Dkt. Mwingulu Nchemba awataka Wabunge kujadili sheria wakati wa Utungwaji na Siyo Wakati wa utekelezaji Wake

Lucas Mwashambwa

JF-Expert Member
Jul 28, 2022
17,739
11,979
Ndugu zangu Watanzania,

Waziri wa Fedha Mheshimiwa Daktari Mwingulu Lameck Nchemba Amewataka Waheshimiwa Wabunge pamoja na watanzania wote kujenga utamaduni wa kujadili sheria wakati wa mchakato wa Utungwaji wake na siyo wakati wa utekelezaji wake.

Ameyasema hayo kutokana na swali lililoulizwa na Mbunge wa Mbozi Mheshimiwa George Ranwell Mwenisongole aliyetaka kujuwa na kufahamu ni kwanini vyama vya ushirika vinalazimishwa na TRA kununua na kuwa na mashine ya EFD wakati havifanyi biashara na huuza mara moja tu kwa mwaka.

Akijibu swali hilo Mheshimiwa Dkt Mwigulu amesema kuwa Ukusanyaji wa kodi unafanyika kwa mujibu wa sheria namba 36(1) ya usimamizi wa kodi ya mwaka 2015. ambapo ni lazima mfanyabiashara anayesambaza bidhaa au kutoa huduma au kupokea malipo kutokana na malipo ya huduma aliyotoa anatakiwa kutoa risiti za kieletroniki.

Lakini pia amesema ya kuwa sheria inasema kuwa mfanyabiashara yeyote anayefanya mauzo ghafi ya millioni 11 na kuendelea kwa Mwaka anapaswa kuwa na mashine ya kielektroniki EFD. Ameendelea kusema ya kuwa lengo ni kuhamasisha utunzaji wa kumbukumbu ambapo EFD ni njia nzuri na rahisi yenye ufanisi mzuri wa utunzaji wa kumbukumbu kwa mfanyabiashara.

Amesema pia kuwa haiwezekani mwalimu wa shule ya msingi atozwe kodi halafu aende aachwe tajiri.au mtu mwenye kipato cha chini cha mauzo chini ya Millioni 3 kwa mwaka atozwe na kulipishwa kodi halafu aende aachwe anayepokea malipo ya millioni Mia Moja.Amesema hii haiwezekani na siyo haki. Na kwamba mwezi ujao bunge litajadili pia masuala ya Kodi ,hivyo kama kuna sheria wabunge wanaona haifai basi ndio wakati wa kuijadili ili kuangalia kama itolewe au kufutwa au kufanyiwa marekebisho.

Mimi Mwashambwa Lucas ningependa kusema ya kuwa Waheshimiwa wabunge wetu wawe na utaratibu mzuri wa kujisomea,kutafiti,kuomba ushauri na kusikiliza wananchi wanasema nini wakati wanapokuwa wanajadili na kupitisha sheria fulani Bungeni itakayotumika kwa wanachi na Taifa kwa ujumla wake.

Nasema hili kwa kuwa imekuwa inasikitisha sana ,kuleta aibu , kufedhehesha,kuonyesha kukosa umakini na kutoelewa kwa undani kile wanachokipitisha ndani ya Bunge. kwa sababu ni kawaida unakuta sheria fulani inapita kwa kishindo na kwa kura zote za ndio, halafu baada ya muda wananchi wakianza kulalamika na kukosoa sheria husika mitaani unaona kuna wabunge wanaanza kushangaa kana kwamba ni kitu kigeni masikioni mwao na wala hawajawa kukisikia wala kushiriki katika mjadala wake wala kuunga mkono.

Jambo linaloonyesha aidha waheshimiwa wabunge wanakuwa wakati mwingine hawajapitia vifungu vyote na makabrasha yote yaliyo mezani pao kujuwa maana ya kile wanacho kipitisha na kukiunga mkono. Wakati mwingine mpaka unajiuliza inakuwaje mwananchi wa kawaida aone kwa haraka na ndani ya muda mfupi tatizo la sheria fulani ,halafu Mbunge anayekaa bungeni na kulipwa posho kwa ajili ya kazi hiyo ashindwe kuona tatizo hilo mpaka anapokuja kuona wananchi wakilalamika na kukosoa kwa nguvu na ndipo sasa naye Mbunge aanze kulaumu na kulalamika kana kwamba hakuwepo wakati wa utungaji na upitishwaji wake?

