Dotto Bulendu: Maoni yangu kuhusu tume ya kuchunguza mchango wa sekta ya madini nchini

GANG MO

JF-Expert Member
Dec 6, 2016
2,092
2,210
Rais Magufuli kaunda tume ya kuchunguza mchango wa sekta ya madini nchini Tanzania,anataka kuona kama kuna ukweli kwenye hii biashara ya madini!.

Rais Magufuli tunakupongeza kwa kuonesha nia ya kuondosha uzania usio sawa kwenye biashara hii ya madini kati yetu na wawekezaji katika sekta hii ya madini nchini!.

Binafsi siwezi kuipongeza serikali kwa kuunda tume ama kwa maneno kutoka kwenye kinywa cha Mh Rais juu ya biashara hii ya madini!.

Suala la tume si jipya,kila serikali inapoingia imekuwa inakuja na maneno makali ya kuonesha kukerwa na biashara isiyo na uzania kwenye sekta ya madini!.

Serikali ya awamu ya tatu ilitoka na ripoti nzuri ya kamati iliyokuwa chini ya Jaji Mstaafu Mark Bomani,ripoti hii imeeleza kinagaubaga juu ya biashara hii ya madini,imeonesha jinsi tunavyoibiwa na nini cha kufanya!.

Serikali ya awamu ya nne nayo ilikuja na kamati yake iliyoitwa kamati ya Masha,nasikia katika ripoti nzuri zenye kuainisha ukweli kuhusu sekta ya madini na hii ni miongoni mwao,Masha na timu yake walipo maliza kazi yao,walikabidhi serikalini na haijawahi somwa,imewekwa sijui wapi!.

Nani anakumbuka hotuba ya Rais mstaafu Jakaya Kikwete trh 5.2.2006 mkoani Shinyanga,Rais Kikwete alitoa hotuba ya kusisimua akionesha kukerwa na uwekezaji kwenye sekta ya madini na kuahidi kupitia upya mikataba yote ili watanzania wanifaike na biashara hii!.

Mwaka 2009 tukatunga sera ya madini na baadae mwaka 2010 sheria yake ikatungwa,hizi nyaraka mbili zilizotungwa na wataalam kutoka serikalini ndiyo zinazotoa ruhusa huo mchanga kwenda nje,hili limerihusiwa kisera,hawa watu hawafanyi biashara kinyume na sheria wala sera!.

TEIT wamekuwa wanatoa taarifa juu ya mapato kutoka sekta hii ya madini,kumekuwa na ubabaishaji mkubwa,leo hesabi zilizopo TRA,TMAA,na wizarani kihusu mchango wa wawekezaji kwenye GDP,hazifanani kabisa,haya mambo hayafanyiki kwa siri!.

Tanzania tumekuwa tunafanya mambo unabaki kujiuliza hivi tumekutwa na nini?Tulianza kuvuna gesi bila uwepo wa sera na sheria ya gesi,hili ni jambo la ajabu kabisa!.

Hawa wawekezaji hawa,wamepewa kibuti na wataalam wetu kutuibia,nakumbuka mwekezaji kutoka Nyamongo alichimba madini bila kuilipa halmashauri ya Tarime mapato kwa muda mrefu,wameanza kulipa miaka mitatu kama iliyopita!

Nakumbuka nilikuwepo kwenye mkutano wa kuarifu Acacia kuanza kulipa mapato,Mkuu wa Acacia akasema walikuwa hawalipi kwa sababu halmashauri ilikuwa haijatunga sheria inayosimamia ulipaji wa mapato!.

Nikajiuliza hivi hii nchi haina wataalam,haina watu wenye maoni?,nakumbuka wakati wa uhai wake Marehemu Chacha Wangwe alilazikisha mgodi kulipa karo za wanafunzi wote wa jimboni kwake!.

Marehemu Wangwe alifanikiwa,baadhi ya vijana walikuwa wanapata ada mpaka za vyuo vikuu kutoka mgodini,hii hakiwa sehemu ya sera kutoka serikalini,ilikuwa
ni nguvu ya Marehemu Wangwe na wenzake!.

