DPP kuiadhibu CHADEMA?

If people are good only because they fear punishment, and hope for reward, then we are a sorry lot indeed.

 
MSAJILI wa Vyama vya Siasa nchini, John Tendwa amesema yupo sahihi katika utendaji wa kazi yake, kwa kuwa anafuata sheria na kwamba endapo Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kitapuuza barua yake ya onyo, sheria za nchi zitachukua mkondo wake ikiwamo kufunguliwa mashitaka na Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka nchini (DPP).

Aidha, Tendwa amesema kamwe hatakitetea wala kukionea huruma chama chochote cha siasa, kikiwamo Chadema endapo kinakiuka sheria nchini.


Alisema kwa kuwa amewaandikia barua Chadema ya onyo, anaamini watatekeleza sheria kwa kufuata taratibu zinavyotaka, lakini kama wakiamua kumpuuza kama walivyodai viongozi
wake, sheria itachukua mkondo wake ikiwamo Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP), kuona ulazima wa kuwachukulia hatua za kisheria kwa mujibu wa sheria au kwa maagizo ya Msajili huyo.

Alitoa kauli hiyo siku moja baada ya Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Willibrod Slaa kuliambia gazeti hili kuwa Msajili huyo amepoteza sifa ya kushika wadhifa huo kutokana na madai kuwa anakipendelea Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika mambo mbalimbali, na kutofanyia kazi malalamiko anayopewa na Chadema.


Katika maelezo yake, Dk. Slaa alilitaja tukio la Jeshi la Polisi mjini Arusha kuwalipulia mabomu ya machozi wafuasi wa chama hicho wakati wa kutawanya maandamano yao mjini Arusha mwanzoni mwa mwaka huu na kusema kuwa licha ya kumuandikia Tendwa barua kulalamikia suala hilo, hakuchukua hatua yoyote.


Akizungumza na gazeti hili kwa simu, Tendwa alisema kwa wadhifa wake, anawajibika kukataza au kuvionya vyama vinavyojihusisha na vitendo vya aina yoyote vyenye kuashiria kuchochea machafuko yenye kusababisha uvunjifu wa amani nchini bila kujali kama ni vya upinzani au chama tawala.


Lakini Tendwa alisema hashangazwi na jambo lolote linalozungumzwa au litakalozungumzwa na Dk. Slaa, kwa madai kuwa anayafahamu matatizo yake ya kuropoka hovyo kutokana na kukosa busara.


"Anachotaka Dk. Slaa ni kunichafua tu, lakini hilo halinisababishi nipindishe sheria katika utendaji wangu na kukipongeza Chadema pale kinapokosea.


Nashukuru kwamba anafahamu vizuri kuwa ninawajibika kwa kufuata sheria na sina woga wala unafiki utakaonifanya nikipendelee chama kimoja na kuvikandamiza vingine kwa sababu za kushinikizwa, upendeleo binafsi au hofu ya kutukanwa kama anavyonifanyia yeye," alieleza Tendwa.


Akifafanua tukio la Arusha, alisema Jeshi la Polisi lilikuwa sahihi kujihami kwa mabomu yale na Chadema ilikuwa imekosea kisheria kulazimisha maandamano yale na hata kutaka kuvamia kituo cha polisi.


"Tatizo la Dk. Slaa ni ufikiri mdogo na kukosa busara, hawakuwa na haki kwa lolote kule Arusha hivyo alipaswa anyamaze na kukishauri chama chake kufuata sheria.


Kila mtu aliona kilichotokea, sasa alitaka mimi nichukue hatua gani dhidi ya Dola? Sana sana walistahili onyo kwa kutishia amani ya nchi na sio kutetewa," alieleza Msajili huyo.


Kwa mujibu wa Tendwa, Padri huyo wa zamani wa Kanisa Katoliki, anapaswa kutulia na kujiuliza ni vipi atarudi kwenye mstari ulionyooka baada ya kuharibu kwa Mungu na wala sio kusimama mbele kuleta vurugu nchini kwa kutumia chama cha siasa.


