Dk Slaa Mbumbumbu - Kamala

profession yangu ni Doctor of medicine, naomba kutoka kwenu wadau au ndugu zangu waliobobea kwenye maswala ya uchumi, mnisaidie nini maana ya GOVERNMENT SUBSIDE na nini maana ya VAT? NIMEPATA ELIMU YANGU CHINA, UKITEMBEA CHINA NZIMA BEI YA CEMENT NI MOJA TU. YAANI MFANO KAMA MWANZA NI TZSHS 5,000, BASI KIGOMA , MTWARA NA SEHEMU ZOTE ITAKUWA BEI HIYO HIYO NA AKIPATIKANA MTU ANAUZA KWA BEI JUU YA 5,000 NI KOSA LA JINAI NA LAZIMA UKATUMIKIE JELA. KAMA CHINA NI NCHI KUBWA HIVYO WAMEMUDU HIYO TANZANIA TUNASHINDWA NINI? TATIZO UCHUMI TUNAUSOMA KWENYE VITABU HATUNA PRACTICALS ZETU WENYEWE.
Mfano uliotumia si sahihi.China ni nchi ya kisoshalist na sisi ujamaa umetushinda.HIzo subsidies hatuzitaki,ni mzigo wa bure kwa serikali.
Kila mtu abebe mzigo wake.Slaa wa kwake na Kikwete wa kwake.Mwenye pesa ya kujengea nyumba abebe mfuko wake wa saruji.
 
Ametindikiwa mambo ya kusema msameheni Kamara wa watu apumzike siasa asubiri uteuzi wa rafiki yake JK
 
Leo, Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk Diodorus Kamala, alisema Dk Slaa katika uchumi ni mbumbumbu na inaonekana anazungumza asichokijua na kudanganya wananchi.

Dk Kamala alisema ahadi hiyo ni ya uongo kwani Sh 5,000 ni gharama ya usafirishaji wa mfuko kutoka Dar es Salaam hadi Mwanza kwa njia ya reli na tani moja ya saruji ya mifuko 20 ni Sh 100,000 hivyo gharama kwa mfuko kuwa Sh 5,000 sawa na bei anayowaahidi Watanzania. Alisema gharama za uzalishaji si chini ya Sh 7,000 kwa mfuko na kabla ya kuongeza gharama nyingine, mfuko wa saruji unapofika Mwanza gharama inakuwa zaidi ya Sh 12,000, hivyo kwa bei yake kuwa kubwa.

Dk Kamala alisema hoja hiyo ni ndoto ambayo hata viongozi wa nchi tajiri duniani hawatarajii kuiota mbali na kuitekeleza na huko ni kudanganya wananchi. Akizungumzia hoja ya makubaliano ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kwamba yanaumiza Watanzania, alisema Dk. Slaa anapotosha kwani msingi mkuu wa makubaliano hayo ni ushirikiano huo kujengwa hatua kwa hatua kulingana na ridhaa ya wananchi. "Serikali imekuwa ikizingatia msingi huu kikamilifu kwa kushirikisha wananchi, likiwamo Bunge ambalo Dk Slaa amekuwamo kwa miaka mingi, mfumo huu unaziwezesha nchi wanachama kupata fursa ya kujipanga vema katika utekelezaji na kuitumia ngazi moja kuwa msingi wa kupanda ngazi inayofuata ya utangamano," alisema Kamala.

Kuhusu mfumo wa kodi katika jumuiya, alisema si kweli kwamba aliuanzisha yeye, kwa kuwa yalianza kabla hajawa waziri na haiwezekani ushuru ufutwe bila kujadiliana na kukubaliana nchi wanachama, hivyo akasema Dk.Slaa hawezi kufuta ushuru huo kwani ni lazima ajadiliane na viongozi wa EAC.

Kuhusu viwango vya VAT alisema Dk. Slaa ameonesha hajui kuwa kodi hiyo si ya Afrika Mashariki na kiasi cha VAT anacholipa mlaji kinategemea bei ya bidhaa katika soko, huku akitolea mfano wa maji ya kunywa ya ujazo wa nusu lita, ambayo Tanzania yanauzwa Sh 500 na Kenya Sh 800 ingawa Mkenya analipa VAT ya asilimia 16 na Mtanzania asilimia 18; Mkenya analipa kiasi kikubwa kuliko Mtanzania.

