Dkt. Nchimbi: Watanzania, msiache kuiombea nchi

Dkt. Nchimbi: Watanzania, msiache kuiombea nchi

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
4,393
Reaction score
14,499
Makamu wa Rais, Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, amewasihi viongozi wa dini na Watanzania kwa ujumla kutumia kipindi cha toba cha Ramadhani na Kwaresma kuiombea nchi, viongozi wa serikali na vyama vya siasa ili kuendelea kujenga taifa lenye upendo, amani na mshikamano.

1773293760364.png

Makamu wa Rais amesema hayo mara baada ya kushiriki futari aliyoiandaa kwa ajili ya wananchi wa Mkoa wa Dodoma pamoja na viongozi wa serikali, taasisi za dini na Chama Cha Mapinduzi (CCM), iliyofanyika mkoani Dodoma.

Amesema jambo muhimu ni kuhakikisha hamasa ya mapenzi ya nchi inakuwepo kwa kila mmoja, huku chemchem ya uzalendo ikijengeka katika mioyo ya Watanzania ili waishi kwa kupendana na kushirikiana chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Aidha, Makamu wa Rais amesema moja ya mambo muhimu ya kufanya katika kipindi cha toba ni kumwahidi Mwenyezi Mungu kuwa kila Mtanzania atajitahidi kuwaunganisha Watanzania wenzake ili kuijenga nchi kuwa taifa moja lenye upendo.

Futari hiyo imehudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhandisi Hamad Masauni, Katibu Mkuu wa CCM, Balozi Dkt. Asha-Rose Migiro, Waziri wa Madini Anthony Mavunde, wajumbe wa Kamati ya Maridhiano, viongozi wa dini, wabunge wa Mkoa wa Dodoma, wakuu wa wilaya pamoja na wananchi.

 
Kumwombea, kuiombea? Hiy kaul anapenda sana kuziongea yale yale ya magufur mniombee mniombe!! Nini kipo nyuma ya hiyo kauli
 
Makamu wa Rais, Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, amewasihi viongozi wa dini na Watanzania kwa ujumla kutumia kipindi cha toba cha Ramadhani na Kwaresma kuiombea nchi, viongozi wa serikali na vyama vya siasa ili kuendelea kujenga taifa lenye upendo, amani na mshikamano.


Makamu wa Rais amesema hayo mara baada ya kushiriki futari aliyoiandaa kwa ajili ya wananchi wa Mkoa wa Dodoma pamoja na viongozi wa serikali, taasisi za dini na Chama Cha Mapinduzi (CCM), iliyofanyika mkoani Dodoma.

Amesema jambo muhimu ni kuhakikisha hamasa ya mapenzi ya nchi inakuwepo kwa kila mmoja, huku chemchem ya uzalendo ikijengeka katika mioyo ya Watanzania ili waishi kwa kupendana na kushirikiana chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Aidha, Makamu wa Rais amesema moja ya mambo muhimu ya kufanya katika kipindi cha toba ni kumwahidi Mwenyezi Mungu kuwa kila Mtanzania atajitahidi kuwaunganisha Watanzania wenzake ili kuijenga nchi kuwa taifa moja lenye upendo.

Futari hiyo imehudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhandisi Hamad Masauni, Katibu Mkuu wa CCM, Balozi Dkt. Asha-Rose Migiro, Waziri wa Madini Anthony Mavunde, wajumbe wa Kamati ya Maridhiano, viongozi wa dini, wabunge wa Mkoa wa Dodoma, wakuu wa wilaya pamoja na wananchi.

Yes,
ndugu makamu wa Rais,
Kama vijana tupo imara kuiombea na kuilinda nchi yetu bila kuchoka wala kukata tamaa.

mamluki wenye mapepo ya fujo na vibaraka wa mabwenyenye ya magaharibi hawana nafasi hata kidogo kuidhuru nchi yetu iwe kiuchumi, kisiasa au kijamii.
 
Nchimbi, hizi ni kauli za kitoto, kitotot na kinafiki kabisa. Hakuna cha kuomba hapa, ni nyinyi mliojivika madaraka kuacha kutenda maovu! Mfano, kulikuwa na sababu gani polisi kuwapiga Bawacha? Umekemea? Kwanini mnamuweka Lisu gerezani bila sababu? Halafu unasema kuomba! Kuomba kwetu ni kuingia "msituni" kupigania haki!
 
Maombi maombi maombi ni silaha ya kututoa kenge utumwani sio?

Wakati wao wanakula keki kwa siagi, na kupanga mapolisi kila kona ya mtaa tuendelee kuwatazama na kuwashangilia na misafara yao ya utumbuaji...

Hypnosis!

Eimeeen!
 
Makamu wa Rais, Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, amewasihi viongozi wa dini na Watanzania kwa ujumla kutumia kipindi cha toba cha Ramadhani na Kwaresma kuiombea nchi, viongozi wa serikali na vyama vya siasa ili kuendelea kujenga taifa lenye upendo, amani na mshikamano.


