Dowans lazima walipwe



SAHIHI NDUU KITUKO EMBU TUJIKUMBUSHE KIDOGO RIPOTI YA BUNGE AMBAYO INAONYEHS TANESCO WALIINGIA MKATABA HALALI NA DOWANS JAPO KWA KUSHURUTISHWA NA WIZARA,NA HAPA MIMI NDIO NASEMA HAWA WALIOIPOTOSHA TANESCO TUWAFILISI,TUWAFUNGE ILA DOWANS WALIPWE HARAKA KUEPUSHA BALAA ZAIDI

Ripoti ya Mwakyembe inasema kuwa
"Tarehe hiyo hiyo 28 Novemba 2006 uongozi wa TANESCO ulimshauri Mwenyekiti wa Bodi kama ifuatavyo:-
(i) Mkataba kati ya Richmond Development Company LLC na TANESCO hauruhusu kukabidhi majukumu ya Mkataba kwa Kampuni nyingine isipokuwa kwa maafikiano ya pande mbili za
Mkataba (Kifungu 15.12)." Tarehe 4 Disemba, 2006
(chini ya siku kumi tangu Karamagi adokeze nia ya Richmond kuhamisha mkataba)
TANESCO walipokea barua kutoka Richmond ambayo ilionesha kuwa kampuni hiyo ilitaka "kutumia haki yake chini ya Kifungu 15.12 cha Mkataba ili kuhamisha majukumu yake yote ndani ya Mkataba huo kwenda kwa DOWANS Holdings, S.A. Aidha, Richmond Development Company LLC ilieleza kwamba tarehe ambayo TANESCO itaridhia mapendekezo hayo iwe ndiyo tarehe rasmi ya kuhamisha mafao na majukumu yote kwa DOWANS Holdings, S.A na kwamba DOWANS Holdings, S.A itawasilisha vielelezo vya utambulisho wake kwa TANESCO"

Hata hivyo, barua hiyo ambayo TANESCO waliipokea Disemba 4, inaonesha kuwa iliandikwa
Novemba 9, karibu mwezi mmoja kabla. Siku moja kabla ya kupokea barua ya Richmond kutaka kuhamishia mkataba wake kwa Dowans yaani tarehe 8 Disemba, 2009 TANESCO ilikuwa imeiandikia Benki ya Citibank isaidie kufanya uchunguzi wa kujua kampuni ambayo Richmond ilikuwa inataka kuhamishia mkataba wake ilikuwa ni kampuni gani na yenye uwezo gani kwani japokuwa masharti ya Mkataba yanaruhusu Mkataba kuhamishwa, TANESCO ingependa kufahamu hasa ni nani anayehamishiwa Mkataba huo"
Kamati Teule haikufanikiwa kupata majibu ya Citibank
ila iliambiwa kulikuwa na shinikizo toka Wizarani "kuwa viongozi wa Wizara kama kawaida yao waliishinikiza TANESCO kukubaliana na ombi la Richmond Development Company LLC la kuhamisha mkataba." Ni kutokana na hilo tarehe 21 Disemba, 2006 TANESCO ikaiandikia kampuni ya Richmond kukubali uhaulishaji wa mkataba huo kwenda kwa Dowans kwa barua yenye SEC. 388/12/206 ambapo pamoja na mambo mengine ilitaka "ipate hati ya uthibitisho kutoka Dowans Holdings, S.A ya kuridhia uwajibikaji kamilifu katika kutekeleza Mkataba wa tarehe 23 Juni, 2006, kati ya TANESCO na Richmond Development Company LLC."

Hivyo tarehe 23 Disemba 2006 Mkataba ukaingiwa kati ya TANESCO na Dowans S.A ambao ulikuwa ni kuhamishia mkataba kati ya TANESCO na Richmond kwenda kwa Dowans Holdings S.A.

