DPP amfutia mashtaka Prof. Lipumba na wenzake

DPP amfutia mashtaka Prof. Lipumba na wenzake

Kwani Lipumba hana haki ya kufutiwa mashtaka?kwani siyo Mtanzania?.Hivi akipewa uwaziri au whatever nafasi ya kuwatumikia Watanzania kuna kosa gani?Tanzania ya kwetu wote .Acheni ubaguzi wa kijinga
Nakupa LIKE mkuu
 
ni utawala tu wa kimabavu walimfungulia kesi alipokua cuf saivi hayuko tena na cuf eti kesi imefutwa wafutieni kesi na wale mashekhe wetu mlio watia rumande bila kosa lolote mpaka leo mmeshindwa kuwahukumu tambueni tu kwamba hapa duniani tunapita kabla yenu kulikua na wenye nguvu zaidi yenu hii leo wako katika ndani ya ardhi na nyinyi mtaondoka na itabaki historia tu kua kulikua na utawala wa kimabavu ukiongozwa na ccm japo kua mnajiona kua mtaishi hapa duniani daima kama mnavyosema maneno yenu ya daimaaa
 
kama kweli ni mzalendo amteue lissu kuwa waziri wa sheria na katiba. pia amteue halima mdee awe naibu waziri wa ardhi hapo nitaamini kwamba yeye ni mzalendo...

utamteua vipi mtu asiyetambua matokeo Yaliyokuweka Madarakani? Waambie wakubali kwanza then ndio wafanikiwe
 
kuna kila dalili za Prof Lipumba kupata nafasi ya kumsaidia Mhe Rais katika awamu hii serikali ya awamu ya tano katika nafasi ambayo Rais ataona inamfaa.kwanini natabiri hilo sababu
1.Prof kaenda kuongea na Mhe Rais.
2.Prof kafutiwa kesi ambayo ilipaswa kutajwa 15/01/2016
3.Prof alikuwa anazungumza kwenye kituo cha TV TBC1 "live" 03/12/2015.
Sii kawaida mambo haya kufanywa kwa mtu ambaye si mwanachama wa chama tawala.
 
JPM usisahau kuipitia POLISI pia imezoea kusumbua raia bila sababu, kama watu wanaandamana kwa amani kazi yao ni kulinda sio kuzuia ili wakalale. Tumewachoka. Ni jipu la kutumbua
 
Kesi yenyewe ilikuwa ya kitoto. Intelijensia za kipolisi wa Tanzania ni dhihaka kwa weredi wa taaluma hiyo duniani. Mkwere aliliuwa kabisa jeshi hili! Likabaki kuwa aibu ya dunia!
 
Mkuu sheikh ponda hajaachiwa ila kashinda kesi

Na hukumu yake ilikua imeandaliwa tarehe 18/18/2015 hata kabla uchaguzi haujafanyika kaka uwe unaongea na ushahidi[/QUOTE]
Wewe sasa ushahidi gani huu uliotoa, hizo tarehe ni za sayari gani !!!!!
 
Baada ya siku moja Mheshimiwa Rais kukutana na Prof Lipumba, kesi yake ikafutiliwa mbali. Kwa Maoni yangu hii kesi imefutwa kwa huruma ya mheshimiwa Rais.

Kinachonifanya nione haya ni kuwa hii kesi ilikuwa isikilizwe Jan 2016 lakini mara baada ya Prof kukutana na Mh. Rais ikabidi isikilizwe kwa hati ya haraka.

Asante sana Rais kwa hili.
 

Attachments

  • image1.png
    image1.png
    204.2 KB · Views: 210
  • image2.png
    image2.png
    112.4 KB · Views: 192
Kamwambia kilichojili

Kwa hiyo kapewa data na mtuhumiwa.
 
huyo ndo magufuli bhanaa katika ubora wake...kesi za unafiki futilia mbali saiz ni mda wa kujenga nchi na kukamata wezi waliotuibia hela zetu
 
Hata ingeendelea wala asingekutwa na hatia, kesi ilikuwa ni mihemuko ya kisiasa.
 
Back
Top Bottom