Rabia Hamid: CCM haiwezi kuondoka leo wala kesho

Rabia Hamid: CCM haiwezi kuondoka leo wala kesho

"Wanaosema CCM Itaondoka, Ni lini, mwaka gani na kivipi..? haiwezekani leo wala kesho CCM kuondoka" - Rabia Abdallah Hamid, Katibu wa NEC Siasa na ubusiano wa kimataifa CCM


Vijana wenyewe ndiyo hawa hapa chini:

TOKA MAKTABA :
24 January 2025
Dar es Salaam, Tanzania


View: https://m.youtube.com/watch?v=woYIDnx1xcw

Wanafunzi wa vyuo na vyuo vikuu mkoani Dar es Salaam wametoa tamko rasmi kuunga mkono azimio la Mkutano Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kumteua Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa mgombea wa urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na Dkt. Hussein Ally Mwinyi kuwa mgombea wa urais wa Zanzibar kwa uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.

Soma Pia:
OTUBA YA Pascrates Albinus Mwemezi kwa vyombo vya habali leo wakiwa Ofisi ya CCM mkoa wa DSM :FIRE:

"Vihongozi wa vijana vyuo vikuu watoa tamko kupongeza mkutano mkuu mahaalum kuunga mkono lahisi wa jamhuri la muhungano wa Tanzania Mh. Samia Hassan kuwa mgombea pekee na lahisi wa Zanzibar mh. Dr. Ussein Hali Mwinyi kuwa mgombea pekee wa ulahisi Zanzibar , wawili ao kupepelusha bendela ya CCM katika uchaguzi wa Oktoba 2025 " - Vihongozi wa Vijana wa CCM Vyuo Vikuhu wasema

Pascrates Albinus Mwemezi Kada huyo wa UVCC kiongozi wa wasomi wanaCCM hakiongea na wahandishi wa habali alikumbushia makubwa yaliyofanywa na mheshimiwa lahisi ikiwemo kuongeza boom kwa wanafunzi wakati alipowahalika vihongozi wa wanafunzi hikulu mwezi Febluali 2022 ...

Ni fulaha kubwa kuona Mkutano Mkuu wa Mahalumu wa CCM kwa kutumia madalaka yake talehe 19 Januali 2025 kwa mujibu wa ibala na kanuni za katiba za chama kuwapitisha wakuhu ao wawili kwa nafasi ya ulahisi ..

Sisi vijana wasomi wa vyuo vikuhu tuna fulaha sana ... kwa lehema ii nyingi kutoka kwa mwenyezi Mungu kutupatiha mheshimiwa lahisi anayetekeleza miladi ya kimkakati inayotuletea nehema na falaja kuu ... miladi kama ya humeme, SGR, Samia Scholarship....
 
Wazee wa chama dola wastuka hakuna vijana ndani ya vyama Kongowe dola:

Radison Blu Hotel, Kempton Park Johannesburg tarehe 25 hadi 28 Julai 2025

MADA : KULINDALI MAFANIKIO YA VYAMA VYA UKOMBOZI BAADA YA UHURU, VINAENDANA NA HAJA YA VYAMA HIVYO KUBAKI MADARAKANI

African National Congress (ANC) itakuwa mwenyeji wa Kongamano la Kilele cha Vyama vya Ukombozi 2025 katika Hoteli ya Radison Blu, Kempton Park kuanzia leo tarehe 25 hadi 28 Julai 2025 chini ya mada: "Kulinda Mafanikio ya Ukombozi, Kuendeleza Maendeleo Jumuishi ya Kijamii na Kiuchumi, Kuimarisha Mshikamano wa Afrika."

Mkutano huu muhimu unathibitisha misingi ya kiitikadi ya vyama sita vya ukombozi Kusini mwa Afrika - ANC, MPLA, SWAPO, FRELIMO, ZANU-PF na CCM - na jukumu lao la kihistoria katika kupata uhuru, utu na maendeleo katika eneo lote la Kusini mwa Afrika.

Pia Kongamano linalenga kusisitiza umuhimu wa harakati hizi kuwa katika mpangilio unaotambua mabadiliko ya mazingira ya kisiasa na kimataifa yanayobadilika haraka.

Vyama vya ukombozi vya Kusini mwa Afrika vilibadilisha hali ya kisiasa ya eneo hilo, kupinga utawala wa kikoloni na ubaguzi wa rangi, na kukaribisha utawala unaozingatia watu.

Tangu uhuru, vuguvugu hizi zimetekeleza sera muhimu kuhusu mageuzi ya ardhi, elimu, makazi, miundombinu na ulinzi wa kijamii.

Hata hivyo, mafanikio haya sasa yanakabiliwa kumegeka kutokana shinikizo jipya la mataifa ya kibeberu, migogoro ya kiuchumi, na majaribio ya kuingiliwa na ukoloni mamboleo.

Mkutano huu unatoa jukwaa moja la kukabiliana na matishio haya na kujumuisha majibu ya kimaendeleo ya kikanda yanayokitwa katika Pan-Africanism (Umajimuhi wa Kiafrika), internationalism na multilateralism.

Mkutano huo ni uingiliaji wa kimkakati katika uanzishaji upya wa mpango kazi (framework), kuimarisha mshikamano wa ndani ya chama, na kurekebisha harakati za ukombozi na matarajio ya kijamii na kiuchumi ya kizazi kipya.

