Dkt. Abbas aagiza watumishi wawili TSN kusimamishwa kazi

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,011
9,878
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Hassan Abbasi ametembelea Shirika la Magazeti ya Serikali (TSN) na kuagiza menejimenti ya taasisi hiyo kuongeza ufanisi kwani kuna watumishi wameanza kuonesha uzembe katika taasisi hiyo.

Katika ziara hiyo, Katibu Mkuu Dkt. Abbasi, ameagiza kusimamishwa kazi mameneja wawili wa idara za matangazo na usambazaji na eneo la uchapishaji ili kupisha uchunguzi wa tuhuma dhidi ya idara wanazoziongoza.

"Kila mtumishi wa umma kwa sasa na natoa wito kwa taasisi za Wizara ya Habari ambao najua wengine mlikuwa hamjazoea kuchukuliwa hatua mjue sasa ni saa za kazi; ukileta uzembe kazini utachukuliwa hatua bila kusita," alisema Dkt. Abbasi.
 
Yaani mnayapangia magazeti cha kuandika na cha kutoandika, yasiponunuliwa mnawaadhibu wauzaji? Hamna aibu kumbeee!!? Hivi nani anunue hazeti la mapambio huku ukweli anauona mitaani?

Hawa watu wa Jiwe hawaendi na wakati; siku hizi biashara ya magazeti imeshuka sana dunia nzima kwani watu wanapata habari kiganjani!! Sasa kuwafukuza watu kazi kwasababu magazeti hayauziki sio suluhisho ya tatizo ni kuonesha umbumbumbu!!!
 
Daily News died long time ago. Sidhani Kama Kuna mtu anayelinunua kwa raha zake
 
Alafu huyu Abass ufanyaji kazi wake ni kama mwanasiasa yaani utasema sio Katibu Mkuu...nadhani ndio katibu mkuu anaeongoza kwa longo longo labda kwa kuwa anahudumu kama Msemaji wa Serikali hivyo inafika mahali majukumu ya Ukatibu yanakuwa yamempita pembeni anajikuta anasimamisha watumish wa umma katika mfumo wa wanasiasa ili ku-gain umaarufu
 
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Hassan Abbasi ametembelea Shirika la Magazeti ya Serikali (TSN) na kuagiza menejimenti ya taasisi hiyo kuongeza ufanisi kwani kuna watumishi wameanza kuonesha uzembe katika taasisi hiyo.

Katika ziara hiyo, Katibu Mkuu Dkt. Abbasi, ameagiza kusimamishwa kazi mameneja wawili wa idara za matangazo na usambazaji na eneo la uchapishaji ili kupisha uchunguzi wa tuhuma dhidi ya idara wanazoziongoza.

"Kila mtumishi wa umma kwa sasa na natoa wito kwa taasisi za Wizara ya Habari ambao najua wengine mlikuwa hamjazoea kuchukuliwa hatua mjue sasa ni saa za kazi; ukileta uzembe kazini utachukuliwa hatua bila kusita," alisema Dkt. Abbasi.
Aiseee!
 
Back
Top Bottom