DPP kufuta kesi ya Iddi Simba ni dhihaka kwa raia

DPP kufuta kesi ya Iddi Simba ni dhihaka kwa raia

kmbwembwe

JF-Expert Member
Joined
Aug 16, 2012
Posts
10,931
Reaction score
7,828
Mwenye macho haambiwi ona, lakini akiona ajabu anaweza kuduwaa kimya mithili hajaona kitu. Kufutwa na DPP kesi iliyokua inamkabili Idi Simba Na wenzake kwa makosa ya uhujumu uchumi ni jambo lililowastaajabisha raia wengi.

Makosa yao ilikua ni pamoja na kuchakachua hisa za shirika la UDA kwa kuzionyesha zina thamani ndogo kuliko hali halisi na kuziuza kwa kampuni ya Simon group hisa hizo kwa bei sawa na bure. Kosa linginne ni kupokea fedha za mauzo ya kampuni hiyo na kuziweka kwenye akaunti zao binafsi.

Ushahidi wa CAG dhidi ya watuhumiwa ulikua barabara ndio maana kesi ikapandishwa daraja kua ya uhujumu uchumi. Wanaoelewa walianza kutilia shaka pale watuhumiwa walipokubaliwa dhamana kwani kesi ya uhujumu uchumi haina dhamana.

Baada ya kufutwa kesi hiyo yapo maswali yanahitaji majibu
1. Je uuzaji wa UDA sasa kisheria ikoje, ndio wizi huu wa mali ya umma umebarikiwa?
2. Hiyo fedha ya umma iliyowekwa mfukoni kwa watu binafsi ndio wizi huo umehalalishwa na DPP?
3. Je DPP kwa nini asiwajibishwe kwa kufuta kesi hiyo?

Hakuna shaka tena katika nchi hii ushirika wa chama tawala serikali na mafisadi ni imara sana. Tulisikia waziri mkuu hivi karibuni akimtaja Idi Simba bungeni kwa unyenyekevu 'Mzee wetu Idi Simba'

Jeuri ya mafisadi sasa iko wazi kutokana na mbinu ya hadaa sasa kugonga mwamba kwani wananchi wamefumbua macho. Sasa ufisadi umeanza kutumia ubabe kwa kuwashambulia raia kwa njia binafsi na kutumia polisi. Juzi waziri mkuu amewaeleleza polisi kuwapiga raia.

Bila shaka polisi watatumiwa kuwapiga wapinzani wa kisiasa kwa kisingizio cha kutotii amri. Msisahau Hoseah wa takukuru naye anamlalamikia DPP kwa kuwekea kifua kesi za mafisadi papa.

Wana jf nawasilisha.
 
sishangai, kwani sijawahi kumwona mwenye hela tena kada wa chama chetu kikongwe eti akafungwa -neva
 
Idd Simba ana rekodi chafu ya ufisadi hivyo wala sihitaji ushahidi wowote kuamini kuwa ana hatia. Nadhani DPP ametumia advantage ya mabomu ya arusha ili watu waelekeze akili huko na kutotilia maanani suala la Idd Simba. Sielewi kwanini DPP ana nguvu kisheria kiasi hiki.
 
Naomba wataalamu wa sheria wanijuze hapa - je, wanaharakati au asasi za utawala bora wanaweza kisheria kuifufua hii kesi mahakamani? Je, wanaweza kumfungulia mashtaka DPP kwa matumizi mabaya ya ofisi ya umma?
 
Walimkamata Rwekatare kwa kesi ya kuchonga ili wawaweke Chadema busy kutoa nafasi ya kuchakachukua hukumu ya ubunge sumbawanga. Wakapiga bomu kanisani Arusha wapete nafasi ya kutengua hukumu ya ubunge Igunga. Wakapiga bomu mkutano wa chadema ili wapate nafasi ya kufuta kesi ya Idd Simba na kupitisha budget yao mbofu mbofu. Watahakikisha kwamba uharamia utaendelezwa mfululizo kuruhusu bomba la gesi ya Mtwara linafika Dar. Tutarajie uvunjifu wa haki za kibinadamu kwa kiwango kukuu sasa maana Pinda keshasafisha uwanja kwa polisi walio mstari wa mbele kutumiwa kuondoa amani.
.
 
Miongoni mwa watu waliokubali kutumika vibaya na watawala ni DPP (Eliezer Feleshi) kwani kwa sasa hatumii weledi na maarifa katika kutenda kazi yake zaidi ya kusubiri kupokea maagizo kutoka kwa watawala na kupanga namna ya kulinda wahalifu na wezi wa mali za umma.

