Lakini tujiulize; inawezekanaje nchi ilivyojaa usalama wa taifa kuanzia uchochoroni hadi Bank wasimjue mchezesha upatu kuwa ni tapeli!
Mwaka wa kwanza, wa pili, wa tatu, wa nne, wa tano tapeli anafanya miamala kimyaa!
Tapeli anasambaa kijiji, kitongoji, wilaya, mkoa hadi taifa kimyaaa!
Hadi mwalimu mmoja anapolalamika ndipo tunajua huyu mcheza upatu ni tapeli. Katapeli bilioni 17, hilo ni kosa!
Tapeli anahukumiwa faini ni million 5 kama hana jela itamhusu!
Halafu akaunti na mzigo wote wa 15 bilioni UNATAIFISHWA! (Ni kosa kuwarudishia waliotapeliwa)
Tapeli tunamwachia aende zake (Case closed)
Mimi niliyeishia darasa la saba nisaidieni kumtambua Tapeli ni yupi!
=========
Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP), Biswalo Mganga amesema ni kosa kuwarejeshea fedha watu waliojiunga na kampuni ya QNET kisha kudai wametapeliwa kwamba kufanya hivyo ni kosa.
Ameeleza hayo jana katika mahojiano maalumu na gazeti hili ikiwa ni siku mbili baada ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) mkoani Geita kurejesha Sh5.48 milioni kwa mwalimu Rose Mgomba wa Shule ya Msingi Lukaranga aliyedai kutapeliwa.
Wasiwasi watanda kampuni ya QNET
Katika maelezo yake, Mganga alisema urejeshwaji wa fedha hizo ni kosa kisheria kwa sababu biashara iliyokuwa inafanywa na kampuni hiyo ni upatu haramu.
Mbali na kukemea suala hilo, alizitaka taasisi zinazofanya uchunguzi kuhusiana na sakata la kampuni ya QNET kushirikiana kwani wanajenga nyumba moja.
Alisema shughuli inayoendeshwa na kampuni ya Qnet ni upatu na tayari Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) ameanza upelelezi kuhusiana na sakata hilo.