Kwa mujibu wa ripoti ya Kamati Teule kusainiwa kwa mkataba huo kati ya TANESCO na Dowans Holding S.A kulileta mambo matatu muhimu ;

-"Tarehe 23 Disemba 2006 ndiyo siku rasmi ambayo Richmond Development Company LLC imekabidhi rasmi majukumu yake ya utekelezaji wa Mkataba kati yake na TANESCO kwa Dowans Holdings S.A";
- "Dowans Holdings, S.A itatekeleza majukumu ya Mkataba uliotiwa saini kati ya TANESCO na Richmond Development Company tarehe 23 Juni, 2006 kwa masharti yote kama yalivyo katika Mkataba";
- "Malipo halisi na madeni ndani ya Mkataba kati ya TANESCO na Richmond Development Company LLC, sasa yatakwenda kwa Dowans Holdings, S.A kuanzia tarehe 23 Disemba, 2006."


 
Kwa kweli nimeamini kuwa hapa ni chuo cha mafunzo ni House of Great Thinker, nakushukuru sana sana Son of Soil kwani umenipa somo kubwa sana leo na kuanzia sasa naungana na Watanzania wenye nia njema wanaounga mkono Dowans ilipwe lakini wakiunga mkono pia mafisadi waadhibiwe vilivyo.

Kutoilipa Dowans ni hatari zaidi ila mkono wa kuwafilisi, kawafukuza na kuwafunga kwa kuhujumu uchumi tunao, serikali huku ikiendelea na mchakato wa kuilipa Dowans ianze mchakato maalumu kuwakamata na kuwafilisi hawa wafuatao kwani wanahusika moja kwa moja:

  • Rostam Azizi
  • Nazir Karamagi
  • Ibrahim Msabaha
  • Edward Lowasa
  • Dr. Idrissa
  • Mzee Kazaura
  • Mwanasheria Fungamtama
  • Dr. Ringo Tenga

Na wote waliopitisha zabuni ya Richmond wafunguliwe mashtaka mara moja.
 
Mali zote za ubalozi na wanabalozi, wote wako covered under diplomatic immunity, hivyo hawashiki kitu, hatuna meli yoyote inayokwenda nje ya nje, hatuna ndege, after all, hao Dowans wenyenyewe ni hewa, sasa hiyo attachment wataiomba wapi?.
 
Aisee,
The Son of soil nadhani una hoja nzuri tu lakini hazina mashiko. Hakuna mtanzania asiyejua mchezo uliofanywa na akina Lowasa/ Kikwete na Rostam Aziz kwenye masuala ya Dowans. Hatukatai matakwa ya kisheria iwe ya ICC au mahakama za Tanzania.
Wengi tunachokataa ni malipo kutoka hali tukijua wazi kabisa tunadhulumiwa. Mitambo hiyo ilinunuliwa na fedha zetu wenyewe - Richmond alipewa fedha za kununua mitambo. Imeendeshwa kwa fedha zetu wenyewe na leo wanataka tuwalipe fedha zetu tena!!!!

Hoja zetu zinaweza kukosa nguvu za Kisheria kama kweli itaonekana hivyo na wanasheria, lakini unapotaka kuwashamoto ni lazima kuwe na moshi. Mwelekeo wetu ni kumwajibisha Kikwete na wahusika wote..... It is a matter of Time!!!! Subiri utaona..... Lakini katika yote kwa kuwa wao ndo wameileta Richmond and Dowans basi tumeanza kuwapa homework ya kufukuza jini walilolikaribisha wenyewe bila kuathiri maisha yetu Watanzania wa kawaida.
 
Naona akina Fungamtama ni wengi humu. Someni the Law of contract kwa makini.
 
Umepitia yote hayo kama nani?

Watanzania wengi wameupitia na kuona feki wewe ni R A pandikizi !

Halipwi mtu hadi kieleweki
 
hao mafisadi mnaosema wawajibishwe ni kina nani?

navyojua mimi kesi za upuuzi kama huu sana sana mtu atakula mvua moja na nusu tena hapo baada ya watu kukomaa sana

serikali iliyoko madarakani haina kitu kinachoitwa uwajibikaji kamwe,..
 
