Dkt. Kipilimba, sasa yatosha!

Kazi ya TISS sio kuangalia ndege bali ni kuangalia Usalama wa nchi kwa ujumla.
Tatizo vitu vidogo tunavikuza kana kwamba vina umuhimu kuliko Watanzania zaidi ya 50Million.
Ndege imekamatwa kama bond ya fidia/deni la zamani enzi ya uhujumu uchumi na utafishaji,sasa inahusiana vipi na TISS.?
Kama yapo madeni yanayohitajika kulipwa walipwe, na sisi kama Taifa kama tunadai mahala nasi tulipwe ili tuendelee kuwalipa wanao/watakao tudai.
 
Mkuu huyu msiba ni TISS na Kipilimba ndio anamtuma

Cyprian Musiba siyo TISS na wala DG Kipilimba hamtumi ila yupo Mtu muhimu nchini Tanzania kwa Kushirikiana na Mwanae Mmoja Kiongozi Mpumbavu fulani kwa Kushirikiana na Watendaji wa Idara wasio na Maadili ndiyo wanamtumia Cyprian Musiba huku wakimlinda na kumjaza Kiburi. Kwa sasa huyu Cyprian Musiba anatumia huu mwanya wa kuwa karibu na hao Watu wawili ( ambao kwa sasa wanadhani kuwa Tanzania yote ni Mali yao kama Ng'ombe zao ) walizoziacha huko Vijijini Kwao na Kuwatishia Watu kuwa nae ni mwana Usalama wa Taifa na bahati mbaya wapo Watu wanaoamini kuwa Yeye ni mwana Idara ( TISS ) wakati wala hayupo huko na hana hata Sifa mojawapo ya kuwa mwana TISS. Nasisitiza tena Cyprian Musiba siyo mwana TISS. Tatizo kubwa DG Kipilimba ni Kukubali Kutumiwa na Wanasiasa hasa wa Chama Kimoja kwa Maslahi yao huku akijua kabisa kuwa ni Kinyume na taratibu za Kanuni Kuu ya hiyo Idara Nyeti na Muhimu katika nchi. Mtamlaumu sana DG Kipilimba ila ukweli ni kwamba walishamtega katika Tego lao na Yeye kwakuwa hana Ukomavu kivile wa Ujasusi ( zaidi ya ule wa mambo ya IT ) pekee nae akauvagaa huo Mtego na sasa wanamtumia wanavyotaka.
 
Acheni siasa na mihemko.

Imani yangu kwa idara ni kubwa mno.
Lakini ukweli ni kuwa haijawahi kuwa imara au mahiri kuliko Mossad au CIA au MI6, tuwe wakweli tushauri ukweli tuache kupotosha.

Huyo Kaburu hayupo peke yake ktk kuratibu na kutekeleza hili tukio, kama umesoma ile email kwenda kwa Kabudi basi utajua Steyn nae alikuwa anapewa 'intel' na watu flani wenye kuweza kupata taarifa nyeti za yanayoendelea chini ya zuria ndani ya serikali.

Kaburu ana tentacles nyingi na ndefu kuweza kufanya aliyofanya. Kuna sponsor wake nyuma ya pazia.
 

Sikupenda nitoe comment kwenye uzi huu lakini naona ni vema mambo kadhaa yawekwe wazi...unajuaje kuwa TISS hawakujua lolote kuhusu huyo mzungu wa Afrika Kusini? Halafu kwa ushahidi upi kwamba TISS imejaa UV-CCM na kwamba eti TISS imegeuzwa kuwa ya kisiasa kwa faida ya CCM?? Allegations za aina hii ni very serious you have to substantiate with facts...Of course TISS wanaweza wakawa na mapungufu yao kama taasisi lakini tuwe na uhakika wa kile tunachosema au kuandika dhidi ya taasisi hiyo...tusiropoke tu na kuipakazia mambo mbalimbali...
 
admin futa huu uzi, nakuomba, huyu ni mpinzani aliyeandika.
hii idara iachwe, haijadiliwi hadharani, huyu Kipilimba ana weledi uliotukuka, tumwache.
 
Au wewe ndie Kitine mwenyewe umeamua kumfundisha/kumkumbusha kijana majukumu yake dhidi ya nchi yake na sio ccm? Hongera sana mkuu
 
Akili za awamu ya tano ndio zimegotea hapo wala usijiulize zaidi ndugu, jiwe anafikiri nguvu anayoitumia dhidi ya vyama vya upinzani nchini basi anaweza kulazimisha jambo kupitia nguvu badala ya haki.
Yaani muandamanaji mmoja amebeba bango eti Nyie Wasauzi tuliwasaidia kuwashinda makaburu duh!

Sasa ina maana kama uliisaidia nchi kupata uhuru ndo uingilie utaratibu wake wa kujiendesha kama taifa huru?
 

It seems some people who presume that they have read books and smart in administrations and investigative matters don’t know the work of TISS. I don’t see as to why you are castigating Dr Kipilima! Nchi kwa sasa inaingozwa vizuri sana kuliko vipindi wa awamu ya tatu na nne. Awamu hii ya tano mpaka sasa imefanya mengi na vyombo vyote vya usalama vinawajibika vizuri. Kumbuka Mwl Nyerere alituachia viwanda lukuki, alituachia mashirika ya umma yalikuwa yakiendeshwa vema, alituachia research institutes imara LAKINI yote/vyote vilifisidiwa!!!! Je kipindi hicho kulikuwa hakuna TISS ya kuishauri kuwa viongozi wa serikali walikuwa wanaingia mikataba ya kuuza nchi????? Leo hii, kipindi cha awamu ya tano, kwa sababu ya utendaji mzuri wa TISS Reli, Mawasiliano na mengine mengi yamerudishwa! Ninaimani pia nyumba walizojigawia zitarudishwa. Kwa hiyo hiyo maandishi yako ya kumlaumu Dr Kipilima au TISS ni akili za narrow minded people ambao hawaoni yanayofanywa na awamu ya tano! Mfano mzuri ilikuwaje pwani yote ya Tanzania pamoja na bandari ya Bagamoyo kuuzwa kwa China na Oman 2014 kwa kipindi cha miaka 200!!!! Kama siyo TISS ya Kipilima Rais Dr Magufuli angalijuaje? Wajerumani walitutawala kwa miaka 40, Waingereza miaka 30 na sasa 2014 viongozi wazawa walidiriki kutukabidhi kwa Oman/China kwa miaka karibu 200!!!!!
 
Rudia tena kusoma mada upya, Usilete tabia za ki CCM hapa
 
Wakati twiga wanapanda ndege,dawa za kulevya zimetapakaa kila kona,bandarini madudu kibao ,wafanyakazi hewa,madini kutoroshwa hovyo,ndio kipindi hicho TISS ilikua imara?
Acheni upumbavu for nothing,mmeshikwa pabaya na bado
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…