Tatizo nini nini? Shida inakuwa wapi? Kwanini hili linatokea kwa sheria inatungwa leo halafu kesho inakuwa inahitaji mabadiliko na marekebisho? Ni wapi panakosekana umakini? Ni nani hatekelezi wajibu wake? Je, waheshimiwa huwa wanapigia makofi na kuunga mkono mambo wasiyo yajua? Nini kifanyike hali hii isiwe inatokea? Kwa sababu tumeona jambo hili katika suala la kikokotoo ambapo wabunge wakiwa wakali kana kwamba siyo wao waiopitisha na wala hawajawahi kushiriki katika mjadala wa aina yoyote ile unaohusu kikokotoo.

Naweka kalamu yangu chini na kuishia hapa, sitaki kuwachosheni. Lakini tujiulize pia kwanini walipa kodi Tanzania ni wachache sana kuliko idadi ya watu wanaostahili kulipa kodi? Kwanini watanzania hawapendi kulipa kodi na hutafuta njia za kukwepa kulipa kodi kuliko kwenda kulipa kwa hiyari? Je ni kutokutambua umuhimu wa kodi kwa maendeleo ya Taifa letu? Je, ni kutokujua kuwa nchi inaendeshwa kwa kodi na kila kitu tunachotaka kufanyiwa na serikali yetu kinatokana na kodi zetu, ambazo tunatakiwa tuone fahari kulipa badala ya kuwa wakwanza kutengeneza mifumo ya Ukwepaji kodi.

Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa.Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
 
Hadithi ys walipakodi ni wachache ni ya kufikirika zaidi kuliko uhalisia. Walipa kodi Tangabyika ni wengi ila inategemea kodi unaiitaje.

Mfano wakulima wote ambao ni kaMa asilimia 65 ya watanganyika wanalipa kodi wakati wanapopata income kutokana na kuuza mazao yao ila kodi inayolipwa inaitwa cess na inachajiwa kwa kila kg ya mazao wanayouza, ingawa inaonekana kana inalipwa na mnunuzi lakini wanaolipa ni wao wakulima.

Mfanyakqzi yeye anaLipa kodi inayoitwa PAYE. Mfanyabiashara analipa incone taxi kila robo mwaka kwa kutegemeana na faida aliyopata.

Ikatikati kila mtu akinunua bidhaa au huduma analipa VAT sasa unasemaje walipakodi ni wachache, Nenda katika halmashauri angalia kwa-mwaka wanakusanya bilioni ngapi toka katika mazao mfano halmashauri zinazolima korosho , miti nk.
 
Wabunge hawa wa Lasaba B?
Bunge letu lina wabunge wengi sana wasomi. Pia mtu anaweza akawa na Elimu kubwa na akawa na mchango mdogo sana katika mijadala.maana hii inategemea na kile atakacho amua kusimamia kati ya UKWELI na siasa au propaganda.

Mwingine anaweza asiwe na Elimu lakini akawa na mawazo mazuri sana kutokana na uzoefu wake katika eneo fulani iwe ni katika biashara,madini,uvuvi,uchukuzi n.k.
 
Sheria nyingi zilifanyiwa mabadiliko ya haraka haraka kipindi cha magufuli yote hayo ili akusanye hela nyingi kugharamia miradi yake baada ya wahisani au mabeberu kwa maneno yako kumpiga PIN.

Kuna haja ya hizo sheria kupitiwa upya ziwe na Maslahi ya wananchi na sio kukandamiza tu. Hii ni pamoja na sheria iliyoleta kikokotoo Kipya. Wizi mtupu, na itashangaza kuona waajiriwa bado wakiunga Foleni kuipigia kura CCM.
 
Sheria nyingi zilifanyiwa mabadiliko ya haraka haraka kipindi cha magufuli yote hayo ili akusanye hela nyingi kugharamia miradi yake baada ya wahisani au mabeberu kwa maneno yako kumpiga PIN. kuna haja ya hizo sheria kupitiwa upya ziwe na Maslahi ya wananchi na sio kukandamiza tu. Hii ni pamoja na sheria iliyoleta kikokotoo Kipya. Wizi mtupu, na itashangaza kuona waajiriwa bado wakiunga Foleni kuipigia kura CCM.
CCM Ndio imeendelea kuwatetea watumishi wa umma ili serikali iangalie upya suala la kikokotoo ambalo limeonekana kuwa mwiba mkali kwa watumishi wa umma wanaostaafu.
 
Ndugu zangu Watanzania,

Waziri wa Fedha Mheshimiwa Daktari Mwingulu Lameck Nchemba Amewataka Waheshimiwa Wabunge pamoja na watanzania wote kujenga utamaduni wa kujadili sheria wakati wa mchakato wa Utungwaji wake na siyo wakati wa utekelezaji wake...
Umbea mtupu wa serikali. Ni wakati gani maoni juu ya miswaada ya sheria yanasikilizwa? Serkali ikiamua kitu mpende msipende, kitapita. Wabunge wa CCM wana wajibu kupitisha utumbo wowote unaopelekwa bungeni kama mswaada. Ni pale tu wanapokuta wanaumizwa na sheria hizo ndio wanaaza kulalamika. Tumeliona hili mara nyingi sana.
 