Umepitia yote hayo kama nani?

Watanzania wengi wameupitia na kuona feki wewe ni R A pandikizi !

Halipwi mtu hadi kieleweki

Unajipa moyo wa kichaa tuu, lakini Watanzania makini wapo na hawatakubali taifa hili liingie kwenye matatizo zaidi.

Dowans watalipwa mpende msipende na nchi itatulia na amani itaendelea kuwepo.

Wale wote walioidanganya TANESCO watashughulikiwa kikamilifu. Nakuahidi,

Sisi sote tutakuwa hapa hapa Jamii Forum, Dowans wakiwa wanapokea hela zao na kina Karamagi, Rostam na wenzao wakiwa wanafunguliwa mlango wa Segerea kwenda kunywa ndoo tayari wakiwa wamefilisiwa, wakiwa maskini wakutupwa.
 
Sisi kama watanzania hatudanganyiki, Kama umetumwa uje kushawishi watu, unapoteza muda. Kuna kesi imefunguliwa mahakama ya bongo, ngoja tusubiri hukumu.
 
 
kama unapesa mleta mada kalipe lkn hapa halipwi mtu kesi imefunguliwa ya pingamizi sasa uharaka wote wa nini
 
Tutaishamishia egypt hapa TZ ...hakuna kulipwa mtu hapa
 
Amaaa Pasco tenkyu kwa kubaeleza,endelea kubaelezea
 

Umetumwa mjukuu wa fashisti Hitler wee! Usituchanganye hapa -- Karamagi alilazimisha mkataba uhamishwe, Tanesco walipinga kimaandishi na kutoa sababu yae -- kubwa ni kwamba Dowans ilikuwa kampuni ilionekana kampuni isiyojulikana -- yaani hewa.
Hivyo anayepaswa kulipa ni Karamagi -- na JK aliyekuwa anaangalia tu madudu yanatendeka.

Wananchi tugome.
 
Kwani, bastola ndogo kabisa zinazoweza ku-shoot mita 80, zenye viwambo vya kuzuia mlio, zinapatikana wapi? sh ngapi?
 




Kamati Teule haikufanikiwa kupata majibu ya Citibank ila iliambiwa kulikuwa na shinikizo toka Wizarani "kuwa viongozi wa Wizara kama kawaida yao waliishinikiza TANESCO kukubaliana na ombi la Richmond Development Company LLC la kuhamisha mkataba." Ni kutokana na hilo tarehe 21 Disemba, 2006 TANESCO ikaiandikia kampuni ya Richmond kukubali uhaulishaji wa mkataba huo kwenda kwa Dowans kwa barua yenye SEC. 388/12/206 ambapo pamoja na mambo mengine ilitaka "ipate hati ya uthibitisho kutoka Dowans Holdings, S.A ya kuridhia uwajibikaji kamilifu katika kutekeleza Mkataba wa tarehe 23 Juni, 2006, kati ya TANESCO na Richmond Development Company LLC."

Hivyo tarehe 23 Disemba 2006 Mkataba ukaingiwa kati ya TANESCO na Dowans S.A ambao ulikuwa ni kuhamishia mkataba kati ya TANESCO na Richmond kwenda kwa Dowans Holdings S.A.


Usikurupuke ndugu TANESCO NA DOWANS waliingia mkataba halali kabisa tarehe 23 desemba 2006 la maana hapa ni nani aliwadanganya TANESCO,ni nani aliwalazimisha kuingia mkataba huu ila issue ya kuwalipa DOWANS nakuhakikishia tena PIGA UA GARAGAZA DOWANS WATALIPWA BILIONI 94 MPENDE MSIPENDE,TENA SIO MBALI NI MWAKA HUUU HUU

 
kwani, bastola ndogo kabisa zinazoweza ku-shoot mita 80, zenye viwambo vya kuzuia mlio, zinapatikana wapi? Sh ngapi?

bastola ya nini we ngumi hujui?/
 
Hakilipwi kitu hapa, nyie njooni na propaganda zenu za ajabu, eti kuperform, kuperform kitu gani bana?
 