Kuna ripoti nyingine iliyopewa jina la "The gorden opportunity,nayo imeainisha wizi wote kwenye sekta ya madini nchini Tanzania,kuna wizi mkubwa kwenye mapato!wawekezaji hawa wamekuwa hawatoi taarifa za ukweli kwa serikali!.

Wawekezaji hawa,wameua watu kwa Risasi,wamewafanya watu walemavu,huko Nyamongo watu walibabuka ngozi,malipo ya fidia yamefanyika kinyonyaji!.

Unajiuliza hivi tunaunda kamati za kazi gani?kweli biashara hii inafanyika muda wote huu,idara ya usalama wa Taifa (TISS)haijui chochote,hivi ninkweli TISS hawafahamu chochote kuhusu biashara hii?

Ni matarajio yangu Rais Magufuli hatakuwa kama watangulizi wake,waliounda kamati na kuishia kuziweka ripoti kabatini!.

Binafsi nina imani kubwa Rais Magufuli atamaliza huu unyonge wa nchi yetu mbeke ya wawekezaji,mwaka mmoja nilifuatana na viongozi wa dini waliokuwa wanakwenda kutembelea na kujionea hali ya uwekezaji,nilisikitishwa na kilichowakuta viongozi hao,maaskofu,mashehe walijibiwa kwa dharau na hata kuzuiliwa kuongia mgodini!.

Leo kuna wafanyakazi wa mgodini wanahangaika huko Kahama,afya zao ni dhaifu kutokana na kazi za mgodini!.

Mishahara kati ta wazawa na wageni ni mbingu na ardhi huko migodini!.
 
Tatizo kubwa ni kwamba..
1/Rais alianza kuyaingilia haya mambo kabla ya kuundwa tume, hivyo sidhani kama tume una ujasiri wowote wa kuchunguza na kuja repoti tofauti na kile ambacho rais alishaonyesha msimamo wake...

2/Rais alishawahi kutamka na kujitamba kuwa serikali yake haitakuwa ya Tume au kamati za kuchunguza kwa sababu ni kupoteza muda na pesa za Tanzania, ghafla ameamua kualamba matapishi yake hadharani bila aibu kwa kutamka kuwa ataunda Kamati kama tatu hivi, ya kwanza ni Wanasayansi(Ndio hii tayari), ya pili ni Wanasheria na nyingine ya wataalamu wa biashara, uchumi na usalama. Bado sijaona mantiki yake.
Angeweza kuunda kamati moja sasa yenye watu tofauti tofauti ikiwa na Agenda zote tatu(Sayansi, Sheria na Biashara) ili waje na kitu kilichokamilika na kuufunga mjadala huu.
 
Natamani kulia ila naona aibu nimekaa na watoto ila kiukweli inatia hasira sana ngoja tumuombee kwa hili anaonekana hanunuliki kama watanguliz wake japo hapangiwi pia
 
Tatizo kubwa ni kwamba..
1/Rais alianza kuyaingilia haya mambo kabla ya kuundwa tume, hivyo sidhani kama tume una ujasiri wowote wa kuchunguza na kuja repoti tofauti na kile ambacho rais alishaonyesha msimamo wake...

2/Rais alishawahi kutamka na kujitamba kuwa serikali yake haitakuwa ya Tume au kamati za kuchunguza kwa sababu ni kupoteza muda na pesa za Tanzania, ghafla ameamua kualamba matapishi yake hadharani bila aibu kwa kutamka kuwa ataunda Kamati kama tatu hivi, ya kwanza ni Wanasayansi(Ndio hii tayari), ya pili ni Wanasheria na nyingine ya wataalamu wa biashara, uchumi na usalama. Bado sijaona mantiki yake.
Angeweza kuunda kamati moja sasa yenye watu tofauti tofauti ikiwa na Agenda zote tatu(Sayansi, Sheria na Biashara) ili waje na kitu kilichokamilika na kuufunga mjadala huu.
maoni mazuri mdau
 