Inaanzia shuleni, unasoma sababu ya tukio la mtihani si tahadhari ya maisha bila elimu.

Sasa usishangae mhimili wa kutunga sheria ukijadili iwapo hiyo sheria inatekelezeka au la ilihali wao ndo waliipitisha, sababu ni kwamba siku ya kuipitisha kichwani palikuwa na tukio la posho si taadhari ya matokeo ya hiyo sheria ikipita.
 
Simkubali Bwana Mwigulu PhD,lakini katika hili naunga mkono hoja yake.Ni Wabunge wachache sana ambao hujipa muda kusoma na kufanya tafiti juu ya mambo mbalimbali ya kibunge.

Zaidi walio wengi wanajua kupitisha maazimio tu,ambayo hayahitaji critical thinking.Hata Job Ndugai aliwahi kushangaa sheria fulani ya uhifadhi ilipitaje na wakati huo huo Yeye ndo alikuwa kwenye kiti wakati Sheria inapita.

Bure kabisa Wabunge wetu.
 
Inaanzia shuleni, unasoma sababu ya tukio la mtihani si tahadhari ya maisha bila elimu.

Sasa usishangae mhimili wa kutunga sheria ukijadili iwapo hiyo sheria inatekelezeka au la ilihali wao ndo waliipitisha, sababu ni kwamba siku ya kuipitisha kichwani palikuwa na tukio la posho si taadhari ya matokeo ya hiyo sheria ikipita.
Ndio maana Mheshimiwa waziri Dkt Mwigulu Nchemba ameamua awaambie ukweli waheshimiwa wabunge
 
Simkubali Bwana Mwigulu PhD,lakini katika hili naunga mkono hoja yake.Ni Wabunge wachache sana ambao hujipa muda kusoma na kufanya tafiti juu ya mambo mbalimbali ya kibunge...
Hata mimi nimemuungaa mkono kabisa Mheshimiwa waziri katika hili kwa kuusema ukweli bila hofu wala uoga.
 
CCM Ndio imeendelea kuwatetea watumishi wa umma ili serikali iangalie upya suala la kikokotoo ambalo limeonekana kuwa mwiba mkali kwa watumishi wa umma wanaostaafu.
MKUU KUNA KIPINDI CHOCHOTE AMBACHO ccm HAIJAWAHI KUWA MADARAKANI BAADA YA UHURU ? NA JE WAAJIRIWA WANATESWA NA CHADEMA AU CUF ?
 
MKUU KUNA KIPINDI CHOCHOTE AMBACHO ccm HAIJAWAHI KUWA MADARAKANI BAADA YA UHURU ? NA JE WAAJIRIWA WANATESWA NA CHADEMA AU CUF ?
Sheria inaweza kupitishwa kwa dhamira njema na baadaye ikaonekana kuwa mzigo kwa watu. Ndio maana kunafanyika marejeo na masahihisho kuendana na wakati.
 
Ndugu zangu Watanzania,

Waziri wa Fedha Mheshimiwa Daktari Mwingulu Lameck Nchemba Amewataka Waheshimiwa Wabunge pamoja na watanzania wote kujenga utamaduni wa kujadili sheria wakati wa mchakato wa Utungwaji wake na siyo wakati wa utekelezaji wake.

Ameyasema hayo kutokana na swali lililoulizwa na Mbunge wa Mbozi Mheshimiwa George Ranwell Mwenisongole aliyetaka kujuwa na kufahamu ni kwanini vyama vya ushirika vinalazimishwa na TRA kununua na kuwa na mashine ya EFD wakati havifanyi biashara na huuza mara moja tu kwa mwaka.

Akijibu swali hilo Mheshimiwa Dkt Mwigulu amesema kuwa Ukusanyaji wa kodi unafanyika kwa mujibu wa sheria namba 36(1) ya usimamizi wa kodi ya mwaka 2015. ambapo ni lazima mfanyabiashara anayesambaza bidhaa au kutoa huduma au kupokea malipo kutokana na malipo ya huduma aliyotoa anatakiwa kutoa risiti za kieletroniki.