"Unajua alisoma sana dini hata akaitwa daktari, sasa huyu nilitegemea angekuwa kiongozi wa amani nchini na mfano wa busara kwa wengine, lakini nasikitika kuwa anakuwa mchochezi wa vurugu kwa kupitia chama chake cha siasa," alidai Tendwa na kuongeza:


"Simshangai Dk. Slaa kwa kuwa nauelewa ufikiri wake finyu, aliweza kuharibu kwa Mungu, sembuse kwenye siasa?


Sasa kama ninalijua hilo kwa nini niendekeze vitendo viovu vinavyoweza kuvuruga amani nchini? "Nitaendelea kuchukua hatua za kisheria kwa chama chochote kitakachokiuka sheria na wala sitabagua.


Sasa cha msingi akubali kufuata sheria ili mambo yaishe, vinginevyo hata kwa shetani nako kutamshinda."


Akimaananisha katika siasa. Katika hatua nyingine, mwanasiasa mkongwe na kada wa CCM, Chrisant Mzindakaya amekitaka chama hicho kujibu hoja za Chadema kwa kuwatumia viongozi wa mikoa ambayo Chadema wanafanya mikutano.


Aidha, alihoji iweje Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC) kuwa kimya muda wote kama iko likizo na kuiachia Serikali kazi ya kisiasa hasa katika kipindi hiki.


Mzindakaya aliliambia gazeti hili kwa simu jana kuwa hali inayoendelea sasa ni mchezo wa kisiasa ambao CCM wanatakiwa kujibu hoja katika mikoa ambayo Chadema wanapita na kutoa hoja zao za uchochezi.


Alisema pia NEC ya CCM inatakiwa kukutana na kutoa tamko kwani chama cha kisiasa kikubwa na chenye sifa kama CCM hakiwezi kuacha Chadema ikaendelee kuvuruga nchi.


"Viongozi wa CCM katika mikoa ambayo Chadema wanapita na kutoa hoja zao, wajibu kwa kuponda hoja hizo ili wananchi waelewe hali halisi na siyo kumsubiri Waziri Mkuu au Rais kujibu hoja," alisema Mzindakaya.


Mwanasiasa huyo aliyekuwa mbunge kwa takribani miaka 40 kabla ya kustaafu mwaka jana, alisema wakati huu ndipo kazi ya kisiasa inatakiwa ifanyike kwa nguvu katika kuelimisha wananchi nini Chadema wanachofanya na siyo kunyamanza kimya na chama hicho cha upinzani kuonekana wanazungumza ukweli.


Ameitaka Chadema kushirikiana na Serikali kuleta maendeleo na siyo kuwagawa wananchi kwani kwa kuwa na wabunge wengi, walitakiwa kushirikiana na Serikali kujenga nchi wakianzia katika majimbo yao.


Alisema uchaguzi umeshafanyika na Serikali imepatikana kinachotakiwa sasa ni kuhangaikia maendeleo kwa kutumia viongozi makini kutoka vyama vya siasa na siyo kuwagawa wananchi.


Chanzo: Habari leo

Tutegemee nini kutoka kwa mtu kama huyu:blah::blah::blah::blah::blah:.Hii ndiyo picha halisi ya chama tawala CCM pamoja na serikali kuanzia Rais JK.Kwa uongozi huu chini ya JK tusitegemee viongozi waadilifu au kauli za busara kwani ni maajabu kwa kiongozi dhaifu kua na timu imara.Atajitahidi kuweka viongozi walio dhaifu kuliko yeye watakaomwabudu na kumlinda kwa kila kitu awe sahihi au la .Dr.Slaa na CHADEMA walipo ibua kashfa za ufisadi na kuwataja wahusika wakuu mwembeyanga,walitwa waropokaji,wachochezi na matusi mengi nini kilifuata?Kwa maandamano ya CHADEMA CCM ijibu hoja si vinginevyo kimya chao ni kua hawana majibu na ukweli uko wazi CCM haina majibu ya kujibu hoja za CHADEMA.Kama alivyo Tendwa,Rais JK,na mafisadi ni bendera kufuata upepo na upepo wao ni ROSTAM AZIZ.JK,CCM,TENDWA,SERIKALI NA MAFISADI NI AIBU KWA TAIFA NA UDHALILISHAJI WALALAHOI.MUNGU IBARIKI TANZANIA.
 
