Noncommited
JF-Expert Member
- Jun 22, 2012
- 1,125
- 369
Wapinzani wamejipambanua kama wao ni maadui wa serikali...CCM walijitahidi katika kipindi kilichopita kuwakaribisha kundini kwa moyo mkunjufu... Raisi Kikwete....alitoa nafasi za ubunge kwa wanachama wa vyama vya upinzani....lakini angalia lugha na vijitabia vya hao watu waliopewa fursa hizo...wanaongoza kwa lugha za kejeli..... wapinzani walipewa hadi uongozi kwenye kamati za bunge... wapinzani walipewa nafasi ya kurekebisha Katiba iliyopo..... TUMEJIFUNZA KUTOKANA NA MAKOSA SASA TUNATAMBUA NIA NA LENGO ZA WAPINZANI KUWA NI MAADUI NA SISI TUNASEMA .....THIS TIME NI VITA NI VITA!!!
Acha upotoshaji Rais kumteua kada wa Chama cha Upinzani haikuanza kwa JK hata Mkapa alimteua kada wa CUF kuwa Mbunge.
Kuhusu Wapinzani kupewa uongozi wa baadhi ya kamati ni kwa mujibu wa Mbunge ya Jumuiya ya Madola na si matakwa ya CCM. Kamati za Mashirika ya umma na serikali za mitaa zinazohusu mahesabu zinatakiwa ziongozwe na Wabunge wa Upinzani.
CCM ndio wanawaona WAPINZANI ni maadui Mfano wanatumia polisi kuwapiga marungu na mabomu, kuwamwagia maji ya kuwasha n.k na imefikia hatua wanawaua kama kuku mf. Mwangosi, Mawazo, mwenyekiti wa CDM kule Arumeru, mauaji ya Wapemba 2001, kupigwa kwa Lipumba, Josephine, Lema, SUGU, Msigwa na mengine mengi sana