Tindo
Platinum Member
- Sep 28, 2011
- 71,410
- 127,908
Naandika Rashda binti Zunde✍️
Watanzania amkeni, Watanzania amkeni tupinge watu kama hawa wanaotusi viongozi wa nchi hadharani. Tuungane kukemea vitendo kama hivi huu ni udharirishaji wa Rais wetu, huwezi kutoka hadharani kusema "hoja za rais ni za kipumbavu".
Wote tunajua kwamba Rais Samia Suluhu ameweka wazi dhamira yake ya kuhakikisha kwamba katiba mpya inapatikana na tayari mchakato umeanza, hivi awamu gani iliwasikiliza chadema kama sio hii ya Mama Samia ?
Mchakato wa Katiba si wa siku moja, serikali imeshaanza mchakato, mmeshirikishwa, na sasa ni kutoa elimu kwa wananchi jambo ambalo serikali tayari ilishaweka wazi kwamba zaidi ya 50% ya Watanzania hawajui kuhusu katiba hivyo ni lazima wapatiwe elimu.
Lazima kila Mtanzania aelewe nini kinaenda kufanyika na ndicho serikali inachofanya, sasa wewe Slaa unavyokuja kusema kwamba hoja za Rais Samia Suluhu ni za kipumbavu umekosea sana, ni dhahiri kwamba hujafuatilia nini kinaendelea umekurupuka.
#mamaanafanikisha uhuru wa maoni lakini sio kutoka hadharani kumtusi kiongozi wako wa nchi, Slaa kaa chini tafakari kabla ya kuzungumza mbele za watu. Unajidharirisha kila siku na ndio maana umevuliwa ubalozi sababu huna hadhi na hakuna balozi mwenye tabia kama zako.
Viongozi wanaoingia madarakani kwa chaguzi za kishenzi ni zaidi ya matusi kwa watanzania. Unataka heshima kwa viongozi wanaoingia madarakani kwa njia zisizo za heshima! Toka lini serikali ikitaka kupitisha jambo isubiri hadi ulewa wananchi uvuke 50%+. Huo utapeli wa nia ya rais mkawaambie wenye uelewa mdogo. Na wapinzani watakuwa wajinga sana iwapo wataamini hiyo porojo iitwayo nia ya rais.