Dodoma: Askari Polisi auliwa na raia

Dodoma: Askari Polisi auliwa na raia

rest in peace kamanda Joseph Isaack Swai my classmate na jirani yangu kitaani Arusha. wana PCB longido high school tutakukumbuka daima kwa ucheshi wako.. polisi jamii Dodoma imepoteza mtu makini sana. i will dearly miss you bro. pumzika kwa amani

Poleni sana .....
 
Afadhali imetokea Dodoma,ingetokea Mbeya,Arusha,Mwanza yangekuwa mengine hapa
 

Attachments

  • 1423065772089.jpg
    1423065772089.jpg
    29.4 KB · Views: 30,598
  • 1423065783281.jpg
    1423065783281.jpg
    33.2 KB · Views: 40,870
Si sahihi kufurahia kifo cha polisi kwa kuwa tu wanahusishwa kwenye kuwadhibiti wanasiasa ambao wengi wao wameathiriwa wao ama viongozi wao.

Mnaweza mkawa mnafurahia mwenzenu kuuawa kwa kuwa ni polisi lakini kumbe ni mmoja wa polisi wanaochukia uovu unaofanywa na baadhi ya polisi wenzake ila kutokana na utaratibu wake wa kazi hawezi kuonesha hisia zake.

Msidhani kwamba vifo vya askari polisi vitawapa unafuu wa mienendo yenu. Polisi hawa mnaowadharau ndio msaada kwa wananchi, au mnataka kutuaminisha kuwa hakuna haja ya kuwa na polisi?

Tumeambiwa kuwa polisi alienda kumkamata mtuhumiwa aliyekuwa anampiga mtoto, sasa kosa ni la nani na siasa za kina Prof. Lipumba zinaingiaje hapa? Au mnakubaliana na uhalifu aliofanyiwa mtoto na badala yake ni kuwa polisi ndiye mwenye kosa?

Kama huu ndio upinzani basi ni too much.
 
Masikini huyo kijana hanaga makuu na mtu ni kijana mwenzetu hakika umekufa ukitetea uhai wa mtanzania mwenzako tunakuweka kwenye kumbukumbu za mashujaa.

Acha watuchukie hila tuliapa kuwalinda hata kwa kwakumwaga damu zetu ee mungu tupe ujasiri na upendo katika kulilinda taifa letu.
 
Waueni tu hila kama nao wengikuwa wauaji km mnavyodai sidhani km mmengukuwa mnaandika utumbo huo kwa amani labda niulize kuna askar aliuwa raia akabaki salama na kazi yake si wote wapo jela? ss mnaposhabikia binadamu mwenzio kuuliwa we unajiona uko salama kbs?

Hapo ni sawa na nyani kucheka wakt chaka linawaka moto wkt jion atakosa pa kulala. Ebu tukemee maovu bila kujali ni nani wala nani kila raia ana haki ya kuishi na mungu hapendi tuwe wanyama kiac hicho.

wewe dada hivi kamuhanda yupo gereza gani vile
 
Habari nyingine huwa zinafanya jioni yaki kuwa nzuriiii na kukupa sababu ya kupiga hata beer mbili tatu za kusheherekea. Safi sana raia WEMA wa Dodoma. Safi mno.

Hata mimi nimeipenda hiyo. Sasa hivi ni hivyo tu. Kwanza sasa hivi vijana ni kujipanga kuwasaka askari wanaokaa mitaani. Make wao wamegeuka wafuasi wa kutumikia mafisadi na kutuona raia kama siyo watu.

Sera ya CUF ndo inayopaswa kutumika. (Jino kwa Jino) Kova anapotoa Mafisadi wanapotoa amri ya kupiga raia basi nasi tujiandae kujibu. Jino kwa jino ndo litatuokoa raia
 
Upumzike unapostahili kamanda...marehemu yaonekana ni muhanga wa films za kichina alizoangalia utotoni kataka ku-act kama komandoo but maskini ya Mungu kumbe hana hata mazoezi yakuruka kamba..

Ujinga wa movie za kichina utamuona mtu anamrukia adui ktk tope na hatelezi ila wewe jaribu kuruka kama yeye uone kama hukujua kilichomtoa mbuni manyoya..

Askari wetu wanatakiwa wajue kwamba Tz ya sasa sio ile ya mtu anaona gwanda anasalimu amri kuna situation nyengine kama mazoezi huna bora utumie gun hata kwa kumtisha mtuhumiwa tu kama sio kumvunja mguu..
 
Umesema sahihi. Suala hili si la kisiasa hata. Lakini kwa lolote linalotkea Tanzania ccm haiwezi kukwepa kwa sababu imejenga taifa ya kinafiki, fitina, mauaji na ulaghai. Kwa uongozi wa ccm, sasa hivi Watanzania wamekosa uzalendo kiasi cha kusema liwalo na liwe. Lakini bado serikali hii haijifunzi kutenda haki ili kujenga imani ya raia kwayo.

Kungelikuwa na Uzalendo japo kidogo, raia ndiyo walitakiwa ktoa mwongozo kwa askari wapi mharifu alipo na wangemlinda aaskari yule dhidi ya uharamia wowote ambao ungefanywa na wenye nia ovu.

Jambo ili si dogo na linatakiwa kulaaniwa na kila mtanzania mwenye mapenzi mema na Tanzania yetu. Lakini ikiwa serikali ya ccm itaendelea kutumia vyombo vyake kunyanyasa raia badala ya kutenda haki, umbali kati ya raia na serikali utazidi kuongezeka. Haya ni matokeo ya wananchi kuiona serikali ni adui wa haki zao na ndiyo maana wanakusudia kufanya lolote kama vile wanamsaidia mwenzao kuua nyoka.

Serikali hii, inatakiwa kuchukua hatua za marekebisho mara moja ili kurejesha imani ya wananchi na heshima yao kwa serikali. Vinginevyo, hii ni hatari sana sana sana.


Tabby

Mimi naomba tutenganisha siasa na mambo mazito kama haya. Mimi naamini kabisa kinachotendeka sasa hivi ni jamabo zito sanaaaaa. Haijatokea hata siku moja wananchi wakamwua askari kikatili hivyo.

Hiyo siyo jadi na mila za Watanzania. Kuna kitu kikubwa sana kipo kinakuja na kitafika. Serikali inatakiwa iwe makini sana na mwendelezo wa vitu vinavyotokea sasa hivi.

Kwa mawazo yangu kinachotokea sasa hivi ni mwendelezo wa mtandao wa kuuawa kwa askari na kupokonya silaha kule Geita(? sikumbuki vizuri ni mwaka jana lilitokea), Tanga, Ikwiriri, na juzi juzi Morogoro. Polisi vilevile wamepigwa mabomu kule Songea mara kadhaa.

Huu ni mwanzo wa ngoma, inakuwa lele baadaye inakomaa. Boko Haram walianza kwa kuwaua Wakristo makanisani sasa wanawaua Waislamu wenzao.


Beware Tanzanians. Beware. Something is coming your way.
 
Afadhari nao wafepo. Wamezoea kutumwa na ccm km mbwa kuua na kupiga raia wasio na hatia
 
jamani mfikishieni mh pinda hii taarifa ili akaifute ile kauli yake ya ( wapigwe tu ) yeye ndio chanzo cha mauaji ya maaskari wetu dhidi ya kauli ile ilyotengeneza uadui kati ya raia na askari,
(RIP askari)
 
IIliyopo sasa ni vita kati ya polisi na wananchi waliowengi wanaochukizwa na namna polisi wanavyotekeleza sheria kwa kukiuka sheria.

Ni wazi kwamba huyu askari kabla ya kwenda jukumu lake hilo alipaswa kuchukua tahadhari na kwenda akiwa na zana zote. Na inasikitisha kwamba hata wananchi waliokuwepo ktk eneo la tukio walishindwa kumpa msaada stahiki askari huyu, na inawezekana ni chuki hiihii tunayoisema!!

Tunawashauri maafisa wa jeshi hili wakubwa wanaotoa amri wakiwa ofisini pamoja na viongozi wa serikali kutotoa amri za ovyoovyo ili zitekelezwe na hawa askari wabeba bunduki na mabomu ya machozi kwa sababu wana risk maisha ya askari hawa maskini wafuata amri.

Hatusemi kuwa jeshi la polisi lisifanye kazi yake bali tunachotaka askari wetu watekeleze majukumu yao kwa kuzingatia weledi wa kipolisi na kufuata sheria na kuheshimu haki za binadamu.

Askari wetu wajiepushe kabisa na wanasiasa walafi wa madaraka kwa gharama ya damu za watu kwani mwisho wa siku ni kwamba pamoja na kuwa wao ni askari wanaobeba silaha kwa namna wanavyoweza kuzitumia mahali popote na wakati wowote ili mradi wamepewa amri ya kuzitumia, ukweli ni huu kwamba bado wao ni binadamu kama sisi wengine na tunaishi nao mitaani na wanahitaji msaada wetu ili waweze kufanya kazi vyema na kwa ufanisi!!..

Lakini kama hali hii itaendelea, wanaowatuma wawahamishie askari wote katika kambi ili wawe wanatoka kwa kwa makundi kutekeleza operesheni zao kama zige na badae wanarudi kwenye viota vyao.....japo haisaidii kwa sababu tutakutana nao sokoni, bar, disco na mikusanyiko mingine ya kijamii. Muhimu ni kujenga mahusiano mema, baaaaasi!

R.I.P Cammander Swai!!!
 
Back
Top Bottom