TANZIA Dkt. Mleoh wa Wizara ya Afya afariki Dunia

TANZIA Dkt. Mleoh wa Wizara ya Afya afariki Dunia

Taarifa iliyotolewa na Wizara ya Afya inaeleza kwamba Dkt Liberate Mleoh alipata ajali akitokea Mkoani Songwe kwenye Mazishi ya Ofisa mwingine wa Wizara hiyo.

Namfahamu Marehemu, alikuwa Mtu Mwema, Namuomba Mungu Aipokee Roho yake, Amina

View attachment 3273015
Kwa kweli mwezi huu wa 3 kama unakitu vile...
Hao watu walokuf mwezi huu tuu ninaowafahamu ni wengi sana.
Acha hao nisiowajua
 
17.3.2021 pia kilikuwa kilio kikubwa nchini.
Hili jinamizi la March, ni mbaya sana
 
Pole sana wanafamilia. Japo sikuwahi kumfahamu lakini kwa kuwa ni mwanadamu mwenzetu, tunayajua machungu ya wanafamilia, ndugu na marafiki. Tunamwomba Mungu awajalie moyo mkuu ili kuyapokea magumu haya kwa moyo wa imani.

NB: Madereva wa Serikali na taasisi zake, wanaendesha magari ovyo sana.

USHAURI: Maafisa wa Serikali wanaokuwa abiria kwenye magari ya Serikali wanatakiwa kuwa wakali dhidi ya madereva wanaoendesha hovyo. Dereva akipuuza malalamiko yako, amua kushuka kwenye hilo gari.
 
Back
Top Bottom