“Viongozi wa CCM katika mikoa ambayo Chadema wanapita na kutoa hoja zao, wajibu kwa kuponda hoja hizo ili wananchi waelewe hali halisi na siyo kumsubiri Waziri Mkuu au Rais kujibu hoja,” alisema Mzindakaya.

kweli mzee umesema.
 
Talking too much bila kutoa suluhisho la tatizo is one of the bla_bla. Bei ya vitu iko juu has chadema given any idea how to reduce it? You reduce by maandamano. Nani hajui kama maisha ni magumu. Nchi zote the life is tough. Is dowans the only resource we depend by means of fund. Pesa zinazotumika kupita mikoani shouting wangewapa mikopo wenye maisha ya kubahatisha. Otherwise they have to stop cheeting people. Nguvu ya umma wakati ni umma wa chadema pekee. Not all citizens like Chadema the way they behave.
Hizo frustration za uchaguzi. Wanajifariji sasa kwa kushawishi wananchi kuwa barabarani.
 
kumbe Habari Leo???/
sasa mlitegemea waandike nini???
wala sina haja ya kujibizana na watu hapa.
 
:blah::blah: tendwa anajua anatetea ulaji wake ila ukweli unabaki pale pale na yeye deep inside anajua cdm wako right in every way

uwezo wa kuifuta cdm hana, cdm sio chama cha makamba au rosti tamu.. cdm ni nguvu ya umma! let him dare..
 
niliwah ckia huyu Tendwa ni sh....ga, hv ni kwel au? Maneno yke yananfnya nianze kuamin. Kwel Tendwa umetendwa knyume na ma.....le! Hacra za nn baba? Taratb basi shost.
 
Mimi nadhan mh. Tendwa anapomkashfu Dr. Slaa kama ni maadili ya kazi yake? ajue kabisa wakati anaandika barua ya onyo alimwandikia mtu binafsi au chama cha siasa iweje akashifu hadi iman ya mtu ndio maadili ya kazi yake? Huyu Tendwa miaka ya nyuma aliisha ingilia hadi utendaji wa chama cha UDP na alimsimamisha mwenyekiti wa chama hicho baadaye akaona aibu, kama ni mwanachama wa chama chochote ni dhahiri azizuie hisia zake, Kikwete kipind cha kampeni alisema kuwa cdm ni chama cha msimu kimefuata ushauri wake tena anabadilisha kauli kuwa wameanza uchochezi sasa na huko bungeni hapatakalika ajue kabisa pamoja na kumweka yule mama ili awazibe midomo wenzake.
 
[Tendwa alisema hashangazwi na jambo lolote linalozungumzwa au litakalozungumzwa na Dk. Slaa, kwa madai kuwa anayafahamu matatizo yake ya kuropoka hovyo kutokana na kukosa busara.

“Tatizo la Dk. Slaa ni ufikiri mdogo na kukosa busara, hawakuwa na haki kwa lolote kule Arusha hivyo alipaswa anyamaze na kukishauri chama chake kufuata sheria

Sasa cha msingi akubali kufuata sheria ili mambo yaishe, vinginevyo hata kwa shetani nako kutamshinda .

Najiuliza huyu bwana Tendwa maneno haya alioongea kama nani?
  1. Mwanasheria
  2. Mwanasiasa
  3. Muhuni tu
  4. Mwana mipasho
  5. Kuwadi
  6. au kama nani?
 
niliwah ckia huyu Tendwa ni sh....ga, hv ni kwel au? Maneno yke yananfnya nianze kuamin. Kwel Tendwa umetendwa knyume na ma.....le! Hacra za nn baba? Taratb basi shost.

Inawezekana kweli kwani Tendwa ni mlevi wa kutupa, halafu akilewa mdomo wake hauvai Condom
 
Kwa mujibu wa Tendwa, Padri huyo wa zamani wa Kanisa Katoliki, anapaswa kutulia na kujiuliza ni vipi atarudi kwenye mstari ulionyooka baada ya kuharibu kwa Mungu na wala sio kusimama mbele kuleta vurugu nchini kwa kutumia chama cha siasa.

