Dodoma leo: Waraka wakusanywa

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Nov 25, 2010
6,135
17,802
Katika kile kinachoonekana kama kugonga mwamba kwa chama tawala (CCM) kusambaza Waraka wa Siri unaobeba Rasimu Mbadala ya Katiba mpya, chama hicho kimeamuru kukusanywa mara moja kwa Waraka huo ili asakwe aliyeuvujisha kabla. Chanzo cha kuaminika toka Makao Makuu ya CCM hapoa Dodoma kinasema kuwa CCM imetaharuki baada ya kugundua kuwa Waraka huo umeshawafikia hadi Wajumbe wapinzani.

'Mambo ni magumu kwetu. Leo umeona tulivyoangushwa kwenye 'kura ya wazi'. Sasa chama kinakusanya Waraka wake. Sina hakika kama huo ndio utakuwa mwisho wa udhibiti wa chama kwa Wajumbe wanaofungamana na chama kwakuwa Waraka huo ndio msimamo wa chama.' kilisema chanzo hicho

'Mambo ya msimamo ni magumu sana. Nadhani,chama kingeweka utaratibu wa kuelimisha Wajumbe taratibu hadi wajue kwanini CCM inasimamia mambo fulanifulani. Hii ya kulazimishana,itaiaibisha chama hapo mbeleni. Hakuna elimu yoyote itolewayo kwa wana-CCM waliopo hapa Dodoma zaidi ya kumezeshwa tu msimamo wa chama.' alisema Mjumbe mmoja wa Bunge la Katiba ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Mkoa wa Mara (CCM)

Siasa za chama changu hunishangaza sana. Waraka ulishasambaa na kusomwa. Itasaidia nini kuukusanya muda huu? Utakusanywaje?

Mzee Tupatupa wa Lumumba (sasa Dodoma)
 
Funny.jpg

Ongeza subira Nape... ndoo itajaa hiyo

Hata mtoto wa miezi sita ana akili kuliko vilaza wa CCM...
 
Hakika hila zina mwisho wake!! Nchi haiwezi kuendeshwa kwa ubabe na kutishiana kiasi hiki. Hii inafanya hadi watoa michango bungeni leo kutoka ccm wametoa kwa woga wakiogopa kuja kubanwa baadaye. Shame on you mlioandika waraka huo. Kuna member alisema angeuweka huo waraka hapa jana sijui imekuwaje tena. JF kitivo cha habari mmekosa waraka huu kweli?
.
 
Hakika hila zina mwisho wake!! Nchi haiwezi kuendeshwa kwa ubabe na kutishiana kiasi hiki. Hii inafanya hadi watoa michango bungeni leo kutoka ccm wametoa kwa woga wakiogopa kuja kubanwa baadaye. Shame on you mlioandika waraka huo. Kuna member alisema angeuweka huo waraka hapa jana sijui imekuwaje tena. JF kitivo cha habari mmekosa waraka huu kweli?
.


Huo waraka natamani uchanwe bungeni... mbele ya maCCM
 
Tatizo la CCM ni kutokutambua nyakati. Wawaache wabunge wao wawe huru katika mjadala na sio kuwamezesha maana watawaaibisha maana itaonekana kila mmoja anaunga alilolisema mwenzake. CCM watambue kuwa hizi nyakati za sayansi na Technolojia watu wanaona kila kitu kinachoendelea bungeni
 
hii mbinu ya kuukusanya waraka ili kubaini nani kaugawa itasababisha usambae haraka kuliko ilivyodhaniwa.


pole mzee tupatupa.
 
Haya wanakalenga, mmeona yanayoendelea huko bungeni, mkimchagua huyo mtoto wa marehemu Mgimwa, ataenda kufanya haya wanayofanya wabunge wenzie kule Dodoma, ccm ni mashetani.
 
Back
Top Bottom