Dongo la Mbatia kwa Dr. Tulia!

Tulia kaingizwa juzi kwenye siasa, na wala hatafika popote kwenye siasa.
Mwisho wa safari yake upo karibu sana maana kashindwa kujiongeza, ukibebwa shikilia sasa yeye kabebwa anajiachia mikono ina cheza tu
 
Yaani hawa Lumumba ni viazi. ngoja watatoroka humu mmoja mmoja kwa kukosa bk7 magufuli akiwa M/kiti wa ccm
 
Ndani ya ukawa hakuna wabunge wanaopigania matumbo yao,wabunge wa ukawa kwanza huo ubunge wameupata kwa uhalai na mbinde kwa kushindana na wagombea wa ccm wenye hila na vitisho,sisi wananchi tulio wachagua ndio tunawaamini
 
KARIBU SANA JF
 
Maisha hayana cross multiplication ndugu.... kwa umri wako kuna wanao kuzidi cheo na madaraka mno tu... ni suala la chance tu.....
Mkuu wala husipoteze nguvu zako nyingi kujadili wala kujibu point za huyu mtu,yeye kamezeshwa cd ya kuitetea ccm na wana ccm wote wanao itetea ccm
 

Tulia kaanza juzi au kaanzishwa juzi! Tofautisha mtoto aliyezaliwa na kukuta kwao kuna maghorofa na kukabidhiwa moja kama zawadi na baba yake na yule anayetafuta mwenyewe tena katika ya vikwazo lukuki. Hivi kwa akili yako Tulia ni mwanasiasa kweli au kawekwa tena hata wanaccm wenyewe walipigwa na butwaa siku anachukua fomu kwa sababu hawanaga uwezo wa kuhoji, basi imekuwa ilivyokuwa
 
Unajionyesha ulivyo mgeni wa siasa za ulimwengu na ni dhahili kuwa ndio kwanza umeanza kulijua bunge na shughuli zake kupitia tbc,kama hujui madhara na thamani ya wabunge wa upinzani kususia vikao vya bunge basi endelea kujifunza zaidi kupitia tbc usiku wa manane
 
kama kukaa muda mrefu kwenye siasa ndio hoja ya kuwa nguli wa siasa na kujua kila kitu basi inabidi timsikilize kingunge tu
 
Tulia mama, tumia Elimu yako kuonesha independence ya maamuzi. Unashusha hadhi ya Taaluma yako.
 
Yeye Tulia kateuliwa kuwa mbunge na kwa kuwa CCM ni wengi bungeni kapata Unaibu spika. Mbatia ni mkongwe kisiasa na mchango wake ni mkubwa. tena ni mwenyekiti wa chama
Hoja isiwe cheo bali mchango wa mtu. Phd si issue katika suala la uongozi.
 
Wewe kwako mafanikio kisiasa ni yapi ebu twambie,
Mfano: Mh, Mbowe huyu amepata mafanikio ya kisiasa, kutoka Chadema chama kilichokua kinaonekana kidogo kuliko NCCR, na kuwa chama kimbilio na watu wote wanaohitaji mabadiriko ya kisiasa, na uongozi wa dolla. NCCR ya mbatia yenyewe imetoka juu, na inatelemka chini, ilikuwa na watu ambao NCCR ingefanikiwa kushika dolla walikuwa wanatosha kuwa viongozi wa nchi. Kwamantiki hiyo Mh, Mbatia hajafanikiwa kisiasa.
 
Dua za ccm kamwe haziwezi kumpata mbatia
 
Dua za ccm kamwe haziwezi kumpata mbatia
Ni mtizamo wako, kamwe maishini mwangu sitokua mwanachama wa chama siasa, kura yangu kila ifikapo uchaguzi naweza wapigia watu watatu tofauti, kulingana nivyoona mimi anafaa, na sio chama chake.
 
Ni mtizamo wako, kamwe maishini mwangu sitokua mwanachama wa chama siasa, kura yangu kila ifikapo uchaguzi naweza wapigia watu watatu tofauti, kulingana nivyoona mimi anafaa, na sio chama chake.
Maajabu hayataisha duniani,nilini mgombea binafsi ameruhusiwa nchini tanzania?
 
Umemjibu vizuri sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…