Ni aibu kubwa kwa DPP kukubali kushiriki dhambi na uovu unaoshamiri sasa hivi hapa nchini wa kupanga matukio ya uongo na kuandaa kesi za kubambikia watu fulani huku wezi wakikingiwa kifua na kulindwa kwa nguvu zote. Ni aibu kubwa inapofikia mahali DPP anadiriki kuingilia na kuvuruga utendaji wa mahakama na vyombo vingine vya umma kwa minajili ya kutimiza matakwa ya watu fulani ama kikundi Fulani huku jamii ikiendelea kutaabika kwa maamuzi ya hovyo ya watu fulani.

Hayo wanayofanya ni uovu uliokidhiri ndani ya taifa letu, ni uvunjifu wa amani na haki za msingi za raia wa nchi hii, hakika Feleshi amekubali kutumika lakini hao wanaomtumikisha kwa masilahi yao binafsi hawatamtetea ama kusimama naye pale jamii itakapopaza sauti kudai haki yao.

Yanayotokea sasa kwa baadhi ya watendaji kuanza kudai kuwa utendaji wao wa kazi unakwamishwa na maamuzi yanayofanywa na ofisi ya DPP ni ishara tosha kuwa hayo anayofanya DPP yatamrudia na itabidi awajibike aidha kwa wema ama ubaya.
 
Mnalalamika nini? Ninyi mumewahi kuchangia chama? Hivi michango inayotolewa kuchangia chama mnafikiri pesa zake zinatoka wapi? Mtanzania gani Zaidi ya Mzee Sabodo aliyenakipato halali kinachotosha kwa familia yake naakabaki na ziada ya kuchangia Siasa? Ukifanikiwa kuchota sehemu yoyote,kisha kiasi fulani peleka Chamani utakuwa salama tuu.Chama kinawenyewe na wenyewe ndiyo..........!Kwa kesi hii naomba Mh,Pinda amuelewe Mkuu wa TAKUKURU Dr,Hosea aliposema anapokuwa anashughulikia kesi kubwa anashikwa mikono!!
 
...Hapa tatizo ni Katiba yetu MBOVU basi, someni hio ibara ya 59 ya katiba muone huyo DPP alivyo na mamlaka makubwa...

Director ofPublic
Prosecutions
Act No.1
of 2005
59B.-(1) There shall be a Director of Public Prosecutions who shall be
appointed by the President from amongst persons with qualifications specified in
subarticle (2) of Article 59 and has continuously held those qualifications for a
period of not less than ten years.
Art.12 (2) The Director of Public Prosecutions shall have powers to institute,
prosecute and supervise all criminal prosecutions in the country.
(3) The powers of the Director of Public Prosecutions under subarticle
(2), may be exercised by him in person or on his directions, by officers under him,
or any other officers who discharge these duties under his instructions.
(4) In exercising his powers, the Director of Public Prosecutions shall be
free, shall not be interfered with by any person or with any authority and shall
have regard to the following -
(a) the need to dispensing justice;
(b) prevention of misuse of procedures for dispensing justice;
(c) public interest.
(5) The Director of Public Prosecutions shall exercise his powers as may
be prescribed by any law enacted or to be enacted by the Parliament.
 
Kwa mtindo huu Serikali ya CCM itatafuta mchawi weee mpaka siku ya kiama.Kumbe mbaya si wanaharakati,Chadema nk.Mbya wa CCM ni CCM yenyewe!Hii kesi mbona ipo wazi kabisa?sasa DPP ametumia vigezo gani kuifuta?......haya mambo ndo yanaoyofanya nchi isitawalike-wala sio Chadema!
 
Sisi waumini wa Kikatoloki tuna msemo kwamba Akilacho Padre pale altareni muumini usimezee mate. Mbuzi hula kulingana na urefu wakamba yake.

Huyu Mzee aliji- Chukulia Chake Mapema
 
kesi haina kichwa wala miguu ilifunguliwa kwa ajili ya public interest na imefutwa kwa ajili ya public interest kilichofanywa na dpp ni sahihi kabisa
 
sishangai, kwani sijawahi kumwona mwenye hela tena kada wa chama chetu kikongwe eti akafungwa -neva
Rajab Maranda ni kada wa CCM aliyefungwa kwenye kesi ya EPA kama kumbukumbu zangu ni sahihi!Hata hivyo I stand to be corrected.


Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
Kama pesa iko uswisi,kagoda,epa wamekula mnataka iweje?ivi ni nan kati ya watawala wetu wa sasa ana moral authority ya kumfunga mwenzie?kwa sasa hayupo-akipigwa mkwara anamkumbusha bosi wake,bosi hapa mkinifunga mtanikoma-basi ananyanyua simu- ww d ipi pi futa iyo kitu.
 