Makamu wa Rais amesema hayo mara baada ya kushiriki futari aliyoiandaa kwa ajili ya wananchi wa Mkoa wa Dodoma pamoja na viongozi wa serikali, taasisi za dini na Chama Cha Mapinduzi (CCM), iliyofanyika mkoani Dodoma.

Amesema jambo muhimu ni kuhakikisha hamasa ya mapenzi ya nchi inakuwepo kwa kila mmoja, huku chemchem ya uzalendo ikijengeka katika mioyo ya Watanzania ili waishi kwa kupendana na kushirikiana chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Aidha, Makamu wa Rais amesema moja ya mambo muhimu ya kufanya katika kipindi cha toba ni kumwahidi Mwenyezi Mungu kuwa kila Mtanzania atajitahidi kuwaunganisha Watanzania wenzake ili kuijenga nchi kuwa taifa moja lenye upendo.

Futari hiyo imehudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhandisi Hamad Masauni, Katibu Mkuu wa CCM, Balozi Dkt. Asha-Rose Migiro, Waziri wa Madini Anthony Mavunde, wajumbe wa Kamati ya Maridhiano, viongozi wa dini, wabunge wa Mkoa wa Dodoma, wakuu wa wilaya pamoja na wananchi.

Wao si wanaiba, wanateka, wanabaka, wananajisi, wanapoteza na kuua raia wa Tanganyika? Basi sisi tunawaombea wapewe malipo stahiki ya maovu yao!
 
Kumwombea, kuiombea? Hiy kaul anapenda sana kuziongea yale yale ya magufur mniombee mniombe!! Nini kipo nyuma ya hiyo kauli
Anatakiwa aeleze kiundani nchi iombewe kwenye aspect gani ili tujenge hoja yenye mashiko mbele za Mungu na kama tutabaini kwa jicho la kiroho kwamba hoja ya MAOMBI yenyewe itaishia kwenye dust bin huo muda ni heri tufanye mambo mengine tu
 
Maombi maombi maombi ni silaha ya kututoa kenge utumwani sio?

Wakati wao wanakula keki kwa siagi, na kupanga mapolisi kila kona ya mtaa tuendelee kuwatazama na kuwashangilia na misafara yao ya utumbuaji...

Hypnosis!

Eimeeen!
Seran tuanze maombi ya kuliombea taifa
 
Makamu wa Rais, Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, amewasihi viongozi wa dini na Watanzania kwa ujumla kutumia kipindi cha toba cha Ramadhani na Kwaresma kuiombea nchi, viongozi wa serikali na vyama vya siasa ili kuendelea kujenga taifa lenye upendo, amani na mshikamano.


Makamu wa Rais amesema hayo mara baada ya kushiriki futari aliyoiandaa kwa ajili ya wananchi wa Mkoa wa Dodoma pamoja na viongozi wa serikali, taasisi za dini na Chama Cha Mapinduzi (CCM), iliyofanyika mkoani Dodoma.

Amesema jambo muhimu ni kuhakikisha hamasa ya mapenzi ya nchi inakuwepo kwa kila mmoja, huku chemchem ya uzalendo ikijengeka katika mioyo ya Watanzania ili waishi kwa kupendana na kushirikiana chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Aidha, Makamu wa Rais amesema moja ya mambo muhimu ya kufanya katika kipindi cha toba ni kumwahidi Mwenyezi Mungu kuwa kila Mtanzania atajitahidi kuwaunganisha Watanzania wenzake ili kuijenga nchi kuwa taifa moja lenye upendo.

Futari hiyo imehudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhandisi Hamad Masauni, Katibu Mkuu wa CCM, Balozi Dkt. Asha-Rose Migiro, Waziri wa Madini Anthony Mavunde, wajumbe wa Kamati ya Maridhiano, viongozi wa dini, wabunge wa Mkoa wa Dodoma, wakuu wa wilaya pamoja na wananchi.

We understand Nchimbis dillema.
Hapo inabidi viongozi wajiombee wenyewe!
Kama kuna nuksi imeingia nchini ni Oktoba 29, hapo hakuna Mtanzania anaweza kukuombea kwa moyo usio na unafiki.
Wajiombee wenyewe na kutubu kw mauaji!
 
Yani badala ya kusema anataka utawala wa sheria anataka tusugue goti? Ni masikitiko sana kuzaliwa kwenye jamii ya namna hii kwa kweli
 
Nchi haiendeshwi kwa maombi.

Hatuwezi kusahau kwanza mpaka hadi yule mpiga risasi wa mwisho akiwajibika na watu watakapopata maiti za ndugu zao wazizike kwa heshima.

Si mliona maiti ya mtanzania iliyokaa miaka 3 huko ila bado walirejeshewa mifupa wazike kwa heshima, mnafikiri ni kwanini?

Hiyo "kamati ya maridhiano" ndio chaka jipya la kupiga pesa za walipa kodi?

Utaridhiana na mtu amezika kiatu cha ndugu yake na video ya maiti yake aliiona nyie mkasema ni AI?
 
Back
Top Bottom