GE2025 Dorothy Semu: Vyombo vya Usalama visitumike tena kutumbukiza kura 'fake' kwenye masanduku kama Chaguzi zilizopita

GE2025 Dorothy Semu: Vyombo vya Usalama visitumike tena kutumbukiza kura 'fake' kwenye masanduku kama Chaguzi zilizopita

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

DuaZaMama

JF-Expert Member
Joined
Jun 2, 2025
Posts
1,882
Reaction score
4,129
Kiongozi wa ACT Wazalendo, Bi. Dorothy Semu, ametoa kauli kali akilaani kile alichokiita matumizi mabaya ya vyombo vya usalama na Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika chaguzi zilizopita.

Akihutubia mkutano wa hadhara Julai 5, 2025 katika eneo la Sapiwi, Jimbo la Bariadi Vijijini, Semu alisema:

“Chaguzi zetu zilizopita—Uchaguzi wa 2020 na Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024—ziligubikwa na kura feki. Aidha, vyombo vya usalama vimekuwa vikitumika na CCM. Hatutaki vyombo hivyo vitumike tena.”

Semu alisisitiza kuwa ili uchaguzi wa mwaka 2025 uwe wa haki na huru, ni lazima vyombo vya dola viwe huru na visivyopendelea upande wowote wa kisiasa. Alisema kuwa wananchi wa Tanzania wanahitaji mabadiliko ya kweli, ambayo hayawezi kufikiwa iwapo taasisi za usalama zitaendelea kutumiwa kama silaha za kisiasa.

Kauli yake inakuja wakati ambapo vyama vya upinzani vimekuwa vikiendelea kutoa wito wa mageuzi ya mfumo wa uchaguzi na usimamizi wa haki ya kupiga kura.

 
Sasa huyu nae sijui tumweteje, kwa hiyo katika chaguzi alizozitaja ni kipi kimebadilika kama sio kutafuta uteuzi wa U RC, tuache na maisha yetu nyie endeleeni kupoteza muda wenu kwa sababu inaonekana hamna cha kufanya.
Kwa kanuni ipi mpate hata diwani mmoja labda mpewe kama asante kwa kushiriki
 
Kiongozi wa chama cha ACT Wazalendo, Dorothy Semu amesema "Chaguzi zetu zilizopita—Uchaguzi wa 2020 na Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024—ziligubikwa na kura feki. Aidha, vyombo vya usalama vimekuwa vikitumika na CCM. Hatutaki vyombo hivyo vitumike tena!"

 
2020
Kura za kumchagua magufuli na kina ponjolo zilipigwa siku 2 kabla ya tarehe ya uchaguzi .zoezi nililishuhudia pale ccm mkwajuni
 
Kiongozi wa chama cha ACT Wazalendo, Dorothy Semu amesema "Chaguzi zetu zilizopita—Uchaguzi wa 2020 na Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024—ziligubikwa na kura feki. Aidha, vyombo vya usalama vimekuwa vikitumika na CCM. Hatutaki vyombo hivyo vitumike tena!"

Huyu ni miongoni mwa wakina mama wajinga na ovyo kabisa.
Anaongea bila kushirikisha ubongo.
 
Mawakala wa ccm hao ! Hawako serious kama wanavyotaka kuwaaminisha
 
Wizi wa kura kawaida kama wizi wa mitihqni wa makonda??
Shujaa aliingia deal na Sauti ya Zege 2020 kwamba amwachie jimbo mkono wa sweta then yeye atatimba bungeni kwa viti maalum

Kisha Sauti ya Zege na Slow Slow wakavuta mpunga kwa wale Covid wengine 18 😂 Slow Slow akanunua Yutong na Sauti ya Zege akavuta Vogue

Siasa ni sayansi miaka 20 mmekaa na Mwamba bila kujua ni nani 😂😂😂😂
 
Shujaa aliingia deal na Sauti ya Zege 2020 kwamba amwachie jimbo mkono wa sweta then yeye atatimba bungeni kwa viti maalum

Kisha Sauti ya Zege na Slow Slow wakavuta mpunga kwa wale Covid wengine 18 😂 Slow Slow akanunua Yutong na Sauti ya Zege akavuta Vogue

Siasa ni sayansi miaka 20 mmekaa na Mwamba bila kujua ni nani 😂😂😂😂
Sauti ya zege na wenzake waliapishiwa grreji pale mjrngoni.
Aliyewaapisha akaahidi kuwalinda kukikomoa chama . Alisahau
Shujaa aliingia deal na Sauti ya Zege 2020 kwamba amwachie jimbo mkono wa sweta then yeye atatimba bungeni kwa viti maalum

Kisha Sauti ya Zege na Slow Slow wakavuta mpunga kwa wale Covid wengine 18 😂 Slow Slow akanunua Yutong na Sauti ya Zege akavuta Vogue

Siasa ni sayansi miaka 20 mmekaa na Mwamba bila kujua ni nani 😂😂😂😂
Damage aliyoiacha huyo anayeitwa shujaa kwa taifa hili ni kubwa sana na itachukua muda mrefu sana kuimaliza
Tuendelee kujifariji tu hapa
 
Kiongozi wa ACT Wazalendo, Bi. Dorothy Semu, ametoa kauli kali akilaani kile alichokiita matumizi mabaya ya vyombo vya usalama na Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika chaguzi zilizopita.

Akihutubia mkutano wa hadhara Julai 5, 2025 katika eneo la Sapiwi, Jimbo la Bariadi Vijijini, Semu alisema:

“Chaguzi zetu zilizopita—Uchaguzi wa 2020 na Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024—ziligubikwa na kura feki. Aidha, vyombo vya usalama vimekuwa vikitumika na CCM. Hatutaki vyombo hivyo vitumike tena.”

Semu alisisitiza kuwa ili uchaguzi wa mwaka 2025 uwe wa haki na huru, ni lazima vyombo vya dola viwe huru na visivyopendelea upande wowote wa kisiasa. Alisema kuwa wananchi wa Tanzania wanahitaji mabadiliko ya kweli, ambayo hayawezi kufikiwa iwapo taasisi za usalama zitaendelea kutumiwa kama silaha za kisiasa.

Kauli yake inakuja wakati ambapo vyama vya upinzani vimekuwa vikiendelea kutoa wito wa mageuzi ya mfumo wa uchaguzi na usimamizi wa haki ya kupiga kura.
Kaongea ndio je ndo dawa,ACT wanatakiwa kuacha siasa za maji taka
 
Back
Top Bottom