Just Pray
JF-Expert Member
- Nov 7, 2023
- 2,142
- 4,779
Rais Samia Suluhu Hassan amemteua Dkt. Delilah Kimambo kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH).
Kwa taaluma, Dkt. Kimambo ni daktari bingwa wa magonjwa ya moyo, na anachukua nafasi ya Profesa Mohamed Janabi ambaye alichaguliwa kuwa Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Kanda ya Afrika.
Kabla ya uteuzi huu, Dkt. Kimambo alikuwa Mkurugenzi wa Huduma za Uchangiaji Tiba katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI).
Ana shahada ya uzamili ya sayansi katika magonjwa ya moyo kutoka Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS), pamoja na shahada ya uzamili ya udaktari kutoka chuo hicho hicho.
Simiyu
16 Juni, 2025
(1) Dkt. Delilah Charles Kimambo ameteuliwa kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili. Dkt. Kimambo anachukua nafasi ya Prof. Mohamed Yakub Janabi aliyechaguliwa kuwa Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Kanda ya Afrika;
(ii) Jaji Mstaafu Hamisa Hamis Kalombola ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Umma kwa kipindi cha pili;
(iii) Bw. Paul Thomas Sangawe ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mfuko wa SELF kwa kipindi cha pili,
(iv) Jaji Rose Ally Ebrahim ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Ushindani (Fair Competition Tribunal); na
(v) Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk amepangiwa kuwa Balozi wa Tanzania nchini Italia.
Sharifa B. Nyanga
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu
Kwa taaluma, Dkt. Kimambo ni daktari bingwa wa magonjwa ya moyo, na anachukua nafasi ya Profesa Mohamed Janabi ambaye alichaguliwa kuwa Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Kanda ya Afrika.
Kabla ya uteuzi huu, Dkt. Kimambo alikuwa Mkurugenzi wa Huduma za Uchangiaji Tiba katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI).
Ana shahada ya uzamili ya sayansi katika magonjwa ya moyo kutoka Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS), pamoja na shahada ya uzamili ya udaktari kutoka chuo hicho hicho.
Simiyu
16 Juni, 2025
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi wa viongozi mbalimbali na kumpangia kituo cha kazi Balozi. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dkt. Moses Kusiluka, uteuzi huo ni kama ifuatavyo:-(1) Dkt. Delilah Charles Kimambo ameteuliwa kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili. Dkt. Kimambo anachukua nafasi ya Prof. Mohamed Yakub Janabi aliyechaguliwa kuwa Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Kanda ya Afrika;
(ii) Jaji Mstaafu Hamisa Hamis Kalombola ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Umma kwa kipindi cha pili;
(iii) Bw. Paul Thomas Sangawe ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mfuko wa SELF kwa kipindi cha pili,
(iv) Jaji Rose Ally Ebrahim ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Ushindani (Fair Competition Tribunal); na
(v) Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk amepangiwa kuwa Balozi wa Tanzania nchini Italia.
Sharifa B. Nyanga
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu