Mkalukungone Mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 2,436
- 5,233
Mgombea mwenza wa Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Emmanuel Nchimbi, amewakumbusha Watanzania kuhusu ahadi za Mgombea Urais wa CCM, Dkt. Samia Suluhu Hassan, alizoziahidi kutekeleza ndani ya siku 100 baada ya kuapishwa endapo atapewa ridhaa ya kuongoza tena nchi.
Amesema hayo alipowasili katika Kata ya Mkula, Wilaya ya Busega, mkoani Simiyu, leo Septemba 1, 2025, kwa ajili ya kunadi sera na ilani ya uchaguzi ya CCM ya 2025–2030.
Dkt. Nchimbi ameeleza kuwa, ndani ya siku 100 za kwanza Madarakani, Serikali ya CCM itaanza kugharamia matibabu ya magonjwa yanayowatesa Watanzania, ikiwemo saratani na magonjwa ya figo.
Amesema hayo alipowasili katika Kata ya Mkula, Wilaya ya Busega, mkoani Simiyu, leo Septemba 1, 2025, kwa ajili ya kunadi sera na ilani ya uchaguzi ya CCM ya 2025–2030.
Dkt. Nchimbi ameeleza kuwa, ndani ya siku 100 za kwanza Madarakani, Serikali ya CCM itaanza kugharamia matibabu ya magonjwa yanayowatesa Watanzania, ikiwemo saratani na magonjwa ya figo.