Kwa nini asizifanyie kazi repoti ya tume zilizopita au zilichomwa? Rais wangu nakukubali sana. Ila.nikumbuka Bashite naishiwa nguvu. Any way let us see
 
Rais alishawahi kutamka na kujitamba kuwa serikali yake haitakuwa ya Tume au kamati za kuchunguza kwa sababu ni kupoteza muda na pesa za Tanzania.
Kuna watu tangu jana katika kutetea kubadili misimamo kwa Rais wanakuja na hoja kwamba "wanasiasa wote ni waongo" wakati mwenyewe anajiita mpenzi wa mungu kwa kuwa anasema kweli kila wakati.


Angeweza kuunda kamati moja sasa yenye watu tofauti tofauti ikiwa na Agenda zote tatu(Sayansi, Sheria na Biashara) ili waje na kitu kilichokamilika na kuufunga mjadala huu.
Kuwa na mantiki kunahitaji utulivu wa akili na siyo akili za kukurupuka. Kuna magogo yanayotumika kama nguzo na shirika la Umeme Tanzania, yananunuliwa Mafinga mkoani Iringa yanapelekwa Dar kwenye ghala na kusafirishwa tena mpaka Songea Mkoani Ruvuma kwa matumizi. Kimantiki kwa nini yasingetoka Iringa na kwenda Songea moja kwa moja badala ya kupelekwa Dar kwanza?

Zanzibar-ASP Usihoji namna hii wenyewe hawapendi!!
 
Natamani kulia ila naona aibu nimekaa na watoto ila kiukweli inatia hasira sana ngoja tumuombee kwa hili anaonekana hanunuliki kama watanguliz wake japo hapangiwi pia
inauma sana
 
Kuna watu tangu jana katika kutetea kubadili misimamo kwa Rais wanakuja na hoja kwamba "wanasiasa wote ni waongo" wakati mwenyewe anajiita mpenzi wa mungu kwa kuwa anasema kweli kila wakati.


Kuwa na mantiki kunahitaji utulivu wa akili na siyo akili za kukurupuka. Kuna magogo yanayotumika kama nguzo na shirika la Umeme Tanzania, yananunuliwa Mafinga mkoani Iringa yanapelekwa Dar kwenye ghala na kusafirishwa tena mpaka Songea Mkoani Ruvuma kwa matumizi. Kimantiki kwa nini yasingetoka Iringa na kwenda Songea moja kwa moja badala ya kupelekwa Dar kwanza?

Zanzibar-ASP Usihoji namna hii wenyewe hawapendi!!
kaka hapo kwenye magogo umenichekesha sana. kwel tz ni nchi ya ajabu sana
 
Ngoja tusubiri tume ifanye kazi!
Ingawa alikuwa anapinga mambo ya uundwaji tume kwenye hii awamu yake!
Cha kushangaza hilo sakata la mchanga zimeundwa tume tatu kwa mpigo!
 
kaka hapo kwenye magogo umenichekesha sana. kwel tz ni nchi ya ajabu sana
Jana nilikuwa nimejumuika na jamaa zangu maeneo ya Igumbilo hapa Iringa nikaona magari kadhaa yakiwa yamebeba nguzo toka Mafinga yakielekea Dar na mengine yanatoka Dar yanaelekea Songea. Hii nchi walaji mshipa wa aibu na woga ulishawakatika kitambo sana!!
 
Rais Magufuli kaunda tume ya kuchunguza mchango wa sekta ya madini nchini Tanzania,anataka kuona kama kuna ukweli kwenye hii biashara ya madini!.

Rais Magufuli tunakupongeza kwa kuonesha nia ya kuondosha uzania usio sawa kwenye biashara hii ya madini kati yetu na wawekezaji katika sekta hii ya madini nchini!.

Binafsi siwezi kuipongeza serikali kwa kuunda tume ama kwa maneno kutoka kwenye kinywa cha Mh Rais juu ya biashara hii ya madini!.

