Dk Slaa: Sina mpango wa kuwania Ubunge Arumeru

Dk Slaa: Sina mpango wa kuwania Ubunge Arumeru

Patriote

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2011
Posts
1,718
Reaction score
1,047
KATIBU Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa amesema hana mpango wa kugombea ubunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki.Juzi, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alikaririwa akisema kama Dk Slaa ataamua kuwania ubunge katika jimbo hilo, chama kitaheshimu uamuzi wake akisema: “Katika suala la kugombea, utashi binafsi ni jambo la msingi... kama Dk Slaa ataamua kugombea ubunge Arumeru Mashariki, tutaheshimu uamuzi wake.”

Mbowe alisema Dk Slaa amekuwa akiombwa kugombea ubunge katika maeneo mengi ikiwemo Igunga na chama hakikuwahi kumlazimisha kwani jambo la kwanza ilibidi mwenyewe aonyeshe utashi binafsi wa kutaka kuwania kiti hicho.“Dk Slaa aliwahi kuombwa akagombee Igunga lakini hakwenda. Hii ni kwa sababu anakubalika karibu kote nchini, hivyo kama atakuwa na utashi binafsi kwanza, nadhani taratibu za chama zitatumika tu kufikia uamuzi,” alifafanua.

Lakini akizungumza katika mahojiano maalumu na Kituo cha Televisheni cha Mlimani jana, Dk Slaa alisema hafikirii kuwania ubunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki kwa kuwa kazi yake ni kukijenga chama kitaifa ili kiweze kupata wabunge wengi.

Alisema hawezi kujifunga kwenye jimbo moja wakati alishasema kuwa kazi yake ni kutetea wananchi wa Tanzania kwa ujumla kwa kukijenga chama chake.“Siwezi kujifungia kwenye jimbo moja, nilishasema kazi yangu ni kukijenga chama ili kiweze kupata wabunge wengi,” alisema Dk Slaa.

Source: Mwananchi

Maoni yangu

Namshkuru sana sana Dk. Slaa kwa kufanya maamuzi haya yenye busara, ni ukweli usiopingika kuwa hata angeamua kugombea asingeshindwa, ila tatizo lililopo ni hawa wenzetu wangefanya michezo yao ya kila aina ili Dk. apoteze ushindi ili wapate ya kusema. Dk. endelea kukijenga chama ili 2015 tuwe na wabunge wa kutosha na hata ikibidi tuishike nchi.
 
kwa sisi ma great thinker tunajua kuwa hawezi kushinda sasa anajikosha kosha tu hana lolote
 
  • Thanks
Reactions: Omr
After being put down by JK in the previous presidential vote, Slaa's appetite for public post seems to have been severely wrecked. That literally was the final time the priest-turned-politico ever contested election. Mbowe should get himself prepared to bear party's flag in the forthcoming poll because it is virtually impossible to prevail upon Slaa to re-think his decision. ,
 
Chadema ni chama chenye kuona mbali sana na nina uhakika mwaka 2015 Kitachukua nchi maana CCM wameshindwa kuwawajibisha mafisadi wao eti kinawaomba watafakari!! Sasa sisi tunasema CCM wawakumbatie mafisadi wao na Chadema kiwakumbatie wananchi.

Arumeru sasa tumeamua hatutachagua mtu bali tutachagua chama na chama chenyewe ni CHADEMA. Kwahiyo nyie msiumize kichwa tuleteeni mtu yeyote lakini asiwe muislamu. Sio kwamba hatutaki uislamu au tunawachukuia hapana kwani tunajua sote tunaabudu mungu mmoja ila tu kwasababu ya culture na eneo letu na ushawishi kwa mama zetu.

Kila mpenda amani anaipenda CHADEMA na tunaamini ukitaka maendeleo ya kweli ni lazima ubadilike kwani tukiendelea kuchagua CCM tutapata yaleyale ambayo hatujaridhika nayo.

CHADEMA Hoyeee.....
 