Alisema kabla Dk. Slaa kusema Tanzania imeliwa, kwa kuwa na kiwango cha juu cha VAT Afrika Mashariki, alitakiwa kuelewa kwamba VAT si kodi ya Afrika Mashariki na katika uchumi, huwezi kulinganisha viwango vya VAT kabla ya kuangalia mfumuko wa bei kwenye nchi unazotaka kulinganisha, na kabla haujakokotoa, lazima uangalie viwango vya thamani ya kubadilisha fedha na gharama ya maisha.

Alimtaka Dk. Slaa kuwaomba radhi Watanzania kwa kuwadhalilisha akiwaita mbumbumbu, kielimu na katika kufanya biashara, huku akitaka kura zao, jambo ambalo si kweli, kwani miaka mingi Tanzania imekuwa kitovu cha elimu katika kanda hii huku viongozi wake wengi wakisoma Tanzania.

Sasa kama CCM Imeshindwa si ikae pembeni?

Kama CCM wameweza kupata mihela ya kutupa na kuamua kusambaza mabango kila sehemu nchi nzima, mabango ambayo hayaleti maendeleo yoyote kwa wananchi, Dr Slaa atashindwaje kupata fedha za ku'subcidise' bei ya sementi na vifaa vingine vya ujenzi kwa manufaa ya wananchi? Nijuavyo, CCM ni wafujaji wa mali ya umma ndiyo maana mtu akishauri kupunguza matumizi ya serikali ili kuboresha huduma za jamii, vigogo wake wanaona anayeshauri hivyo hajui uchumi! Kwani uchumi wa Dr Kamala yeye kasomea wapi, ambako wengine wameshindwa kwenda kujifunza huo uchumi? Tatizo la nchi yetu siyo upatikanaji wa fedha, ni namna gani hizo fedha zinatumika - finance management!
 
Kibunango, Dr. Slaa angekuwa mbumbumbu mamilioni ya WATANZANIA wasingemkubali na juu ya yote nyie asingewakosesha usingizi kama mnavyohaha hovyo wakati huu!!
Huyu bwana ni makini na anajua anasema nini, huwezi kumfananisha na jamaa yenu hajui hata sababu ya nchi anayoitawala kwanini ni maskini!!

A science project gone wrong.Think
 
wananchi wa jimbo lake hawakumwonea kumpiga chini kwenye kura za maoni
wailikuwa sahihi
nimeamini unaweza ukawa na elimu ya phd ukawa huna taaluma.

VOTE FOR SOMEBODY WHO IS ABOUT TO BRING CHANGES TO THE LOWEST CLASS PPL.
 
Huyo Alieko wa sisiem anamadem kiabo hapa A town au unataka picha zao na majumba wanayoporomosha???????????

KIHEREHER KIMEMEMPONZA HAKUNA ASIYEJUA GONJWA LINALOMSIBU. TATUMNYANYAPAI HATA HIVYO
 
Dr kamala, naomba nisadie kwanini Gharama ya kusafirisha sementi kufika mwanza ni sh. 5000 wakati Sementi inayoletwa kutoka Misri Pakistan na China inauzwa kwa bei ya chini kuliko inayozalishwa Dar, Ni Umbali, kodi, Umeme au?

Je sio busara kuongelea njia za kupunguza changamoto (kama zipo) ili bidhaa hizo zishuke bei?, Dr kamaala waziriwa afrika mashariki unayepiga debe ili kupata moja ya nfasi kumi za uteizini, kwanini unaongelea kuuza Mwanza, lakini hausemi hiyo Sementi yako kama unaweza kuizua kenya?
 
Yeye angekuwa na akili si angeaminiwa na wananchi wake kule jimboni? Mbona walimpiga chini pamoja na kuhonga? Atakuwa anawinda kuteuliwa!

Tena alimwagwa na mwanamke (Assumpta) wenyewe Kyaka (Jimbo Nkenge) wanaita mpishi wa rais (sijui kama ni kweli). Sasa ameanza kuwania nafasi za upendeleo na wanawake. Na mwaka huu hamzipati hata hizo kumi.
 
Kilaza KAMALAAAAAAAAA hivi unafikiri wenzako wanatumia kamasi kufikiri kama wewe, ukiona kitu Dr Slaa kakisema ina maana kakifanyia kazi kwa kina, Kamala ulikuwa waziri EAC lakini hukuwa na lolote zaidi ya kulala bungeni, au ndio umekula rushwa kuididimiza serikali na sasa umejenga Guest House Moro karibu na Keep left cha Kambarage? Unatetea ujinga wako eeeh, we katafute chaka bwana umeshachemsha EAC na kuingiza nchi kwenye matatizo tuliza ngende wanaume wafanye kazi.Kwenu wenyewe Nkenge hawakumind utamindiwa na watanzania uliowatusi kwa Mai na Museveni? Sepa kivyako bwna kabla hatujakuharibia pozi la kuhongwa PhD.Mbumbumbu na Popopopo mkubwa wewe.
 
Msameheni hajui asemalo. Hata hivyo, adhabu aliyopewa jimboni kwa inatosha (yabesha).
 
Kamala CCM hawakutaki njoo Chadema ule kuku

CHADEMA Haichukui watu wapumbavu, wezi na wazembe kama Kamala. Huyu sio Dr. tena kashaibwaga ile Phd feki. Viongozi wetu washamba sana ikija issue ya kujadili badala ya kutetea maslahi ya Tanzania wanashabikia kanuni za jumla za taasisis za nje. Ndiyo iliyotuponza wakati wa Mkapa na sera za Privatization na kuondoa huduma za umma za IMF na WB
.
 
Si mbumbumbu kwenye uchumi tu, hata katika maisha yake binafsi amejionyesha ni mbumbumbu... Utatembeaje na mke wa mtu bila kujua?

Hizo ndo hoja za kithithiem, wala hatushutuki, wanaounga mkono ssm ni vihiyo wa kutupwa, wanaburuzwa bila kutumia fikra zao, ukisha pewa 5000 na T- shirt, basi akili inahama.
 
kamala? aah sh..nz amefanya nini hadi leo hii?kwanza yeye nani hadi amuongelee slaa?sio mgombea, sio mpiga propaganda, so anajifurahisha tuu
 
Kama yeye hawezi wengine wanaweza hata darasani unaweza shindwa swali mwenzako akalifanya kwa dk moja.

"Dk Kamala alisema ahadi hiyo ni ya uongo kwani Sh 5,000 ni gharama ya usafirishaji wa mfuko kutoka Dar es Salaam hadi Mwanza kwa njia ya reli na tani moja ya saruji ya mifuko 20 ni Sh 100,000 hivyo gharama kwa mfuko kuwa Sh 5,000 sawa na bei anayowaahidi Watanzania. Alisema gharama za uzalishaji si chini ya Sh 7,000 kwa mfuko na kabla ya kuongeza gharama nyingine, mfuko wa saruji unapofika Mwanza gharama inakuwa zaidi ya Sh 12,000, hivyo kwa bei yake kuwa kubwa."
Hata hili unazi umetufanya tushindwe kulijadili?Au hesabu tatizo??
 
Halafu Mbumbumbu huyu anapenda mijimama...
slaa%26Rose.jpg


josepheni1.jpg
 
CHADEMA Haichukui watu wapumbavu, wezi na wazembe kama Kamala. Huyu sio Dr. tena kashaibwaga ile Phd feki. Viongozi wetu washamba sana ikija issue ya kujadili badala ya kutetea maslahi ya Tanzania wanashabikia kanuni za jumla za taasisis za nje. Ndiyo iliyotuponza wakati wa Mkapa na sera za Privatization na kuondoa huduma za umma za IMF na WB
.

Fools will learn at no other.Where's the contradiction coming from?Kazi sana
 
.....diverting from core issues to elementary entities is 1,000,000,000,000,000,000,000,000,000,000,000,000,000 times umbumbumbu!!!! anatoka kwenye mada ya cement na EAC analeta ishu ya 'mke wa mtu'. hii ina maana amemuelewa na kumkubali Slaa (PhD) hivyo hana comment katika mchakato mzima wa kushusha gharama za building hardware. anyway,in other ways, hao CCM wasiochukua wake za watu wamesaidia nini katika nation economy at large na social welfare? amka wewe!!!
 
Back
Top Bottom