Ernesto Sheka
Senior Member
- Oct 24, 2010
- 102
- 0
Hivi Kamala ni Dr. wa nini??
You're not an independent,mshabiki in hiding.
Hivi Kamala ni Dr. wa nini??
Mfano uliotumia si sahihi.China ni nchi ya kisoshalist na sisi ujamaa umetushinda.HIzo subsidies hatuzitaki,ni mzigo wa bure kwa serikali.profession yangu ni Doctor of medicine, naomba kutoka kwenu wadau au ndugu zangu waliobobea kwenye maswala ya uchumi, mnisaidie nini maana ya GOVERNMENT SUBSIDE na nini maana ya VAT? NIMEPATA ELIMU YANGU CHINA, UKITEMBEA CHINA NZIMA BEI YA CEMENT NI MOJA TU. YAANI MFANO KAMA MWANZA NI TZSHS 5,000, BASI KIGOMA , MTWARA NA SEHEMU ZOTE ITAKUWA BEI HIYO HIYO NA AKIPATIKANA MTU ANAUZA KWA BEI JUU YA 5,000 NI KOSA LA JINAI NA LAZIMA UKATUMIKIE JELA. KAMA CHINA NI NCHI KUBWA HIVYO WAMEMUDU HIYO TANZANIA TUNASHINDWA NINI? TATIZO UCHUMI TUNAUSOMA KWENYE VITABU HATUNA PRACTICALS ZETU WENYEWE.
Leo, Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk Diodorus Kamala, alisema Dk Slaa katika uchumi ni mbumbumbu na inaonekana anazungumza asichokijua na kudanganya wananchi.
Dk Kamala alisema ahadi hiyo ni ya uongo kwani Sh 5,000 ni gharama ya usafirishaji wa mfuko kutoka Dar es Salaam hadi Mwanza kwa njia ya reli na tani moja ya saruji ya mifuko 20 ni Sh 100,000 hivyo gharama kwa mfuko kuwa Sh 5,000 sawa na bei anayowaahidi Watanzania. Alisema gharama za uzalishaji si chini ya Sh 7,000 kwa mfuko na kabla ya kuongeza gharama nyingine, mfuko wa saruji unapofika Mwanza gharama inakuwa zaidi ya Sh 12,000, hivyo kwa bei yake kuwa kubwa.
Dk Kamala alisema hoja hiyo ni ndoto ambayo hata viongozi wa nchi tajiri duniani hawatarajii kuiota mbali na kuitekeleza na huko ni kudanganya wananchi. Akizungumzia hoja ya makubaliano ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kwamba yanaumiza Watanzania, alisema Dk. Slaa anapotosha kwani msingi mkuu wa makubaliano hayo ni ushirikiano huo kujengwa hatua kwa hatua kulingana na ridhaa ya wananchi. "Serikali imekuwa ikizingatia msingi huu kikamilifu kwa kushirikisha wananchi, likiwamo Bunge ambalo Dk Slaa amekuwamo kwa miaka mingi, mfumo huu unaziwezesha nchi wanachama kupata fursa ya kujipanga vema katika utekelezaji na kuitumia ngazi moja kuwa msingi wa kupanda ngazi inayofuata ya utangamano," alisema Kamala.
Kuhusu mfumo wa kodi katika jumuiya, alisema si kweli kwamba aliuanzisha yeye, kwa kuwa yalianza kabla hajawa waziri na haiwezekani ushuru ufutwe bila kujadiliana na kukubaliana nchi wanachama, hivyo akasema Dk.Slaa hawezi kufuta ushuru huo kwani ni lazima ajadiliane na viongozi wa EAC.
Kuhusu viwango vya VAT alisema Dk. Slaa ameonesha hajui kuwa kodi hiyo si ya Afrika Mashariki na kiasi cha VAT anacholipa mlaji kinategemea bei ya bidhaa katika soko, huku akitolea mfano wa maji ya kunywa ya ujazo wa nusu lita, ambayo Tanzania yanauzwa Sh 500 na Kenya Sh 800 ingawa Mkenya analipa VAT ya asilimia 16 na Mtanzania asilimia 18; Mkenya analipa kiasi kikubwa kuliko Mtanzania.
Alisema kabla Dk. Slaa kusema Tanzania imeliwa, kwa kuwa na kiwango cha juu cha VAT Afrika Mashariki, alitakiwa kuelewa kwamba VAT si kodi ya Afrika Mashariki na katika uchumi, huwezi kulinganisha viwango vya VAT kabla ya kuangalia mfumuko wa bei kwenye nchi unazotaka kulinganisha, na kabla haujakokotoa, lazima uangalie viwango vya thamani ya kubadilisha fedha na gharama ya maisha.
Alimtaka Dk. Slaa kuwaomba radhi Watanzania kwa kuwadhalilisha akiwaita mbumbumbu, kielimu na katika kufanya biashara, huku akitaka kura zao, jambo ambalo si kweli, kwani miaka mingi Tanzania imekuwa kitovu cha elimu katika kanda hii huku viongozi wake wengi wakisoma Tanzania.
Sasa kama CCM Imeshindwa si ikae pembeni?
Kibunango, Dr. Slaa angekuwa mbumbumbu mamilioni ya WATANZANIA wasingemkubali na juu ya yote nyie asingewakosesha usingizi kama mnavyohaha hovyo wakati huu!!
Huyu bwana ni makini na anajua anasema nini, huwezi kumfananisha na jamaa yenu hajui hata sababu ya nchi anayoitawala kwanini ni maskini!!
Yeye angekuwa na akili si angeaminiwa na wananchi wake kule jimboni? Mbona walimpiga chini pamoja na kuhonga? Atakuwa anawinda kuteuliwa!
Kamala CCM hawakutaki njoo Chadema ule kuku
Si mbumbumbu kwenye uchumi tu, hata katika maisha yake binafsi amejionyesha ni mbumbumbu... Utatembeaje na mke wa mtu bila kujua?
Kama yeye hawezi wengine wanaweza hata darasani unaweza shindwa swali mwenzako akalifanya kwa dk moja.
CHADEMA Haichukui watu wapumbavu, wezi na wazembe kama Kamala. Huyu sio Dr. tena kashaibwaga ile Phd feki. Viongozi wetu washamba sana ikija issue ya kujadili badala ya kutetea maslahi ya Tanzania wanashabikia kanuni za jumla za taasisis za nje. Ndiyo iliyotuponza wakati wa Mkapa na sera za Privatization na kuondoa huduma za umma za IMF na WB
.
Ametindikiwa mambo ya kusema msameheni Kamara wa watu apumzike siasa asubiri uteuzi wa rafiki yake JK