Wakati mwingine kifo huwa kina kitu kama msimu hivi, kikifika kitachukua watu mliokuwa pamoja either kazini, nyumbani, au mtaani, hasa kama mkiwa na umri unaokaribiana.
Basi ataanza kuondoka wa kwanza kwenye kundi, kisha atafuatia mwingine, baadae tena atafuata mwingine list inaenda mpaka waishe wote.
Kama ni nyumbani, basi ataanza kuondoka kaka mkubwa, atafuatia mdogo wake, atafuatia mwingine...
Ukifuatilia kwa makini hapo ndani ya miaka mitano au sita, unaweza kukuta kundi fulani limesafishwa na kifo, baada ya hapo upepo unatulia kwa wale watakaobahatika kubaki, ambao wataondoka mmoja mmoja mbele ya safari.
Dr. Ibrahim Msabah amefariki muda mfupi uliopita Muhimbili. Katika uhai wake, Msabaha alishawahi kuongoza wizara ya nishati na madini mwaka 2006 mpaka 2007 kama waziri.
Dkt. Msabaha alikuwa rafiki wa karibu wa Hayati Edward Lowassa.
Hapana mkuu hawa walikuwa watu wadogo sana hawakuwa na nguvu kwenye siasa za tanzania ndio maana mambo yalivyokuwa mengi alijiuzulu akawaachia wenye nguvu zao, na hata bungeni aliweka wazi kuwa yeye ni anapokea orders kutoka juu haisiki na mambo hayo , hata report ya mwakyembe ilimuweka huru, alikuwa hana makuu wala sio mpenda madaraka au mroho kwa hilo naweza kumtetea
Dr. Ibrahim Msabah(72) amefariki muda mfupi uliopita Muhimbili. Katika uhai wake, Msabaha alishawahi kuongoza wizara ya nishati na madini mwaka 2006 mpaka 2007 kama waziri.
Dkt. Msabaha alikuwa rafiki wa karibu wa Hayati Edward Lowassa.