Do alliens exist?

Do alliens exist?

Anhaa kumbe kablaya adamu na hawa walitengenezwa binadamu wengine wakatoroka sasa wako wapi mkuu kwa sasa na jee hawakupatikana tena(bali najua ni chai lakini wacha nijitoe ufahamu niulize tu)
Mkuu hata kama ni chai ila sio yangu imeandaliwa Mwandishi wa kitabu.Na mimi nilipokuwa nakisoma niliiona ni chai ndo maana sikukimalizia kukisoma hicho kitabu.Ila nimeamua kuyaandika hapa baada ya jamaa niliyemu quote ameongea mambo ambayo hicho kitabu kiliyazungumzia sana.

Ukitaka kujua hao watu wako wapi kitafute ukidownload kinaitwa Atlantis visitation and Genetic manipulation. By Michael Tsarion
 
Isue inayofanana na hii niliwahi kuisoma kwenye kitabu fulani kinaitwa Aliens visitation sikukisoma mpaka mwisho kwa sababu niliona kinanichanganyia madesa.Ila kinavyodai

Asili ya binadamu ni alliens waliofukuzwa katika sayari fulani ndipo wakaja duniani.Wakaanza kuishi chini ya ardhi ndo maana kuna underground tunnels kubwa sana zina miaka mingi sana duniani ambazo wanasayansi wengi wanajiuliza nani alizijenga.Baada ya hapo wakaenda kuishi bara la atlantis ambalo lilikuja kuzama mwanafalsafa Plato katika kazi zake za "Timaus" na "Critias" amelizungumzia sana bara la atlantis na kuzama kwake.Japo kuna watu sasa wanadai Antarctica ya Leo ndio Atlantis.Kiufupi Atlantis ndio yalikuwa makao makuu ya hawa aliens.

Baada ya kuishi Atlantis miaka mingi wakaamua kutengeneza kiumbe watakayemfanya awe mtumwa wao.Lakini wakakosea kwa sababu walitengeneza binadamu aliyekuwa sawa kiuwezo na wao.Hivyo akaja kuwaasi akawatoroka akaenda kuishi mabara mengine.

Baada ya kufanya kosa kumpa uwezo binadamu sawa na wao.wakaamua kutengeneza kiumbe dhaifu atakayewaheshimu milele na kuwa mtumwa wao daima ambao ndio Adam na Hawa wakawekwa bustanini.

kuna mengi sana naomba kuishia hapa.

Kweli watu theories nyingi lakini hata kwenye story ya genesis uumbaji inasema tuumbe mtu kwa mfano (wetu)...
Kama kuna mtu haamini uwepo alliens na ukaribu wao na binadamu wa zamani atafute kuhusu hivi vitu mtandaoni...
  1. Acient uraniam reactors gabon
  2. Antikythera Mechanism
  3. Baghdad Battery
  4. The Coso Artifact
  5. The Giant Stone Spheres of Costa Rica
  6. Rama's bridge(rama setu).story kamili kutoka vitabu vya kale.
  7. Swali la mwisho waliwezaje kujenga pyramids kubwa kiasi hicho wakati teknolojia ilikuwa ndogo sana na ni nani ali waelekeza wajenge pyramids hizo katika mstari ulio nyooka kukatiza dunia katika mabara yote wakati walikuwa hawajuani wala hawakuwa na imani sawa (ukiangalia Teotihuacan pyramid iliyopo Mexico, Tenerife (Guimar) katika Canary Islands, Ancient Egypt, mpaka Xi'an nchini China)
  8. Kuna vitu vingi hatuvijui na hatutakaa tuvijue binadamu umriwake miaka 100 dunia ina miaka bilioni kadhaa
 
Aliens ni demons, au unaweza wait a fallen angels. Ni viumbe wa kiroho hawana miili kama Mimi na wewe. Viumbe Hawa, wamekuwa wakifanya maingiliano ya kingono na wanaadamu na kutengeneza viumbe (hybrid) wenyewe maili kama ya watu wa kawaida. Viumbe Hawa wana bases zao katika baada la Antarica, na pia katika Bermuda triangle, na hata katika Dragon's Triangle. Bermuda triangle kuna mlango wa kuingia katika bara la Antarctica(south pole). Meli, na hata ndege hupotea au kuzama katika Bermuda triangle. Aliens, au damons, ndiyo nyakati zingine wanaitwa "Watchers", au " Guardians". Aliens wapo , na ndiyo wanaosaidia nchi za Marekani, Russia, China, na hata Japan, katika matengenezo ya silaha za kivita kama vile madege ya B2 ambao ni anti gravity,na silaha za laser. Vile vile , Hawa Aliens ndiyo waliomsaidia Adolf Hitler kutengeneza submarine aina ya U-Boat, na hata matengenezo ya gari isiyotumia maji wakati wa vita juu ya pili ya Dunia.. Aliens wapo, na base yao iko Antartica ambako Hitler alitorokea.
Jazia ...wanabadilishana na mataifa hayo kwa madini aina ya copper ambayo wanahitaji sana kwa ajili ya kuunda vitu vyao mbali mbali hasahasa vifaa vya kivita kujiweka sawa kabla ya kuanza mapigano mengine na another aliens species..
 
Mkuu hata kama ni chai ila sio yangu imeandaliwa Mwandishi wa kitabu.Na mimi nilipokuwa nakisoma niliiona ni chai ndo maana sikukimalizia kukisoma hicho kitabu.Ila nimeamua kuyaandika hapa baada ya jamaa niliyemu quote ameongea mambo ambayo hicho kitabu kiliyazungumzia sana.

Ukitaka kujua hao watu wako wapi kitafute ukidownload kinaitwa Atlantis visitation and Genetic manipulation. By Michael Tsarion
Nimekusoma mkuu ngoja nitafute PDF yake
 
wapo tena kuna viumbe wengi tuu marekani ambao no crossbreed ya binadamu na alliens
 
Anhaa kumbe kablaya adamu na hawa walitengenezwa binadamu wengine wakatoroka sasa wako wapi mkuu kwa sasa na jee hawakupatikana tena(bali najua ni chai lakini wacha nijitoe ufahamu niulize tu)
Ucjitoe ufahamu agiza vitafunwa tu maana hamna namna
 
Alien wapo uwa zikitokea public wanafanya cover up but still info zina leak
 
Nani amekudanganya ?. Satanism na Illuminati ni kitu kimoja. Ni kama ilivyo Giza na Kivuli. Ile alama ya jicho lililo katika pyramid ambayo haijaisha, unjua jicho hilo ni la nani kama sio Lucifer mwenyewe?.
Mkuu satanism ilianzishwa na ANTHONY LARVEY mnamo mwaka 1966 na illuminati ilianza before 1 May 1776. na ilianzishwa na mtu mmoja wanamuita......Adam Weishaupt (1748–1830), ilijulikana kama Bavarian Illuminati MKUU USIMEZE KILA KITU TAFADHALI SOMA UELEWE MA kwa maelezo zaidi google hayo majina ilo usome historia zao
 
Usitazame walioanzisha. Tazama malengo, na madhumuni ya societies hizo kuanzishwa. Kwa hiyo hawatoi kafara?. Hao huwezi kuwatenga lengo lao ni kuabudu ibilisi.. Kalaga baho.
 
Aliens wapo kwa sababu hata sisi binadamu ni alliens wa zamani hii story inajulikana arround all world's culture.

We human being we are the ancient alliens from the space.
 
Back
Top Bottom