Sisi kama watanzania hatudanganyiki, Kama umetumwa uje kushawishi watu, unapoteza muda. Kuna kesi imefunguliwa mahakama ya bongo, ngoja tusubiri hukumu.

ACHA KULALA SOMA MAMBO NA UYAELEWE KESI ILIYOFUNGULIWA NDIO HII HAPA CHINI ISOME NA UONE KAMA KUNA POINT HATA CHEMBE NI SIASA TUPU NA BLAA BLAA NYINGI HAPA HAMNA HATA REF,SECT,AU HATA ARTICLE ZA CONTRACTS HAMNA HATA CASEPRESEDENT HAWA WANATANIA SOMA HUU UPUPU HAPA UNIAMBIE UNA NAFASI GANI KWENYE ILE HUKUMU YA DOWANS

UPUPU WA WANAHARAKATI;


1: Kwamba Bodi ya Zabuni ya Tanesco (TTB) ilikuwa na watalaam weledi katika kufanya kazi ya kuchambua zabuni, na kwa hakika huko nyuma ilikwisha kufanya kazi nyingine nyingi. Kwa maana hiyo kama kulikuwa na wasiwasi juu ya uwezo wa TTB katika suala zima la mkataba wa Richmond, basi ingebidi kupitia zabuni zote za huko nyuma na si wa Richmond pekee;
2: Kwamba kamati iliyoundwa na Wizara ya Nishati na Madini kupitia mchakato wa kufungwa kwa mkataba wa Tanesco na Richmond iliundwa nje ya utaratibu wa Sheria ya Ununuzi wa Umma (PPA);
3: Kwamba Tanesco ilishughulikia vilivyo zabuni ya Richmond kitaalam na kufikia hitimisho kuwa kampuni hiyo, haikuwa na uwezo wa kitaalam wala wa kifedha kufanya kazi hiyo. Richmond haikuwa na historia (rekodi) ya kufanya kazi kama hiyo walioyokuwa wameomba kama moja ya sharti mojawapo la msingi la kupata zabuni hiyo ambalo liliwekwa kwenye tangazo la kuomba kazi kama hiyo (kuzalisha umeme) na angalau kuwa na mtaji wa Dola za Marekani milioni tano (wakati huo Sh. bilioni tano).
4: Kwamba hata pale kazi ya kutafuta mzabuni wa kufanya kazi ya kuzalisha umeme megawati 100 ilipochukuliwa na Wizara ya Nishati na Madini, haikufanywa na Bodi ya Zabuni ya wizara hiyo, kitu ambacho ni kinyume kabisa na sheria ya PPA.
5: Kitu pekee kilichorejesha mchakato wa zabuni hiyo kwa Tanesco ni kutafutwa kwa saini ya kiongozi wa Tanesco ambaye hata hivyo alilazimishwa kusaini baada ya kuambiwa kwamba kama akikataa kitu chochote kingeweza kumpata;
6: Kwa maana hii basi, mchakato wote ambao uliishia kuipa Richmond kazi ya kufua umeme wa megawati 100, ulifanyika bila kuitishwa kwa zabuni kwa mujibu wa sheria ya PPA, lakini pia bila kushirikisha mamlaka zozote ambazo kisheria zinawajibu wa kushughulikia zabuni hizo, yaani Bodi ya Zabuni ya Wizara au Bodi ya Zabuni ya Tanesco (TTB);
7: Kwamba uchunguzi wa Kamati teule ya Bunge na ule wa Mamlaka ya Manunuzi ya Umma (PPRA), uligundua kuwa Richmond haikuwa ni kampuni iliyosajilia kama jina lake lilivyokuwa linasema na hata jina la RDEVCO LLC ambalo pia Richmond ilikuwa inajitambulisha kwalo, ilikuwa ni kampuni nyingine tofauti kabisa na Richmond iliyoomba kazi ya kufua umeme nchini;