Lakini pia amesema ya kuwa sheria inasema kuwa mfanyabiashara yeyote anayefanya mauzo ghafi ya millioni 11 na kuendelea kwa Mwaka anapaswa kuwa na mashine ya kielektroniki EFD. Ameendelea kusema ya kuwa lengo ni kuhamasisha utunzaji wa kumbukumbu ambapo EFD ni njia nzuri na rahisi yenye ufanisi mzuri wa utunzaji wa kumbukumbu kwa mfanyabiashara.

Amesema pia kuwa haiwezekani mwalimu wa shule ya msingi atozwe kodi halafu aende aachwe tajiri.au mtu mwenye kipato cha chini cha mauzo chini ya Millioni 3 kwa mwaka atozwe na kulipishwa kodi halafu aende aachwe anayepokea malipo ya millioni Mia Moja.Amesema hii haiwezekani na siyo haki. Na kwamba mwezi ujao bunge litajadili pia masuala ya Kodi ,hivyo kama kuna sheria wabunge wanaona haifai basi ndio wakati wa kuijadili ili kuangalia kama itolewe au kufutwa au kufanyiwa marekebisho.

Mimi Mwashambwa Lucas ningependa kusema ya kuwa Waheshimiwa wabunge wetu wawe na utaratibu mzuri wa kujisomea,kutafiti,kuomba ushauri na kusikiliza wananchi wanasema nini wakati wanapokuwa wanajadili na kupitisha sheria fulani Bungeni itakayotumika kwa wanachi na Taifa kwa ujumla wake.

Nasema hili kwa kuwa imekuwa inasikitisha sana ,kuleta aibu , kufedhehesha,kuonyesha kukosa umakini na kutoelewa kwa undani kile wanachokipitisha ndani ya Bunge. kwa sababu ni kawaida unakuta sheria fulani inapita kwa kishindo na kwa kura zote za ndio, halafu baada ya muda wananchi wakianza kulalamika na kukosoa sheria husika mitaani unaona kuna wabunge wanaanza kushangaa kana kwamba ni kitu kigeni masikioni mwao na wala hawajawa kukisikia wala kushiriki katika mjadala wake wala kuunga mkono.

Jambo linaloonyesha aidha waheshimiwa wabunge wanakuwa wakati mwingine hawajapitia vifungu vyote na makabrasha yote yaliyo mezani pao kujuwa maana ya kile wanacho kipitisha na kukiunga mkono. Wakati mwingine mpaka unajiuliza inakuwaje mwananchi wa kawaida aone kwa haraka na ndani ya muda mfupi tatizo la sheria fulani ,halafu Mbunge anayekaa bungeni na kulipwa posho kwa ajili ya kazi hiyo ashindwe kuona tatizo hilo mpaka anapokuja kuona wananchi wakilalamika na kukosoa kwa nguvu na ndipo sasa naye Mbunge aanze kulaumu na kulalamika kana kwamba hakuwepo wakati wa utungaji na upitishwaji wake?

Tatizo nini nini? Shida inakuwa wapi? Kwanini hili linatokea kwa sheria inatungwa leo halafu kesho inakuwa inahitaji mabadiliko na marekebisho? Ni wapi panakosekana umakini? Ni nani hatekelezi wajibu wake? Je, waheshimiwa huwa wanapigia makofi na kuunga mkono mambo wasiyo yajua? Nini kifanyike hali hii isiwe inatokea? Kwa sababu tumeona jambo hili katika suala la kikokotoo ambapo wabunge wakiwa wakali kana kwamba siyo wao waiopitisha na wala hawajawahi kushiriki katika mjadala wa aina yoyote ile unaohusu kikokotoo.

Naweka kalamu yangu chini na kuishia hapa, sitaki kuwachosheni. Lakini tujiulize pia kwanini walipa kodi Tanzania ni wachache sana kuliko idadi ya watu wanaostahili kulipa kodi? Kwanini watanzania hawapendi kulipa kodi na hutafuta njia za kukwepa kulipa kodi kuliko kwenda kulipa kwa hiyari? Je ni kutokutambua umuhimu wa kodi kwa maendeleo ya Taifa letu? Je, ni kutokujua kuwa nchi inaendeshwa kwa kodi na kila kitu tunachotaka kufanyiwa na serikali yetu kinatokana na kodi zetu, ambazo tunatakiwa tuone fahari kulipa badala ya kuwa wakwanza kutengeneza mifumo ya Ukwepaji kodi.

Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa.Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
ephen_ wee ni nyau
 
Wabunge wa CCM ni wajinga sn wao huwa hawasomi zaidi huwa wanashangilia na kupitisha hata hawajui kilichomo, Ndugai amewahi kushangaa sheria kama ilipita bungeni na wakati yeye alikuwa Spika. Jinga sn
 
Back
Top Bottom