ANC inaamini kwamba uhai wa kisiasa, kiuchumi na kiutamaduni wa urithi wa ukombozi wa Kusini mwa Afrika unahitaji kuchunguzwa kwa uaminifu, ukweli, kujifunza kwa pamoja na umoja unaoweza kutekelezeka.
Mkutano huo utaendeleza mifumo ya ushirikiano kati ya vyama, ushirikiano wa kikanda, ushirikishwaji wa vijana, na utawala huru wa rasilimali.

Kupitia kuthibitisha tena maadili ya pamoja na kuimarisha ushirikiano, Kongamano la Vyama la Ukombozi 2025 utapanga njia mpya ya kusonga mbele, ambayo inalinda mafanikio ya zamani huku ikijenga mustakabali wa Afrika wenye haki, jumuishi na unaojiamulia.

Vyombo vya habari vinashauriwa kuzingatia yafuatayo:
Wajumbe wameanza kuwasili leo, Alhamisi, tarehe 24 Julai 2025 na Wakuu wengi wa Wajumbe watawasili kesho Ijumaa, tarehe 25 Julai 2025. Watatua kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Oliver Reginald Tambo, Wanaowasili Kimataifa,.

Wakuu wa Ujumbe :

  • Cde. Mizengo Kayanza Pinda, Head of Delegation, CCM, Tanzania
  • Cde. Chakil Aboobacar, Katibu Mkuu, FRELIMO, Msumbiji
  • Cde. Mara Baptista Quiosa, Naibu Rais, MPLA
  • Cde. Sophia Shaningwa, Katibu Mkuu, SWAPO
  • Cde. Obert Mpofu, Katibu Mkuu wa ZANU-PF
  • Cde. Liu Jianchao, Kamati Kuu ya CPC (IDCPC), Chama cha Kikomunisti cha China (CPC)
  • Cde. Mohamed Yeslem Beisat, Mkuu wa Ujumbe, Polisario Front
  • Cde. Jibril Rajoub, Katibu Mkuu, Harakati ya Ukombozi wa Kitaifa ya Palestina - FATAH
  • Cde. Solly Phetoe, Katibu Mkuu wa COSATU
  • Cde. Solly Afrika Mapaila, Katibu Mkuu, SACP
  • Cde. Mike Soko, Katibu Mkuu wa SANCO
  • Cde. Apa Poe, Katibu Mkuu, PAC
The African National Congress (ANC) will host the 2025 Liberation Movements Summit at the Radison Blu Hotel, Kempton Park from the 25th to 28th of July 2025 under the theme: “Defending the Liberation Gains, Advancing Integrated Socio-Economic Development, Strengthening Solidarity for a Better Africa.”
Source : https://www.anc1912.org.za/liberati...ng-the-gains-confronting-the-future-together/
 
Basi tuseme CCM ni chama cha kutawala milele, vizazi na vizazi, karne na karne! vyama vya upinzani vimeundwa kimagumashi tu ili kuwazuga wahisani/wafadhili ionekane Tanzania nayo ina demokrasia ya vyama vingi!. Mpinzani wa kweli kuwahi kutokea wa chama cha upinzani ni Lissu tu na ndani ya chama tawala TANU/CCM ni Kambona tu, hawa wengine wanazuga wananchi tu kwamba ni wapinzani kumbe pro chama tawala na wananufaika nacho kama wafanyakazi wao! Itoshe kusema CCM ni chama pekee kilichopo Tanzania tangu kuanzishwa kwake, yaani Tanzania ni nchi ya mfumo wa chama kimoja kama China na chama chao CCP ambacho ni rafiki mkubwa wa CCM. CCP haiko tayari kuona rafiki yake mkubwa aliyeko Afrika anaanguka na kupotea kwenye utawala wa dola ! Waasisi wa CCM walikuja na kauli mbiu ya chama chao isemayo kidumu cha cha mapinduzi, wakaitikwa kidumu, wakaindeleza na kusema kitaendelea kudumu na kina wenyewe, wenyewe ndio sisi, mimi pamoja na wewe!!!
 
Kauli kama hizi ni mbovu, husababisha maafa kama yale ya Oktoba 29, ni kauli za kijuha na kishari. Kauli hizi za kishenzi husababisha majanga nchini na kupelekea wananchi kutokuona umuhimu wa kupiga kura kama ilivyotokea uchaguguzi mkuu uliopita wananchi wengi hawakwenda kupiga kura huku wakiwa tayari wana vitambulisho vya kupiga kura. Wananchi wanaona kwenda kupiga kura ni kujisumbua tu kwa kuwa CCM tayari inajinasibu kuwa haitaondolewa madarakani kwa namna yeyote ile
 
"Wanaosema CCM Itaondoka, Ni lini, mwaka gani na kivipi..? haiwezekani leo wala kesho CCM kuondoka" - Rabia Abdallah Hamid, Katibu wa NEC Siasa na ubusiano wa kimataifa CCM

Huyu ,atunze maneno ,pumbavu , nani alijua tz Rais anaweza kufa akiwa madarakani , hajui Dunia , ccm ilishakufa kilichopo ni kiini macho kwa mgongo wa vyombo vya dola
 
Viongozi wengi wa ccm wana vyeti vya mirembe sasa huyu mmoja wao🤣🤣
 
Naunga Mkono Hoja kwa 💯% kaongea Ukweli Ambao naongea kila siku Humu Kuwa CCM itaongoza na kusalia madarakani mpaka Mwisho wa Dunia
 
Back
Top Bottom