Nimependa sana haya maneno ya Tendwa kumbe nae anajuwa kama huyu padri katumwa na kanisa katoliki (wafutilie mbali baba)

Haya endeleeni kukukuruka mie nawasikiliza munavyoparamiana
 
Kwa nini Chadema msiitishe maandamano hapa Dasalama? Nina usongo wa kufa mtu. Tutapiga hodi hapo nyumba ya domocrazy mtaa wa shaban robert.

Du ze nidful pliiz!
 
Kwa Kauli ya Tendwa nashindwa kuamini kua imetoka kwa mtu aliye pewa madaraka makubwa ya kusimamia vyama vya siasa.

Tendwa hapaswi kutoa maneno ambayo unaweza kuyatafsiri kama ni matusi kwa kiongozi mkubwa wa chama cha CDM, Je anaweza kutoa kauli ya kejeli kwa mkuu wa CCm ambayeni JK kwa kiwango hicho hicho? au anataka kumfurahisha huyo alie muweka hapo na sio kwa maufaa ya taifa hili?

Tendwa anatakiwa aombe RADHI Kwa Dr. Slaa Na Wa TZ wote.
 
Mimi nimegundua Tendwa ndio anauelewa Finyu sana na anakurupuka,

Kwanza wafuatao ni wateule wa JK na hawawezi kutenda kinyume na maslahi ya CCM ama JK na Serikali yao:
1. Msajili wa Vyama, na hata huyo DPP
2.Jaji Mkuu
3.Mkuu wa Jeshi la Polisi
4.Mkuu wa Jeshi la Ulinzi JWTZ
5.Mwanasheria Mkuu
6.Mkurugenzi wa Takukuru
7.Waziri Mkuu (ingwa huwa anathibitishwa na Bunge lakini bado ni uteuzi wa JK)
8.Wakuu wa Mikoa na Wilaya.

unategemea Chadema wampelekee nani kilio chao kati ya hao hapo juu!!?:A S 13:

sasa kwa hali kama ilivyo Chadema hakiwezi kutendewa haki popote kama kinaoneka kuwa ni tishio la ajira la hawa wote, sasa kwa kuwa mwajili wa JK ni wananchi, Chadema kimeona ni vyema kuwaeleza wananchi jinsi ambavyo mali zao zinavyohujumiwa na wao kujikuta kati kati ya dimbwi la umaskini.

CCM na hao hapo juu walizoea kuona wananchi wakidaganywa, kukandamizwa na kuachwa gizani, na kwa mfumo huu wa vyama vingi bado walitegemea kupata nafasi ya wao kuendelea kuwadanganya wananchi kwa ziara za wakubwa kama waziri mkuu, rais na makamu wa rais wakitumia mali za serikali kwa mgongo wa ziara za kikazi za serikali kumbe wanahubiri sera zao za CCM huku vyama vingine vikiwa vimelala Vikisubiri uchaguzi mkuu mwingine ndio wapate muda kiduchu wa kutangaza chama na sera zao.

Sasa CHEDEMA hakidanganyiki kimegundua hilo na kitaendelea na mikutano ambayo pamoja na ubovu wa katiba iliyopo lakini imeruhusu kuwa ni haki ya watanzania kuandamana, kukutana na kufanya mazungumzo.

Chadema Songa Mbele usisikilize maneno ya vibaraka kama akina Tendwa.

naomba kuwasilisha.
 
sidhani kama tendwa ndiye aliyesema maneno ya chooni labda atakuwa miraji kikwete ndiye mwenye akili ndogo kam sisimsi na kama ni tendwa basi uyu ni mbakaji wa haki za watu na ana ufukara wa mawazo hafai anahitaji kunyongwa bila huruma uyu ni fisadi wa haki.
 
Tendwa Gongo imemuharibu akili kabisa; Shime Marando na Tundu tunataka kesi ya tendwa kumtukana Dr Slaa, ipandishwe mahakama kuu sasa hivi..
 
Back
Top Bottom