Suala la tume si jipya,kila serikali inapoingia imekuwa inakuja na maneno makali ya kuonesha kukerwa na biashara isiyo na uzania kwenye sekta ya madini!.

Serikali ya awamu ya tatu ilitoka na ripoti nzuri ya kamati iliyokuwa chini ya Jaji Mstaafu Mark Bomani,ripoti hii imeeleza kinagaubaga juu ya biashara hii ya madini,imeonesha jinsi tunavyoibiwa na nini cha kufanya!.

Serikali ya awamu ya nne nayo ilikuja na kamati yake iliyoitwa kamati ya Masha,nasikia katika ripoti nzuri zenye kuainisha ukweli kuhusu sekta ya madini na hii ni miongoni mwao,Masha na timu yake walipo maliza kazi yao,walikabidhi serikalini na haijawahi somwa,imewekwa sijui wapi!.

Nani anakumbuka hotuba ya Rais mstaafu Jakaya Kikwete trh 5.2.2006 mkoani Shinyanga,Rais Kikwete alitoa hotuba ya kusisimua akionesha kukerwa na uwekezaji kwenye sekta ya madini na kuahidi kupitia upya mikataba yote ili watanzania wanifaike na biashara hii!.

Mwaka 2009 tukatunga sera ya madini na baadae mwaka 2010 sheria yake ikatungwa,hizi nyaraka mbili zilizotungwa na wataalam kutoka serikalini ndiyo zinazotoa ruhusa huo mchanga kwenda nje,hili limerihusiwa kisera,hawa watu hawafanyi biashara kinyume na sheria wala sera!.

TEIT wamekuwa wanatoa taarifa juu ya mapato kutoka sekta hii ya madini,kumekuwa na ubabaishaji mkubwa,leo hesabi zilizopo TRA,TMAA,na wizarani kihusu mchango wa wawekezaji kwenye GDP,hazifanani kabisa,haya mambo hayafanyiki kwa siri!.

Tanzania tumekuwa tunafanya mambo unabaki kujiuliza hivi tumekutwa na nini?Tulianza kuvuna gesi bila uwepo wa sera na sheria ya gesi,hili ni jambo la ajabu kabisa!.

Hawa wawekezaji hawa,wamepewa kibuti na wataalam wetu kutuibia,nakumbuka mwekezaji kutoka Nyamongo alichimba madini bila kuilipa halmashauri ya Tarime mapato kwa muda mrefu,wameanza kulipa miaka mitatu kama iliyopita!

Nakumbuka nilikuwepo kwenye mkutano wa kuarifu Acacia kuanza kulipa mapato,Mkuu wa Acacia akasema walikuwa hawalipi kwa sababu halmashauri ilikuwa haijatunga sheria inayosimamia ulipaji wa mapato!.

Nikajiuliza hivi hii nchi haina wataalam,haina watu wenye maoni?,nakumbuka wakati wa uhai wake Marehemu Chacha Wangwe alilazikisha mgodi kulipa karo za wanafunzi wote wa jimboni kwake!.

Marehemu Wangwe alifanikiwa,baadhi ya vijana walikuwa wanapata ada mpaka za vyuo vikuu kutoka mgodini,hii hakiwa sehemu ya sera kutoka serikalini,ilikuwa
ni nguvu ya Marehemu Wangwe na wenzake!.

Kuna ripoti nyingine iliyopewa jina la "The gorden opportunity,nayo imeainisha wizi wote kwenye sekta ya madini nchini Tanzania,kuna wizi mkubwa kwenye mapato!wawekezaji hawa wamekuwa hawatoi taarifa za ukweli kwa serikali!.

Wawekezaji hawa,wameua watu kwa Risasi,wamewafanya watu walemavu,huko Nyamongo watu walibabuka ngozi,malipo ya fidia yamefanyika kinyonyaji!.

Unajiuliza hivi tunaunda kamati za kazi gani?kweli biashara hii inafanyika muda wote huu,idara ya usalama wa Taifa (TISS)haijui chochote,hivi ninkweli TISS hawafahamu chochote kuhusu biashara hii?