8: Kwamba Richmond ilitoa anwani sawa na ile ya RDEVCO, lakini ofisi zao zilipotembelea na Kamati ya Bunge, iligundulika kwamba (RDEVCO) haikuwahi kufanya shughuli yoyote ya kuzalisha umeme kwa kutumia gesi asilia na kwa maana hiyo haikuwa na ujuzi wala fedha za kuweza kutekeleza kazi hiyo iliyoomba;
9: Kwamba TTB yaani Bodi ya Zabuni ya Tanesco ilikuwa sahihi kabisa kwa kutupilia mbali maombi ya Richmond katika kutekeleza kazi hiyo, kwa kuwa haikuwa na uwezo na haikukidhi masharti ya tangazo la zabuni la kazi ya kuzalisha umeme wa dharura wa megawati 100;
10: Kwamba Wizara ya Niashati na Madini iliishinikiza TTB na Bodi ya Tanesco kuvunja sheria kwa kupunguza siku za kutangaza zabuni kutoka 45 hadi 20; lakini utarartibu unaokubalika na PPA wa ama kutafuta kampuni ya kimataifa (International Shopping au Single sourcing) ukiwekwa kando, kwa kuwa katika utaratibu huu Tanesco ingewajibika kutafuta kampuni yenye historia ya kufanya kazi ya kuzalisha umeme wa dharura ambayo Richmond moja kwa moja isingefikiriwa kwa kuwa ilikwisha kujuliakana haina uwezo;
11: Wizara ya Nishati na Madini ililazimisha Tanesco na Bodi ya Tanesco ibadili zabuni iliyokataliwa yaani Richmond kuwa iliyokubaliwa licha ya kuwepo kwa vigezo vya dhahiri kabisa, kitaalam na uwezo wa fedha, ambavyo vilikuwa vimekwisha kumweka kando Richmond; kwa kufanya hivyo sheria ya PPA ilivunjwa;
12: Kwamba kamati iliyoundwa na Wizara ya Nishati na Madini kushughulikia zabuni ya Richmond, haikuwa na mamlaka ya kufanya kazi hiyo, ilivunja sheria ya PPA hata kama ilikuwa imechukua wataalam kutoka Tanesco na Wizarani.
13: Kwamba kamati hiyo, yaani ya wizara, ilifanya mchakato wa zabuni wa kufufua umeme wa megawati 100 ambao ushindi alipewa Richmond, kwa kutumia nyaraka ambazo Bodi ya Zabuni ya Tanesco ilikwisha kuzifuta kwa kuwa Richmond ilishindwa kutumiza matakwa ya tangazo la zabuni;
14: Kwamba Richmond aliruhusiwa kuwasilisha nyaraka nyingine za ziada kwenye kamati ya Wizara, ambazo hazikuwa kwenye zabuni iliyotangazwa Februari 27, 2006 na kisha Richmond ikashindwa; kwa kifupi kulikuwa na utaratibu wa makusudi wa kuhakikisha Richmond inashinda;
15: Kwamba wakati Richmond ilisajili jina la RDEVCO LLC Machi 2008 hii ilikuwa ni baada ya matukio mawili, kwanza baada ya kuwa imekwisha kuingia mkataba na Tanesco Juni 23, 2006 kwa bosi wa Tanesco kutishwa ili asaini, lakini pia baada ya Dowans kuwa amekwisha kuchukua mkataba huo; Lakini pia jina hilo halikusajiliwa kwenye mkataba wa kuzalisha umeme wa dharura uliofikiwa Juni 23, 2006.
16: Kwamba Mamlaka ya Manunuzi ya Umma (PPRA) ilithibitisha pasi na shaka yoyote kwamba mchakato wa ufungaji wa mkataba wa Richmond na Tanesco ulikiuka sheria ya manunuzi ya umma;
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…