tuko sawa tu. Sasa mtu kama Lwaitama, mwalimu wa chuo kikuu anaongea vile je layman asemeje. Nilimuondoa kwenye listi ya wasomi huyu mzee wakati wa mchakato wa urais 1995. Alikuwa anatoa maoni yake kumlengeshea JK kuwa ndo anaafaa kuwa Rais, in short the old man has got no own ideas............ni kama Mjengwa anaangalia upepo wapi next week ataalikwa.....................

Umeniabisha Lwaitama 1964+50 = 2011?. Najua wewe ni historian je hati ya uhuru kutoka kwa Malkia imeandikwa Tanganyika au Tanzania Bara.
 
Tanganyika- naam jina tamu na hatuwezi kulikana kwa hoja dhaifu kama: eti lilibuniwa na wakolon (Lwaitama)i; au Tanganyika ilishakufa! Nani anasema Tanganyika ilikufa? Hivi muungano ukivunjika leo (na hili liko wazi) nchi yetu itaitwaje? Tanzania Bara? Hili si ndo jina tutakuwa tumelikataa baada ya muungano kuvunjika, make hakuna cha umoja wa bara na visiwani tena hapo! Tutaanzisha tena mashindano ya kutafuta jina jipya wakatiTanganyika ipo? Tuache maskhara, Tanganyika inaishi hata kama imefungiwa kabatini.
 
Back
Top Bottom