Kwa kweli ujana ni maji ya moto.....................Hii maneno ikikupata miaka hii, utaozea Segerea
Ha ha ha haaaaaaaaaaaaaaaaa...................... Kumbe bado mnalikumbuka eh!Stori imekaa ki-Jitambuejitambue fulani... How I miss that paper...
umeonaeeeeeee!!!!!!Ungeanza na kusema "Hadithi Hadithi hapo zamani 1989 palikuwa na mwalimu na mtoto mmoja ......" ningeelewa vizuri
Mzee mwenzangu salaam,
Yaani kila naposoma threads zako namkumbuka sana Marehemu Munga Tehenan (RIP) Mzee wa Jitambue. (Jitambue na jina lako Mtambuzi vinaendana endana.
Katika gazeti lake la jitambue kulikuwa na makala za "SIKU NILIYOFEDHEHEKA". Thread zako zinanirudishaga kwenye makala hizo.
Ha ha ha haaaaaaaaaaaaaaaaa...................... Kumbe bado mnalikumbuka eh!
Subiri mkuu tunajipanga kurudi upya, ngoja tukusanye Mikwanja.......................
Hiyo naikumbuka aisee........................................!huwa simsahau jamaa aliyehangaika na maisha saana na kuwa na mali nyingi lakini kwa kutegemea waganga wa kienyeji alikuja kufilisika. Akaendelea na waganga na masharti mbalimbali,hakuna alichofanikisha. Mwisho akasema hakuna mganga yeyote anayesema ukweli..
Mkuu mkiingia mtamboni upya tustuane, ntakuomba unipe kolamu yangu niwe narusha makala zangu pale. Nilikuwa mwanachama hai wa Jitambue na nllikuwa natuma michango yangu sana kule. Dah! Nimekumbuka mbali sana wakati nikiwa paparazi wa kujitolea wa magazeti ya Taifa Letu, Nipashe na Alasiri.Haswaaa................Ni kweli mkuu, mimi ni miongoni mwa waliokuwa waandishi wa gazeti lile, makala za siku niliyofedheheka ni mojawapo ya makala nilizoweka michango yangu. Ulikuwa ni ubunifu wa hali ya juu. Bado kuna matumaini ya kurudi tena katika sura mpya, lakini tunakwamishwa na vyanzo vya mitaji, lakini nia ipo sana ya kulirudisha gazeti lile pendwa.