Dodoma Leo: Kwani CCM, UKAWA mmejipangaje?

Dodoma Leo: Kwani CCM, UKAWA mmejipangaje?

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,004
Hatimaye leo, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dr. John Pombe Magufuli atalihutubia Bunge na kulizindua rasmi Bunge hili la 11. Kumekuwa na minong'ono isiyo na mfano kuhusu kitakachotokea leo ndani ya Bunge leo kabla,wakati na baada ya Rais Magufuli kuhutubia.

Wapo wanaosema huku wakihema kuwa UKAWA watatoka Bungeni. Wapo wanaosema kutwa nzima kuwa UKAWA watazomea au kupiga kelele zisizo na vigeregere. Wapo wanaosema na kutamani kuwaona UKAWA wakibaki na kumsikiliza Rais Magufuli akihutubia Bunge na kueleza mwelekeo wa nchi yetu kisiasa, kiuchumi,kijamii na kiutamaduni.

CCM wanasemwa kama walijipanga kushangilia na hata kulia kwa furaha isiyo na karaha wakati Rais akihutubia. Wanatajwa kama wenye furaha isiyo na kifani wala kupimwa kwenye mzani kabla, wakati na baada ya hotuba ya Rais Magufuli leo hapa Dodoma. Nami, kama kada wa CCM, nitaondoka hapa Dodoma baada ya Rais kuhutubia. Nami nimo.

Kusemwasemwa kote huku kunachagizwa, si kuigizwa, na mkwamo wa kikatiba huko Zanzibar. UKAWA hawatamani wala kutaka kumuona Rais Shein wa Zanzibar akiingia Bungeni kama Rais halali wa Zanzibar. CCM wanasema kuwa Rais Shein ni halali kwakuwa uchaguzi wa Zanzibar umefutwa na yeye Dr. Shein anabaki kuwa Rais hadi mpya achaguliwe.

Ni VUTA-NKUVUTE hapa Dodoma. Hali lakini iko shwari na hakuna yoyote tahadhari wala hatari. Kwani, CCM na UKAWA mmejipangaje? Leo, afe mkwezi au zipasuke nazi, mambo yatafanyika hapa!

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Dodoma)
 
Last edited by a moderator:
ni bora shein kutohudhuria ili mambo yaende sawa,mbali na hapo tutarajie patashika ndani ya bunge

nipo na wewe mkuu. japokuwa kwa AFRIKA HAIWEZEKANI. Tz-ni miongoni mwa nchi chache sana ambazo walioko madarakani wanawatambua wapinzani ni Kama maadui. Kumbe siyo maana yake, wapinzani ni wajibu wao kukosoa, na kupinga pale haki au sheria inapokiukwa.
 
Ni bora Shein kutohudhuria ili mambo yaende sawa,mbali na hapo tutarajie patashika ndani ya bunge

Nani amekudanganya!! UNYUMBU unaendelea !!!!! Dr Shein ni rais Halali wa Zanzibar na ataingia Bungeni.... Maalim seif OUT!!! Mkileta vurugu maji ya washa washa halali yenu... Tanzania bila UKAWA inawezekana!
 
Ni bora Shein kutohudhuria ili mambo yaende sawa,mbali na hapo tutarajie patashika ndani

Bunge linaongozwa na sheria,ukawa tusiwe malo.. na wapu...,tumedanganya mara ngapi?Mara ICJ,mara hataapishwa?lipi limetokea?Shein ataingia na mambo yataenda tuuu...,tusijifariji kwa mambo ya kipu....
 
nipo na wewe mkuu. Tz-ni miongoni mwa nchi chache sana ambazo walioko madarakani wanawatambua wapinzani ni Kama maadui. Kumbe siyo maana yake, wapinzani ni wajibu wao kukosoa, na kupinga pale haki au sheria inapokiukwa.

Wapinzani wamejipambanua kama wao ni maadui wa serikali...CCM walijitahidi katika kipindi kilichopita kuwakaribisha kundini kwa moyo mkunjufu... Raisi Kikwete....alitoa nafasi za ubunge kwa wanachama wa vyama vya upinzani....lakini angalia lugha na vijitabia vya hao watu waliopewa fursa hizo...wanaongoza kwa lugha za kejeli..... wapinzani walipewa hadi uongozi kwenye kamati za bunge... wapinzani walipewa nafasi ya kurekebisha Katiba iliyopo..... TUMEJIFUNZA KUTOKANA NA MAKOSA SASA TUNATAMBUA NIA NA LENGO ZA WAPINZANI KUWA NI MAADUI NA SISI TUNASEMA .....THIS TIME NI VITA NI VITA!!!
 
Jambo la msingi kabisa ni wabunge wote kujiuliza, nini faida na hasara ya ama zomeazomea au kutozomea hotuba ya rais. Wananchi wanataka kusikia zomeazomea au hotuba ya rais?
 
Wapinzani wamejipambanua kama wao ni maadui wa serikali...CCM walijitahidi katika kipindi kilichopita kuwakaribisha kundini kwa moyo mkunjufu... Raisi Kikwete....alitoa nafasi za ubunge kwa wanachama wa vyama vya upinzani....lakini angalia lugha na vijitabia vya hao watu waliopewa fursa hizo...wanaongoza kwa lugha za kejeli..... wapinzani walipewa hadi uongozi kwenye kamati za bunge... wapinzani walipewa nafasi ya kurekebisha Katiba iliyopo..... TUMEJIFUNZA KUTOKANA NA MAKOSA SASA TUNATAMBUA NIA NA LENGO ZA WAPINZANI KUWA NI MAADUI NA SISI TUNASEMA .....THIS TIME NI VITA NI VITA!!!

