Si kila mchawi au mshirikina ana uwezo wa kupaa...uchawi na ushirikina una level zake kama ilivyo kwenye viwango vya elimu
Mchawi anayejipendekeza kupaa bila kupata maarifa kamili hujikuta akipiga mweleka mkubwa sana kutokana na uzito wake au vinginevyo
Na huko angani kuna tufani za kila aina Usijaribu kupitisha helicopter yako kwenye anga la Boeing hutafika safari yako
Lakini pia kwenye kupaa kuna mahesabu yake...kwamba utapaa upande gani na umbali gani na urefu gani.kwamba kama unaenda Lamu kwa mwendo wa kawaida pengine ni masaa matatu hivi lakini wewe unataka kwenda kwa sekunde tatu tuu inabidi ujigawe roho na mwili yani unacheza kamari na Mungu
Kwahiyo unautanguliza mwili kwanza kisha ndio roho hufuata...vikishafika vyote salama huungana tena na kuwa binadamu kamili na kuendelea na mambo yake
Kupaa kwa ungo huo ni usafiri wa wengi kama daladala na ni usafiri wa kimaskini
Kupaa kwa fimbo huu ni advanced na usafiri binafsi sana sana unaweza kumpa lift mtu mmoja na hapa kuna majini yanahusika
Kusafiri kiroho hii ni level ya juu kabisa ambako kwenye uchawi huu huu hakuna time limit wala umbali yani ni kama dunia iko kiganjani mwako na ni kiasi cha kujisogeza tuu
Mshana somo hili linatundisha nini kaka?, si ulishastaafu!? napenda nimeet na wewe siku 1 kwani inaonyesha una nondo za kutosha kuhusu ulimwengu usionekana.