After being put down by JK in the previous presidential vote, Slaa's appetite for public post seems to have been severely wrecked. That literally was the final time the priest-turned-politico ever contested election. Mbowe should get himself prepared to bear party's flag in the forthcoming poll because it is virtually impossible to prevail upon Slaa to re-think his decision. ,
Umeandika ki Faiza Foxy bibie
 
After being put down by JK in the previous presidential vote, Slaa's appetite for public post seems to have been severely wrecked. That literally was the final time the priest-turned-politico ever contested election. Mbowe should get himself prepared to bear party's flag in the forthcoming poll because it is virtually impossible to prevail upon Slaa to re-think his decision. ,
"Kichenchede" (by Bigirita)
 
KATIBU Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa amesema hana mpango wa kugombea ubunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki.Juzi, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alikaririwa akisema kama Dk Slaa ataamua kuwania ubunge katika jimbo hilo, chama kitaheshimu uamuzi wake akisema: “Katika suala la kugombea, utashi binafsi ni jambo la msingi... kama Dk Slaa ataamua kugombea ubunge Arumeru Mashariki, tutaheshimu uamuzi wake.”

Mbowe alisema Dk Slaa amekuwa akiombwa kugombea ubunge katika maeneo mengi ikiwemo Igunga na chama hakikuwahi kumlazimisha kwani jambo la kwanza ilibidi mwenyewe aonyeshe utashi binafsi wa kutaka kuwania kiti hicho.“Dk Slaa aliwahi kuombwa akagombee Igunga lakini hakwenda. Hii ni kwa sababu anakubalika karibu kote nchini, hivyo kama atakuwa na utashi binafsi kwanza, nadhani taratibu za chama zitatumika tu kufikia uamuzi,” alifafanua.

Lakini akizungumza katika mahojiano maalumu na Kituo cha Televisheni cha Mlimani jana, Dk Slaa alisema hafikirii kuwania ubunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki kwa kuwa kazi yake ni kukijenga chama kitaifa ili kiweze kupata wabunge wengi.

Alisema hawezi kujifunga kwenye jimbo moja wakati alishasema kuwa kazi yake ni kutetea wananchi wa Tanzania kwa ujumla kwa kukijenga chama chake.“Siwezi kujifungia kwenye jimbo moja, nilishasema kazi yangu ni kukijenga chama ili kiweze kupata wabunge wengi,” alisema Dk Slaa.

Source: Mwananchi

Maoni yangu

Namshkuru sana sana Dk. Slaa kwa kufanya maamuzi haya yenye busara, ni ukweli usiopingika kuwa hata angeamua kugombea asingeshindwa, ila tatizo lililopo ni hawa wenzetu wangefanya michezo yao ya kila aina ili Dk. apoteze ushindi ili wapate ya kusema. Dk. endelea kukijenga chama ili 2015 tuwe na wabunge wa kutosha na hata ikibidi tuishike nchi.
Exactly! I expected such an answer from the allmighty His excellence Dr.WPS.
 
Uamuzi mzuri kwa manufaa ya chama na wanachama wake,endelea kujenga chama ili 2015 nchi izaliwe upya mikononi mwa wana-chadema,endeleza plogram Dr Slaa
 
..
After being put down by JK in the previous presidential vote, Slaa's appetite for public post seems to have been severely wrecked. That literally was the final time the priest-turned-politico ever contested election. Mbowe should get himself prepared to bear party's flag in the forthcoming poll because it is virtually impossible to prevail upon Slaa to re-think his decision. ,
MaximumMagambas at work,tatizo lenu nyie wana Magamba mnaiogopa Chadema pia mnamuogopa sana tena sana Dr WP Slaa na mjue imekula ndie tumtakae zaidi 2015
 
Nilitegemea kauli kama hii kwa kiongozi makini mwenye Maono ya mbali Mh Dr WP Slaa,unahitajika sana na waTz mkuu wangu Dr Slaa.
 
kwa sisi ma great thinker tunajua kuwa hawezi kushinda sasa anajikosha kosha tu hana lolote

tumesalitiwa,tumenyonywa, tumeisha,
dk ni kibiko chenu magamba,
how much are you paid, hata kama ni milioni hiyo kazi ya laana,wizi ,ubabe,dhuluma, kudanganya kamwe sitaikubali daima!
 
After being put down by JK in the previous presidential vote, Slaa's appetite for public post seems to have been severely wrecked. That literally was the final time the priest-turned-politico ever contested election. Mbowe should get himself prepared to bear party's flag in the forthcoming poll because it is virtually impossible to prevail upon Slaa to re-think his decision. ,

Dada, hivi una undugu na Mwita25 Mnafanana..
 
Bahati yake kaona mbele, hii ndio ingekuwa pigo la pili kwake.
 
Back
Top Bottom