Wakati mabwana zako wamejifungia ndani wanafikiria njia za kuzuia aibu isitokee, wewe na wenzako mavuvuzela msio elewa nini kinaendelea mnaona sawa tuu kwa akili zenu hizo zisizo jaa hata kikombe cha chai.
Nyie ndio mnaipunguzia heshima CCM mpaka inaonekana imejaa mambumbumbu wengi wasio elewa maana ya Demokrasia ya vyama vingi na kudhani Taifa hili ni property ya ccm. Ndio nyie mnaimba eti mtaisoma namba! Wakati hali zenu ni mashaka matupu
View attachment 306607
 
Mapambano yanaendelea alisema Lowassa jumapili.
The battle has been lost but the war continues................
 
Jambo la msingi kabisa ni wabunge wote kujiuliza, nini faida na hasara ya ama zomeazomea au kutozomea hotuba ya rais. Wananchi wanataka kusikia zomeazomea au hotuba ya rais?

Wamesema hawataki hotuba? Rais atahutubia tuu, lakini utata waliosema ni wa Shein kuingia kama Rais wakati muda wake umekwisha na majibu kuhusu nini katiba inavyosema hayajajibiwa ipasavyo bali kihuni huni na AG kama vile bora liende.
Sasa ili kuheshimiana, wao nao wanao wajibu wakuonyesha kuwa Shein hastahili kuingia mle. Wataonyeshaje? Hilo mtalijua wakati ukifika.
Hivi huyo Shein kama angekuwa na malaria angeletwa hapo akiwa kitandani? Hivyo sio lazima aingie, kama mumeona kuna utata SII ASIJE TUU? Mbona mnalazimisha sana?
Eti wanategemea kuwatoa msobe msobe wakishangilia bila ukomo na Rais akishindwa kuhutubia? Hiyo misobe misobe hata wananchi wanaipenda kwani wanajua kuwa kumbe wawakilishi wao wakiamua kutetea kitu hawajikombi na wanasimamia wanalo amini. Ushahidi ni jinsi Mhe. Sugu alivyo komba kura na kuwa mbunge mwenye kura nyingi bungeni
 
umesema vizuri sana ndugu, kitendo cha shein kuingia ndani kitaharibu kila kitu na ndio utakuwa mwanzo wa vurugu kubwa kitu kitakachosababisha AIBU kwa Taifa


Shein kuna kosa gani akija bungeni nani aje na yeye ndio Rais wa Zanzibar
 
Wapinzani wamejipambanua kama wao ni maadui wa serikali...CCM walijitahidi katika kipindi kilichopita kuwakaribisha kundini kwa moyo mkunjufu... Raisi Kikwete....alitoa nafasi za ubunge kwa wanachama wa vyama vya upinzani....lakini angalia lugha na vijitabia vya hao watu waliopewa fursa hizo...wanaongoza kwa lugha za kejeli..... wapinzani walipewa hadi uongozi kwenye kamati za bunge... wapinzani walipewa nafasi ya kurekebisha Katiba iliyopo..... TUMEJIFUNZA KUTOKANA NA MAKOSA SASA TUNATAMBUA NIA NA LENGO ZA WAPINZANI KUWA NI MAADUI NA SISI TUNASEMA .....THIS TIME NI VITA NI VITA!!!

Wewe ninani?
 
Jambo la busara na kubwa kuliko yote Shein asubiri nje. Pia kwa kuwa hakuna baraza la wawakilishi basi hata serikali hakuna zanzibar, na kwa kuwa serikali hakuna zanzibar hata rais anaongoza serikali gani?
 
Bunge linaanza saa ngap mana sitaki likosa leo
 
Ni bora Shein kutohudhuria ili mambo yaende sawa,mbali na hapo tutarajie patashika ndani ya bunge

Dr Shein ndiye ajipime kama anatosha kuingia kwenye uzinduzi wa Bunge la 11 au la!!! Kwa maana lolote litakalotokea yeye ndiye wa kulaumiwa, ndiye chanzo kwa sababu nina hakika hapo alipo anafahamu ukweli wa kilichotokea Zanzibar na roho yake itakuwa inamsuta. Anafahamu pasipo shaka kuwa safari hii kura hazikutosha kwake.
 
Watanzania wa ajabu sana mnawapamba ukawa ni chama hakipo ila hao ukawa wasifanye ujinga hapo bungeni leo
 
Jambo la msingi kabisa ni wabunge wote kujiuliza, nini faida na hasara ya ama zomeazomea au kutozomea hotuba ya rais. Wananchi wanataka kusikia zomeazomea au hotuba ya rais?

Mimi niliyepigia kura ukawa nataka wabunge wafanye chochote kitakachowasilisha ujumbe kuwa hatukubaliani na ubakaji wa demokrasia unaofanywa na CCM ktk uchaguzi wa Zanzibar.
 
Mie naona Dr shein ijipime mwenyewe kama anauhalali wa kudhuru bungeni wakati mda wake wa kukaa madarakani umekwishakukoma na mie nilifikilia Dr atakoma kuwa raisi tu endapo atashiriki kugombea kiti cha uraisi maana kuendelea kukalia kiti cha uraisi huku ukikitafta ni miongoni mwamakosa makubwa maana kiuhalisia mara tu mda wako wakuisha unapashwa kuachia nafasi kwa watu ambao wanaweza kuiongoza nchi ikiwa raisi bado hajapatikana nilitegemea Zanzibar itakuwa chini ya jaji mkuu au katibu mkuu kiongozi kwa mda wote pindi wakiwa wanatafta mwafuaka maana kuendelea kukalia kiti cha uraisi kwa Dr shein nikuonyesha jinsi gani asivyoheshimu kanuni na taratibu za nchi.
 
Hivi ukiwa ccm ubongo unakuwa na utando wa kijani pia?
 
Back
Top Bottom