Katibu Mkuu wa CHADEMA Dr.Wilbroad Slaa akiwahutubia Maelfu ya Wakazi wa Urambo Tabora alisema Mbinu zote na Dhaifu za CCM zipo Mikononi mwa Chama hiki (Chadema), Kwa Mujibu wa Dr.Slaa CCM Wakiendelea Kutumia Mbinu hizi hizi, Chaguzi zijazo, Saa 4:00 Asubuhi Siku ya Uchaguzi, Watanzania Waanze Kushangilia Ushindi Kwa Sababu hakuna Mbinu yoyote Waifanyayo yenye Manufaa Dhidi yao, ila Mbinu za Kuwaangamiza Vibaya, akifafanua Dr.Slaa anasema "CCM Chaguzi zilizopita 2005 na 2010 Walijiamini sana na Mbinu za Wizi wa Kura hasa Maeneo ya Vijijini, ila Chadema Inapenda Kuwahakikishia Kwamba Chaguzi zijazo 2014/2015 ni Kipindi Kigumu sana Kwao Wapende Wasipende, Watake Wasitake... Haitawezekana tena. Zipo Mbinu Kadha wa Kadha Kama zile za Kuwaondoa Kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura, Baadhi ya Wanachama, Wafuasi na Wakereketwa Wetu wanaoonyesha Msimamo Mkali ndani ya Chadema, hili nalo tunaahidi Kulishughulikia Ipasavyo Kuanzia sasa, na hakika Mpaka Kufikia Uchaguzi wa Mwaka Kesho Kitakuwa Kimeeleweka". MAONI!