Tangu mwanzo nilijua kesi ya Idd Simba itapigwa chini ilikuwa ni suala la muda tuu na si vinginevyo.Kwanini Idd Simba ashitakiwe ikiwa yeye ni miongoni mwa wateule wachache wenye haki ya kufanya chochote bila kushtakiwa.Ikumbukwe Idd Simba ni muanzilishi wa sera za uzawa kama si Mwl Nyerere kupiga kelele ubaya wa sera ya uzawa ambayo ililenga kunufanisha wanasiasa na viongozi wakuu wa kiserekali.Baada ya sera ya uzawa kutupwa Idd Simba akajiingiza katika makundi ya kupigania haki za waislamu nia na madhumuni yakiwa ni yale yale ya kutumia mwavuli wa dini ili kujinufaisha yeye na kikundi chake Saigon kashindwa mikono yake iliyojaa tamaa ya mali ikamlazimu atimuliwe wizara ya biashara na viwanda kupitia misamaa ya kodi haramu ya sukari.

Ghafla Idd Simba akaibukia kama mwenyekiti wa wazee wa Dar nikacheka,nikajua kesi yake ya ufisadi UDA haina nguvu tena kwani jukwaa alilokimbilia ni jukwaa muhimu sana kwa Rais Kikwete.Najua Felesi kaambiwa kijana ebu futa hiyo kesi ya Simba na wenzake kwa maslahi ya taifa.Kwakuwa katiba yetu mbovu haina kipengele cha kuhoji maamuzi ya mkurugenzi wa mashtaka hiyo ndiyo basi tena tusishangae majambazi yakikimbilia siasa kwakuwa huko kuna kinga nzuri ambayo huitaji mawakili mahiri.
 
Tangu mwanzo nilijua kesi ya Idd Simba itapigwa chini ilikuwa ni suala la muda tuu na si vinginevyo.Kwanini Idd Simba ashitakiwe ikiwa yeye ni miongoni mwa wateule wachache wenye haki ya kufanya chochote bila kushtakiwa.Ikumbukwe Idd Simba ni muanzilishi wa sera za uzawa kama si Mwl Nyerere kupiga kelele ubaya wa sera ya uzawa ambayo ililenga kunufanisha wanasiasa na viongozi wakuu wa kiserekali.Baada ya sera ya uzawa kutupwa Idd Simba akajiingiza katika makundi ya kupigania haki za waislamu nia na madhumuni yakiwa ni yale yale ya kutumia mwavuli wa dini ili kujinufaisha yeye na kikundi chake Saigon kashindwa mikono yake iliyojaa tamaa ya mali ikamlazimu atimuliwe wizara ya biashara na viwanda kupitia misamaa ya kodi haramu ya sukari.

Ghafla Idd Simba akaibukia kama mwenyekiti wa wazee wa Dar nikacheka,nikajua kesi yake ya ufisadi UDA haina nguvu tena kwani jukwaa alilokimbilia ni jukwaa muhimu sana kwa Rais Kikwete.Najua Felesi kaambiwa kijana ebu futa hiyo kesi ya Simba na wenzake kwa maslahi ya taifa.Kwakuwa katiba yetu mbovu haina kipengele cha kuhoji maamuzi ya mkurugenzi wa mashtaka hiyo ndiyo basi tena tusishangae majambazi yakikimbilia siasa kwakuwa huko kuna kinga nzuri ambayo huitaji mawakili mahiri.

.
Watendaji baada ya kushtuka kuwa ikulu kuna boya wanaamua na kutenda watakavyo. Lakini haya yanayofanywa na watawala kwa sasa ni kwa maangamizi yao wenyewe.
.
 
Idd Simba ana rekodi chafu ya ufisadi hivyo wala sihitaji ushahidi wowote kuamini kuwa ana hatia. Nadhani DPP ametumia advantage ya mabomu ya arusha ili watu waelekeze akili huko na kutotilia maanani suala la Idd Simba. Sielewi kwanini DPP ana nguvu kisheria kiasi hiki.

Uchafu wa Idd Simba na Ufisadi wote huo tangu huko nyuma SUKITA, NASACO,SUKARI amepona tu kwa kuwa ni mzee wa ccm na swahiba wa Mkwer..e katika kijiwe cha SAIGONI. Katika nchi za haki na democrasia IDDI SIMBA HAFAI KUWA HATA MJUMBE WA KAMATI YA MAULIDI YA MTAA AU MAZISHI.LAKINI BADO NI DIRECTOR WA KAMPUNI KADHAA WAKATI ALIKWISHA KOSA SIFA HIZO.
 
KWANI KK HUJUI KUWA CHAMA KINAENDESHWA NA MAFISADI? UFISADI NDIO MSINGI MKUU WA CHAMA NA SERIKALI YA CCM. huwezi kuutenganisha ufisadi na ccm na usishangae DPP kufuta kesi ya simba na kupinga rufaa ya rwakatale..
DAWA YAO NI VIJANA KUKATA SHAHADA YA KUPIGA KURA NA KUFANYA MAAMUZI SAHIHI..
 
Back
Top Bottom