Ni matarajio yangu Rais Magufuli hatakuwa kama watangulizi wake,waliounda kamati na kuishia kuziweka ripoti kabatini!.

Binafsi nina imani kubwa Rais Magufuli atamaliza huu unyonge wa nchi yetu mbeke ya wawekezaji,mwaka mmoja nilifuatana na viongozi wa dini waliokuwa wanakwenda kutembelea na kujionea hali ya uwekezaji,nilisikitishwa na kilichowakuta viongozi hao,maaskofu,mashehe walijibiwa kwa dharau na hata kuzuiliwa kuongia mgodini!.

Leo kuna wafanyakazi wa mgodini wanahangaika huko Kahama,afya zao ni dhaifu kutokana na kazi za mgodini!.

Mishahara kati ta wazawa na wageni ni mbingu na ardhi huko migodini!.
Well said
 
Jana nilikuwa nimejumuika na jamaa zangu maeneo ya Igumbilo hapa Iringa nikaona magari kadhaa yakiwa yamebeba nguzo toka Mafinga yakielekea Dar na mengine yanatoka Dar yanaelekea Songea. Hii nchi walaji mshipa wa aibu na woga ulishawakatika kitambo sana!!
kaka ukiona miundombinu ambako yanatoka hayo magogo, karatasi, mbao na majani ya chai utashangaa sana. we are not serious
 
Nachofahamu matokeo ya hiyo tume hayatakuja kama anayotaka Mh.Pombe,

Atachukizwa na matokeo ya hii tume kama Majaliwa alivyochukizwa na matokeo ya kupotea kwa Faru John.
 
Alipowekwa Muhongo pale nishati na madini watu wakapata matumaini makubwa sababu eti ni mbobezi na msomi mahiri wa miamba,wazungu wanamtumia and so and so, but I tell you Muhongo hajaleta kitu kipya hapo zaidi ni kuendeleza business as usual na mbaya zaidi Muhongo amekuwa mwanasiasa zaidi kuliko wanasiasa aliowakuta. Muhongo alitakiwa ang'oke tangu ile issue ya mita ya mafuta pale bandarini but politically aka survive na bado ile ya Mramba wa tanesco aka survive pia kwa kumtoa chambo Mramba. They guy is smart ass
 
Mimi nilipongeza uamuzi huu Kuzuia Mchanga wa Dhahabu, Magufuli Anastahili Pongezi. Tusiishie Kwenye Madini Tuu na Gesi Jee?!.

Tanzania tunaibiwa kwenye madini kwa sababu we don't know how. Vivyo hivyo na kwenye gesi pia tunaibiwa! . Hivyo nimependekeza tusisubiri hadi miaka 20 ijayo ndipo tujue tunaibiwa hivyo nimependekeza tusiishie kwenye madini tuu bali twende hadi kwenye gesi.
Gesi asili: Is it "day light robbery?!" Watanzania tunaibiwa mchana kweupe!

Paskali
Ndio maana naichukia CCM na hata hii CCM ya Magu nayo naona haina hata uhalali wa kuchunguza hii mikataba bali wanastahili kuwa jela maana baadhi yao ni sehemu ya huu wizi kwa kupitisha sheria hizi Bungeni na wengine kwa kuwa wajumbe wa mabara ya mawaziri waliobariki huu wizi.

Kwakweli inanikera sana kuona watu walioshiriki kupitisha sheria hizi mbovu na mikataba hii ya kinyonyaji eti leo ndio wanajidai kushituka na kuunda Tume.

Hii ni hadaa na inakera sana.
 
Tusubiri matokeo ya wataalam.. Kafumu Alisha mwaga yake yakitaalam humuhumu.. Naye Lissu akaja na yakisheria..
Sisi wengine tusubiri matokeo ndio tujadili.. Sasa hivi tunajitia hasira za buree kabisa..
 
Back
Top Bottom