Kuna wakati ni vizuri kutokuandika chochote, huu ni zaidi ya upuuzi, kuanzisha vikundi vya uharamia unasema ni uana mapinduzi! Na unaona njia sahihi, kwa hiyo unaamini kama ndiye aliyemuua padri basi yuko sahihi, maana aliongea hadharani, Ushabiki ukizidi unatutoa akili..
Lugha ya mkosa hoja ni hiyo hapo kwenye red. Nimetoa maoni yangu ya awali kwa mujibu wa video ambayo iliwekwa kuhusu huyu jamaa akihamasisha mapinduzi katka nchi yake anayoipenda. Kwenye ile video hakuna neno wala picha ya padri yoyote, na nilitegemea maoni yatokane na ile video.
Kwanza kabisa mimi sijui uhusiano wa huyu mtu na kifo cha padri mushi, na siwezi kukubali kuuawa kwa mtu yeyote yule awe padri mushi au sheikh ilunga. Kumtandika mtu risasi ni ugaidi. Alichokisema huyu brazamen kwenye ile video yake ni uanamapinduzi.
Naomba nikupe somo dogo tuu.
1. Serikali ya uingereza ilimwita general Washington gaidi wakati Marekani inapigania uhuru wake dhidi ya utawala wa uingereza.
2. Uingereza na marekani walimwita Mandela gaidi kwa sababu hizohizo.
3. Jomo Kenyatta na wakenya wenzake (sipendi kutumia neno mau mau) waliitwa magaidi wakati wakipigania uhuru wao.
Sasa hili neno gaidi ni neno "subjective", na gaidi wako wewe anaweza kuwa mpigania uhuru wa mtu mwingine.
Kwa mujibu wa hiyo video hapo juu, hakuna ugaidi hapo, bali ni uanamapinduzi.
Lakini kwa kuwa tuna elimu za viwango tofauti, kwa hiyo umuhimu wa "evidence" nao pia ni tofauti kutoka mtu mmoja mpaka mtu mwingine.